Penzi la mke wa mtu....

MR. DRY

JF-Expert Member
Oct 5, 2011
637
122
Nimebahatika kuwa karibu na familia moja yenye mke(age 40's)+mme+watoto+wajukuu, mme ni mtu anayesafiri mara kwa mara mikoani. Ukaribu wangu kwao ukapelekea wakiface tatizo wanajaribu kuniomba kama ninauwezo nalo(mtoto na mjukuu wake waliumwa vipindi tofauti nikatoa msaada sio mara moja).mzee akiwa safarini akapewa(shangazi+mjomba wa mke) taarifa mimi natembea na mke wake! Ikapelekea akirudi anampiga sana mke wake na mzee kupunguza pesa ya matumizi. Siku 1 mtoto kaumwa kupelekea kulazwa, mme yuko safarini pesa ikawa imepelea, akamwambia mke aniombe mimi kiasi cha kujazia, bila iyana nikampatia.
Nikamwambia isije ikaendeza matatizo yenu.
Akajibu mzee atanirudishia.
Siku mme akapata muda kama miezi miwili kupumzika nyumbani, mida ya jioni akapigiwa simu na mjomba wa mke kuwa mimi nilikuwa nae mjini!mme kushanga muda aliotajiwa mke wake alikuwa nyumbani ndipo alipoanza kupata ukweli wangu kwa mke wake.
Akanitafuta siku 1 na kunieleza mambo meeengi pia kunirudishia laki 130 nilizotumia na nyongeza ya elfu 20. KUNIAMBIA WEWE NI KIJANA MWEREVU SANA SIKUWA NAELEWA. Tokea hapo tukawa zaidi ya rafiki naendelea kumpa heshima zote.

Mke+mtoto wakaenda kwa mjomba+shangazi kuwapiga kwa kuwachonganisha na mme/baba w/yake.
Mke akanifuata na kuniomba msamaha.
Cha ajabu anasema amepigwa sana kwa ajili yangu mimi kwa kosa la uongo anachotaka/analazimisha yeye kufanya mapenzi na mimi ili aridhike/kujipooza kwa machungu ya kipigo.
Anasema nitafute siku twende nae mjini kutafuta hotel(mida ya saa 5 hadi jioni ndo turudi)
nikamwambia mimi sitaweza kufanya mapenzi na wewe kwani itakuwa ni hasira unazo,endapo ametulia na mme wake ndo nitamkubalia.
Wadau huyu mke amening'ang'ania nifanye nae mapenzi.
Maswali: mahusiano yangu na mme wake yatakuwa kwenye hali gani?
Naweza kumkwepa vipi?
Mawazo yenu yataniweka katika upeo mwingine.

Incase kunatopic inayo-relate na hii unaweza kuniwekea link.
Msaada wenu wana MMU.
 
kimbia upesi kama una akili.
Ila kama vya arusha viko kichwani unajilipa afu unatapa kazi ya kumchenga muweze forever sababu hutaweza kumtizama machoni tena. Kama ulipo ni nyumba ya kupanga unahama kabisa ila kama umejenga unatoboa emergence door upande mwingine.
 
Jitoe mhanga tu uoene kazi ya kudandia wake za watu, kwani hujui kumtishia mtu anayekulazimisha? Ita afande kula kula !!!!!!!!!!!
 
Acha uzembee weweeee
Kamua mautamu hayo, alaaaaah.....unakuwa ka sio kinega?



Il Gambino.
 
kimbia upesi kama una akili.
Ila kama vya arusha viko kichwani unajilipa afu unatapa kazi ya kumchenga muweze forever sababu hutaweza kumtizama machoni tena. Kama ulipo ni nyumba ya kupanga unahama kabisa ila kama umejenga unatoboa emergence door upande mwingine.

mkuu yeye anakaa kwake ila mimi ni jirani yake nymba zimepakana.
Vitu vya arusha havipanti kabisa, kipi kingine nifanye?nukta
 
Be a real man...thibitisha kwa vitendo kwamba ulichotoa ni msaada na haikua hisani! Masikini baba wa watu keshakuomba msamaha kiutu uzima na kukupa werevu uliotukuka,leo unathubutu kupokea ofa ya 'kutuliza hasira za mama?...then kwa maelezo yako ya awali seem bi mkubwa huyo ni mtu mzima kwako hivyo pamoja na mambo mengine epuka laana kijana...kimbia!
 
Be a real man...thibitisha kwa vitendo kwamba ulichotoa ni msaada na haikua hisani! Masikini baba wa watu keshakuomba msamaha kiutu uzima na kukupa werevu uliotukuka,leo unathubutu kupokea ofa ya 'kutuliza hasira za mama?...then kwa maelezo yako ya awali seem bi mkubwa huyo ni mtu mzima kwako hivyo pamoja na mambo mengine epuka laana kijana...kimbia!

hapo ndo kinacho nishangaza kwa huyu mke anasisitiza nia ni kufanya kweli!
Je heshima na utu wangu nitaenda kuununua wapi tena pindi mme akijua?nukta
 
Hulazimiki kufanya chochote nae. . . .
Kama kweli hutaki mjulishe huna muda huo na ukae nae mbali.

kama umenisoma vizuri, nimemweleza hicho kitu sitaweza kufanya. Ndo ikabidi nimdanganye mpaka hapo watakapo kuwa sawa na mme wake.
This time anakuja nakusema wako ok and yuko ready kunipa penzi la kweli.
 
Isijekuwa umeshaonja ndio unakuja kutaka ushauri? - lol.
Fikiria iwapo huo mpango kausuka yeye na mume wake au mtu wake wa karibu?
Ninakuusia, mwanamke huyo usimwamini hata kidogo, mkwepe, mkimbie kama upupu.
Msaada wako usijekukutumbukia nyongo, au unataka tukuite marehemu mtarajiwa?
 
Mkuu km hukuzaliwa kwenye vijiji vya ujamaa utakua umewahi kuangalia katuni za Tom & Jerry....hapa ni km tunajaribu kukunasua kwenye bomu ilihali unatamani kulikumbatia...keep going mkuu! Uu mtu mzima kufanya maamuzi makubwa pasi kuomba ushauri so far seem una solution tayari hapa unapima akili za watu tu!
 
kama umenisoma vizuri, nimemweleza hicho kitu sitaweza kufanya. Ndo ikabidi nimdanganye mpaka hapo watakapo kuwa sawa na mme wake.
This time anakuja nakusema wako ok and yuko ready kunipa penzi la kweli.

Wewe ulimwahidi ili iweje?

Nwy pamoja na hayo bado unashindwa nini kumwambia hutaki?Naona kila anaekwambia umpotezee unampa visingizio. . .ni kama vile unataka kuambiwa umkubalie tu so amua mwenyewe.Yatakayokukuta yatakua ni juu yako. . . kua tu mwangalifu .
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom