Wa Mjengoni
JF-Expert Member
- May 4, 2010
- 480
- 128
Mkuu,
Hiyo Sheria ilitungwa na Warioba?
Mtoto wa nyoka ni nyoka - Kama Katiba ni Sheria Mama inayoongoza sheria zote nchini kwa nini Rasimu yake (nimeiita mtoto) isiwe Sheria?
Mkuu,
Hiyo Sheria ilitungwa na Warioba?
Wakuu,
Huwezi kuamini lakini ndivyo ilivyotokea Mahakama Kuu ambapo Wakili Peter Kibatala alipoiambia Mahakama hiyo kwamba eti Rasimu ya Warioba ni Sheria. Watu tulikuwa tunajiuliza kwa nini UKAWA walikuwa wanakomalia sana Rasimu ya Warioba kumbe wenzetu waliamini kwamba hiyo ni Sheria.
Hayo yako kwenye kesi ya Saed Kubenea v. Attorney General, Misc. Civil Cause No. 28 of 2014 katika ukurasa wa 9 tunapata haya yafuatayo:
It was Mr. Masajus further argument that the Draft Constitution has no legal force, that it is a mere annex to the Commissions Report [relying on section 20 (1)] and can only serve as a working document. He wondered how could a document that is not part of the law be binding on the Constituent Assembly. Submitting on this point, Mr. Kibatala stated that the Draft Constitution was law and therefore binding.
Lakini Mahakama Kuu ilijibu katika ukurasa huo huo wa 9 kwa ujasiri kama ifuatavyo:
We would respectfully differ from both counsel on this point, though we differ more markedly from counsel for the petitioners position. We do not think that the Draft Constitution is law, as it has not been enacted into one.
Tunawashauri wana-UKAWA wakubali tu Hukumu ya Mahakama Kuu kwamba Rasimu ya Warioba ilikuwa sio Sheria bali ni "WORKING DOCUMENT" ili kutengeneza Katiba Mpya!
Pia Kibatala na usomi wake wote kuamini kwamba RASIMU YA WARIOBA ni SHERIA nalo linatupa mashaka sana na weledi wake!
Ni hayo tu kwa leo, karibuni kwa mjadala!
Kwa sababu sio Sheria!
chukua like mkuu!ndiyo ilikuwa sheria kwa sababu ilibeba maoni ya watz namna gani waongozwe na kuwadhibiti mafisadi. Lakn fisadi likakabidhiwa kuandika katiba na mafisadi menzie likatupilia mbali
Kwangu mimi naunga mkono hoja kwamba, katiba ya warioba ni sheria kuliko katiba pendekezwa. Sababu ni kwamba katiba pendekezwa imeandikwa na kina chenge mafisadi waliokubuhu. Wakati rasimu imeunganisha maoni ya watanzania juu ya katiba waitakayo!
Unga hauwezi kuwa ugali mpaka hatua zote za kusonga ugali ziwe zimepitiwa!
Umeandika meengi mazuri
Lakini kwa mfano kama huu umejidhalilisha!
Nadhani ulimaanisha ugali hauwi ugali hadi hatua zote za kusaga unga na kusonga zikamilike!
Ukishasonga ugali hupati tena unga-labda kwenu!
Mie naendelea kuamini kwamba kwa BMK, Rasimu ya TUME ilikuwa ni sheria kuu
Hiyo "Sheria" ilitungwa na Warioba?
Kwa hiyo kila unaposonga ugali lazima ukasage unga kwanza? Makubwa haya; anyway. Mzee Waryoba na team yake walikuwa wanaandaa tu rasimu ya katiba mpya. Kwa hivyo basi hii katiba (sheria mama) inayopendekezwa ni matokeo tu ya kazi akina Waryoba na mwisho wa siku baada ya wananchi kuikubali, ifikapo 2016 Tanzania itakuwa imepata katiba (sheria mama). Hata hivyo ni matumsini yangu kuwa wananchi wataikataa rasimu hii maana imeondoa mambo mengi ya msingi, muundo wa serikali.Umeandika meengi mazuri
Lakini kwa mfano kama huu umejidhalilisha!
Nadhani ulimaanisha ugali hauwi ugali hadi hatua zote za kusaga unga na kusonga zikamilike!
Ukishasonga ugali hupati tena unga-labda kwenu!
Mie naendelea kuamini kwamba kwa BMK, Rasimu ya TUME ilikuwa ni sheria kuu
Mkuu, tatizo tulilonalo ni kuwa WASANII katika kila jambo. Tume imeundwa kisheria sasa kwa nini kazi yake isiwe sheria?Imeandikwa wapi kuwa Rasimu ya Warioba ikisainiwa na Rais basi inakuwa Sheria?