Nuoxian
Senior Member
- Mar 15, 2020
- 169
- 237
Baada ya Arsenal kuchezea kichapo cha goli moja kwa bila dhidi ya Nottingham forest ni rasmi ubingwa wa ligi kuu uingereza msimu wa 2022/2023 unakwenda kwa manchester city ambaye anajumla ya point 85 huku anaemfuata Arsenal akiwa na point 81 na amebakiwa na mchezo mmoja mkononi ili kumaliza ligi wakati man city yeye akibakiza michezo miwili.
Ubingwa huu aliochukuwa man city chini ya kocha Pep Guardiola utakuwa ni ubingwa wao wa tatu mfululizo kuchukua chini na Kocha Pep Guardiola akifanya ivyo msimu wa 2019/2020, 2021/2022, 2022/ 2023 Wakati huo huo man city bado yupo kwenye mbio za kugombania makombe mengine fainali kombe la FA Ambayo atamenyana na Manchester United, fainali ya Uefa champion league dhidi ya Inter Milan, Kiufupi Guardiola ameshindikanika.
Licha ya makombe anayozidi kuyakusanya katika club mbalimbali pia guardiola ni kocha anayesifika kwa kufundisha mpira unaovutia kwa watazamaji mpira wa pasi nyingi, ikumbuke ile Barcelona ya akina Iniesta, Xavi na Lionel Messi, ilikuwa ni hatari mpaka Furgeson anatetemeka mikono . Kumbuka jinsi alivyoweza kuibadilisha Beyern Munich kutoka kwenye piga tukimbizane mpaka mpira wa pasi nyingi.
Haya ni baadhi ya makombe makubwa aliyowahi kuyachukua Mtaalam Pep Guardiola.
1. Uefa champion league..... ×2
2. Uefa Supercup....×3
3. Spanish (Laliga)......×3
4. England premier league.......×5
5. Bundersliga..........×3
6. Fifa club world cup......×3
Ubingwa huu aliochukuwa man city chini ya kocha Pep Guardiola utakuwa ni ubingwa wao wa tatu mfululizo kuchukua chini na Kocha Pep Guardiola akifanya ivyo msimu wa 2019/2020, 2021/2022, 2022/ 2023 Wakati huo huo man city bado yupo kwenye mbio za kugombania makombe mengine fainali kombe la FA Ambayo atamenyana na Manchester United, fainali ya Uefa champion league dhidi ya Inter Milan, Kiufupi Guardiola ameshindikanika.
Licha ya makombe anayozidi kuyakusanya katika club mbalimbali pia guardiola ni kocha anayesifika kwa kufundisha mpira unaovutia kwa watazamaji mpira wa pasi nyingi, ikumbuke ile Barcelona ya akina Iniesta, Xavi na Lionel Messi, ilikuwa ni hatari mpaka Furgeson anatetemeka mikono . Kumbuka jinsi alivyoweza kuibadilisha Beyern Munich kutoka kwenye piga tukimbizane mpaka mpira wa pasi nyingi.
Haya ni baadhi ya makombe makubwa aliyowahi kuyachukua Mtaalam Pep Guardiola.
1. Uefa champion league..... ×2
2. Uefa Supercup....×3
3. Spanish (Laliga)......×3
4. England premier league.......×5
5. Bundersliga..........×3
6. Fifa club world cup......×3