Peugeot 404 pikup Inauzwa

Peugeot 404 pikup Inauzwa

Tindo

Platinum Member
Joined
Sep 28, 2011
Posts
69,571
Reaction score
123,036
Peugeot 404 pikup inauzwa maeneo ya Arusha mjini, iko katika hali nzuri na inaweza kufanya vizuri sana hasa kwa watu wa mashambani na ina roho ngumu hasa kwa kubeba mizigo sokoni, minadani nk. Bei ya kutupa.
 
Sema bei mkuu tujipange

3.8 Millioni na kuna nafasi ya majadiliano ya ziada baada ya kuiona. Hiyo gari sio ya kusukumu iko tayari kwa kazi.
 
Ya mwaka gani?

Mkuu unauliza peugeot 404 ni ya mwaka gani, hilo ni gari la miaka ya nyuma ila ni roho ya paka. Ukiiona ndio utajua unapatania gari ya aina gani. Magari ya kuuliza mwaka ni IST, PRADO, VX, VOGUE nk. Hizi nyingine old model unaangalia hali ya gari maana sio la kuenda beach au kubebea harusi.
 
ss wakulima ndiyo tunayahitaji! mtoko ni kwenda mnadani
 
Peugeot 404 pikup inauzwa maeneo ya Arusha mjini, iko katika hali nzuri na inaweza kufanya vizuri sana hasa kwa watu wa mashambani na ina roho ngumu hasa kwa kubeba mizigo sokoni, minadani nk. Bei ya kutupa.

LAKINI SPARE ZAKE NI ZA KUCHONGA!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!1
 
LAKINI SPARE ZAKE NI ZA KUCHONGA!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!1

spare zake zipo na mafundi wake wapo tena vijana tu lakini wengi hawapungui miaka 30. Ni nadra kupata fundi wa gari hili mwenye miaka chini ya 25 maana sio la kukagua kwa computer.
 
Nitainunua ikae Kwenye makumbusho yangu home vijana wa Auto hawaijui hata ukimpa haendeshi.

Mkuu hilo gari lilikuwa la mzee wangu R.I.P, si unajua tena mambo ya urithi, alikuwa analipenda ile mbaya maana alikuwa anasema wale mateja wala unga hawana hata muda wa kuiba side mirror!! Ila linafanya kazi maana alikuwa analiendesha mpaka ilipofika mwezi may mwaka huu akawa amezidiwa kabla ya mauti. Shida yangu kubwa ni kumpata dereva hivyo nimeona niliuze maana sitaki stress na madereva. road licence yake imeisha tarehe 29-6-2016 hivyo ni ya kurenew inadaidwa laki 212,500 Tra, pamoja na insurance ni 105,000 tu.
 
Nitainunua ikae Kwenye makumbusho yangu home vijana wa Auto hawaijui hata ukimpa haendeshi.

Kuna mzungu mmoja Mfaransa alikuwa analitaka kwa mzee siku nyingi lakini akawa anagoma, si unajua tena kipendacho roho ..... Huenda na yeye alitaka kufanya kama wewe.
 
spare zake zipo na mafundi wake wapo tena vijana tu lakini wengi hawapungui miaka 30. Ni nadra kupata fundi wa gari hili mwenye miaka chini ya 25 maana sio la kukagua kwa computer.
MIMI NILIJIFUNZIA UDEREVA KWA VW BETTLE (.MGONGO WA CHURA)
 
Mr Tindo hiyo wanaiita Forofoo!ha ha ha ha!tupia kapicha kaka!
 

Attachments

  • IMG-20161015-WA0004.jpg
    IMG-20161015-WA0004.jpg
    171 KB · Views: 47
Back
Top Bottom