Perfect strangers

Perfect strangers

my name is my name

JF-Expert Member
Joined
Jan 12, 2015
Posts
2,016
Reaction score
2,402
Perfect strangers ni muvi ambayo inazungumzia hasara za simu katika maisha ya mahusiano na maisha ya kawaida.

Hii muvi inahusu marafiki wanne na wake zao ambao wenyewe wanaamini wanafahamiana vizuri hawafichani kitu kila tukio baya zuri wanashare hamna siri kati yao. Wamekuwa wakifahamiana tangia utotoni wamekuwa pamoja.

Sasa siku moja wameamua kukutana pamoja. Walivyokutana wanaamua kucheza mchezo ambao kila mmoja anaweka simu mezani. Simu ikiita unaweka loud speaker kila mtu anasikia unachoongea. Mesej ikiingia unasoma kwa sauti kila mtu anasikia na anaona.

Ila kilichokuja kutokea yani yule mtu unaona unamfahamu vizuri hamfichani kitu kumbe Kiukweli humfahamu kabisa ni mtu mgeni kwako. Hata mke na mume ni wageni hawafahamiami 😂 maana kila mtu ana mambo yake mabaya au mazuri anayaficha na hakuna mtu anajuwa zaidi ya yeye mwenyewe tu. Hata mmoja wao katika kundi lao kumbe anatembea na mke wa mmoja wa rafiki yake 😂

Hii muvi imetolewa kwa mara ya kwanza nchini Italy 2016 kwa Jina la perfetti sconosciuti. Ilifanya vizuri katika box office nchini humo. Baadae kuna nchi zika remake hii movie na kila nchi iliyoremake mauzo yake pia yalikuwa mazuri ktk box office.

Nchi zilizo remake ni ugiriki kwa Jina la (Teleioi xenoi), Spain kwa Jina la (perfectos desconocidos), Turkey kwa Jina la (Cebimdeki Yabanci) na France kwa Jina la (Le jeu)

Hii muvi inaonesha uhusiano wa technology na mahusiano. Ni muvi nzuri sana na version zote nzuri. Nani yuko tayari kucheza huo mchezo na yule mtu unayemuamini sana na hamfichani kitu?

IMG_20190825_232724.jpg
 
Sipendi kuangalia movie zenye tafsiri ya maandishi, ubongo unakuwa na kazi nyingi kufatilia maneno ba uyatafsiri kwa lugha yangu ya kibantu kisha ufatilie na movement...

Wakitoa yenye tafsiri ya kiingereza ntaitazama.

With my phone, Dadii can have it for a whole year na siku ananirudishia atanitungisha mimba tuu. Sinaga mipango ya kando.

Yake sihitaji kuwa nayo, namhitaji yeye zaidi ya kujua anafanya nini nje ya upeo wa macho yangu.

Moyo wa mtu kichaka..
 
Yani wenyewe kwa akili zao fupi wakaamini kwamba mtu anaweza kukwambia mambo yake yoye anayoyafanya thubutuuuuu hasa kwenye simu..

Ina maana hawaelewi maana ya neno privacy? Wajinga kweli hao
Wapo kweli watu wa aina hiyo hasa wazungu wana amini. Mimi nilikuwa na bf mwanzoni tu ya relationship akaniambia sitaki uongo au siri kati yetu. Mara ya kwanza nilijuwa anasema tu kumbe mwenzangu yuko serious. Kweli alikuwa anifichi kitu. Na alikuwa muwazi sana Sometimes nilikuwa najisemea mwenyewe kwani lazima aniambie. Na mimi nikawa namwambia yangu hata nikimuongopea alikuwa anaamini. Aliniamini sana kiasi hata nikimwambia uongo anaamini na wala haoneshi kutoniamini.
 
Sipendi kuangalia movie zenye tafsiri ya maandishi, ubongo unakuwa na kazi nyingi kufatilia maneno ba uyatafsiri kwa lugha yangu ya kibantu kisha ufatilie na movement...

Wakitoa yenye tafsiri ya kiingereza ntaitazama.

With my phone, Dadii can have it for a whole year na siku ananirudishia atanitungisha mimba tuu. Sinaga mipango ya kando.

Yake sihitaji kuwa nayo, namhitaji yeye zaidi ya kujua anafanya nini nje ya upeo wa macho yangu.

Moyo wa mtu kichaka..
Ya kifaransa inapatikana netflix with english subtitles kwa Jina la nothing to hide. Kama kweli wewe ni muamnifu basi hongera ila mara nyingi watu kama nyie huwa hampati watu sahihi. Wewe mchunguze mwenzako utagundua tu.
 
Wapo kweli watu wa aina hiyo hasa wazungu wana amini. Mimi nilikuwa na bf mwanzoni tu ya relationship akaniambia sitaki uongo au siri kati yetu. Mara ya kwanza nilijuwa anasema tu kumbe mwenzangu yuko serious. Kweli alikuwa anifichi kitu. Na alikuwa muwazi sana Sometimes nilikuwa najisemea mwenyewe kwani lazima aniambie. Na mimi nikawa namwambia yangu hata nikimuongopea alikuwa anaamini. Aliniamini sana kiasi hata nikimwambia uongo anaamini na wala haoneshi kutoniamini.

Huyo bf naye hana akili nawewe mkuu ilibaki kidogo ukose akili bahati yako wewe ulikua unamdanganya
 
Huyo bf naye hana akili nawewe mkuu ilibaki kidogo ukose akili bahati yako wewe ulikua unamdanganya
Sio kukosa akili ni misingi yao waliojiwekea, wakiwa na mtu wao wa karibu kunatakiwa kusiwe na siri kati yao. Na ikitokea usimwambie halafu akaja kujuwa mwenyewe hata ukaribu au urafiki wenyewe unaweza kuisha.
 
Back
Top Bottom