Penzi halina mjuaji wala msomi,

Makau Js

Member
May 25, 2017
93
233
WordPlay- Penzi ni moja ya kitu kigumu ambacho kimetushinda wanadamu wengi ,Penzi halina mjuaji wala msomi,na ndio maana maandiko yalitupa tahaadhali wanaume,''Pombe na wanawake huwapotosha wanaume wenye akili.'' kwa maana hiyo kama una akili kimbia pombe na wanawake.

Robert Gabriel Mugabe linapokuja swala la ,mahusiano huwa anakuwa romantic kwa mkewe ,Grace Marufu bila kipingamizi chochote ,Mugabe akiwa faragha huwa naye anabembeleza mkewe na kumpa maneno matamu.

Penzi lina nguvu sana ndio maana hata watu wanaoteka watu nchini Tanzania nao hutekwa na mapenzi na kuwa watumwa wa penzi.

Penzi linawaliza watu maskini na matajiri ,wanasiasa wanawadanganya sana wananchi ,ila linapokuja swala la mapenzi wanasiasa ndio wanakuwa watumwa wakubwa wa mapenzi ,mapenzi yana watesa sana wanasiasa kuliko siasa yenyewe.

Nasisitiza mwanamke bora kabisa kwa mwanaume ni mke wake wa ndoa,Mke wa ndoa ndio mwanamke bora kabisa kwenye maisha yote ya mwanaume .

Kama unatembea na mume wa mtu na wewe ni binti ambaye haujaolewa jua unatumiwa kama chombo cha starehe, sababu mwisho wa siku mume atarejesha mwili wake na akili yake kwa mke wake wa ndoa wewe unakuwa daraja la hitaji lake la mwili.

Mabinti wanatumia muda mwingi sana kupost picture kwenye social media ,kuwavutia wanaume ,ile wavulana ndio hupenda like picture zao .

Wanaume tunajua uzuri wa mwanamke upo kwenye akili yake ,moyo wake na kinywa chake, Pasport size ,vitambulisho vya taifa na card za kupigia kura huonyesha uhalisia na uzuri wa mwanamke na sio picture za Instagram , na Facebook.

Hata Professor Ibrahim Haruna Lipumba huna anakuwa romantic kwa wake mwandani wake.The true measure of romantic love is commitment and trust, not physical attraction.[HASHTAG]#Romantic[/HASHTAG].
 
Ndo maana wanasema 'ku fall in love'
yaani kuanguka kwenye penzi..

Ukitumia akili huanguki...lakini mioyo huanguka
 
Robert Gabriel Mugabe linapokuja swala la ,mahusiano huwa anakuwa romantic kwa mkewe ,Grace Marufu bila kipingamizi chochote ,Mugabe akiwa faragha huwa naye anabembeleza mkewe na kumpa maneno matamu

Mmmmh, ushahidi tafadhali..!!
 
Mkuu mbona kama ku mwandiko wa Benjamini James fbook
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…