Pesa mwanaharamu, hakuna pesa halali duniani usidanganyike

Pesa mwanaharamu, hakuna pesa halali duniani usidanganyike

Bonde la Baraka

JF-Expert Member
Joined
Sep 22, 2016
Posts
4,580
Reaction score
7,953
Acheni pesa iitwe pesa, kuna wakati pesa inaingia mfukoni mwako huku umeishiwa nguvu ukiwaza jinsi ulivyoipata.

Hakuna kitu kilichojificha duniani na mbingini kama pesa.

Mungu mwenyewe ukimtafuta kwa bidii unamuona ila pesa kuna watu wameanza kuitafuta ujanani mpaka uzeeni hawajaiona.

Pesa hata kama unaona umeipata kwa njia halali huyo aliyekulipa au kukupa hiyo fefha kaipata kwa njia isiyo halali.

Lazima kuna mtu au kampuni imenyonywa au kuibiwa.

Asubuhi mara chache chache huwa nakuwa Gerezani Kariakoo, nauona umati unatokea Mbagala, Gongo la mboto na viunga vya Temeke. Kila mtu akiwa busy na kasi ya ajabu kuingia Kariakoo kutafuta pesa.

Nitaiheshimu pesa daima
 
Ili mradi umeipata kwa njia halali basi kwako halali aliyekupatia huna haja ya kujua kaipataje kwani wewe polisi au mpelelezi?
 
Povu la Pesa !
Pesa halali IPO na uhalali unautengeza wewe unavyoipata.

Kama kuna mtu kaja kwangu kulipia huduma ninayoitoa wakati yeye hakuipata kwa halali ...Uharamu unaishia kwake na uhalali unaanzia kwangu.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Haijalaaniwa hayo ni mawazo ya kimaskini anayoambiwa na tajiri ili maskini aendelee kuwa maskini akiwaza kuwa akipata pesa atalaaniwa
Hujanielewa namaanisha nini.
Sijamaanisha kuwa tusiitafute kwa bidii, bali nimetazama impacts zake ktk jamii
 
Hujanielewa namaanisha nini.
Sijamaanisha kuwa tusiitafute kwa bidii, bali nimetazama impacts zake ktk jamii
Mwanadamu ndiyo chanzo cha yote hata siyo pesa. Mwanadamu kawa nyang'au hata kabla ya pesa kuanza kutumika. We are thr Gods we create and destroy
 
Pesa haramu huwa inatakatishwa na aliyepata kiharamu. Hivyo ikija kwa mwingine anayeihenyea wala haiwi haramu tena.
 
Pesa haina uharamu wowote ila unaweza kuifanyia matumizi haramu...
 
Hivi si karatasi zilipakwa rangi na kuandikwa maandishi? Kwanini zisitengenezwe nyingi na wenye shida zao wagawiwe?
 
Hivi si karatasi zilipakwa rangi na kuandikwa maandishi? Kwanini zisitengenezwe nyingi na wenye shida zao wagawiwe?
Pesa mbaya, mke au mume mnaweza kushibana na msifanye cheating but Dangote akimtaka mke wako unaweza ukajikuta umemruhusu achepuke naye bila kutarajia
 
"Fedha fedheha" huu msemo una maana gani?
 
Back
Top Bottom