Pesa halali ni ipi?

Pesa halali ni ipi?

Under-cover

JF-Expert Member
Joined
Nov 13, 2023
Posts
2,211
Reaction score
3,517
Wakuu naomba kuuliza, ivi pesa inayolipwa as mishahara kwa watumishi ni pesa unayopatikana ki halali?, mfano labda pesa zinapatikana kupitia kodi labda tuseme kodi iliyokusanywa katika makampuni ya michezo ya kubahatisha, sasa zichukuliwe zile pesa zije zitumike labda kulipa mishahara kwa watumishi.

Hapa kwa wale wanaoamini sana kuhusu dini na maandiko, kamari imekatazwa sawa, lakini serikali zetu zimeidhinisha na wanachukua kodi na kufanya mambo mbali mbali. Swali je hawa watumishi wanaopata hizo mishahara na kufanyia mambo yao katika maisha na kwenda mbele zaidi kutoa sadaka, vipi MUNGU anapokea pesa hizo?

Swali la nyongeza kamari ni dhambi kwa mujibu wa maandiko kwasababu ni kama kubahatisha ili uweze kutajirika, lakini kwani tukiangalia maisha ya sasa iv, mbona kila kitu ni kamari/ kubahatisha, iwe kupata kazi, kuvuna mazao nakadharika.

NAWASILISHA
 
Je wajua ,kilimo kwa Africa na biashara ni kama kamari tu?

Unaweka mbegu chini ukitegemea mvua mara isinyeshe mara inyeshe je ni dhambi ? Inatofauti gani na kuweka pesa kwa kubahatisha kwamba timu gani ishinde?

Umeweka uzi ukibahatisha utapata wachangiaji pia je ni dhambi?
 
IMG-20240627-WA1259.jpg
 
Je wajua ,kilimo kwa Africa na biashara ni kama kamari tu?

Unaweka mbegu chini ukitegemea mvua mara isinyeshe mara inyeshe je ni dhambi ? Inatofauti gani na kuweka pesa kwa kubahatisha kwamba timu gani ishinde?

Umeweka uzi ukibahatisha utapata wachangiaji pia je ni dhambi?
mkuu ndio hapo sasa nawaza hii inakuaje
 
Back
Top Bottom