FRANC THE GREAT
JF-Expert Member
- May 27, 2016
- 5,416
- 7,828
Jetson: Teknolojia ya 'Laser' yenye uwezo wa kutambua watu kutokana na mapigo ya mioyo yao
Teknolojia iliyoandaliwa na Idara ya Ulinzi ya Marekani (DOD) imefungua uwezekano wa kutambua watu kutokana na mapigo ya mioyo yao. Teknolojia hiyo inajulikana kama Jetson, ambayo hutumia laser (Laser Vibrometry) kusoma mapigo ya moyo wa mtu (Cardiac Signatures).
Teknolojia hii ni ya kipekee kama ilivyo ile ya alama za vidole, yenye madhumuni ya kufanya utambuzi. Teknolojia hii ya utambuzi ni ngumu zaidi kuepukika tofauti na zingine ambazo kwa namna moja ama nyingine zinaweza kuepukika mfano, 'Face Recognition' ambayo unaweza kuiepuka kwa kuvalia kifunika uso (Mask) ama ndevu bandia.
Teknolojia hii imepewa uwezo wa kutambua mtu kutoka hadi umbali wa mita 200 kwa kuchunguza harakati za dakika juu ya uso wa ngozi dhidi ya mapigo yake ya moyo. Hi ni njia bora zaidi ya utambuzi sababu inaweza kutambua mtu akiwa umbali mrefu zaidi kuliko kuchunguza sura yake ama kuvikaribia vidole vyake kwa ajili ya 'Finger Prints' ambapo itahitajika mlengwa awe karibu.
Teknolojia hii imeundwa kutokana na maombi mbalimbali kutoka katika vitengo maalumu vya kijeshi nchini Marekani kuja na mbinu bora zaidi zenye kufanya utambuzi kwa usahihi zaidi na kwa umbali mrefu zaidi.
Makao makuu ya Idara ya Ulinzi nchini Marekani, Pentagon.
Meneja wa Programu ya Ofisi ya Usaidizi wa Kiufundi ya Kupambana na Ugaidi ya Pentagon, Stewart Remaly akitolea ufafanuzi kuhusiana na Teknolojia hii, alisema kuwa Teknolojia hii ina usahihi wa asilimia 95 na kwa nadharia inaweza kutumika kwa umbali mrefu zaidi.
Remaly alisema "siwezi kusema kwamba unaweza kutambua mapigo ya moyo kutokea anga za mbali lakini kwa umbali mrefu na wa kawaida hilo linawezekana kabisa".
Utambuzi kwa kutumia Teknolojia hii unaweza kutumia hadi sekunde thelathini (30) huku mlegwa husika akiwa mahali pamoja. Mara baada ya taarifa kukusanywa zinaweza kutumika kufuatilia magaidi wanaofikiriwa au watu wengine wenye maslahi binafsi.
Pamoja na kwamba Teknolojia hii ina usahihi kwa kiwango kikubwa lakini kutokana na upya wake na pia baadhi ya changamoto itahitajika zaidi kuhakiki majibu yake kwa kutumia teknolojia nyinginezo zilizo thibitishwa zaidi kama vile, Teknolojia ya utambuzi wa sura (Face Recognition).
Changamoto nyingine pia ni kutokana na upungufu wa taarifa za kutosha (Database) za za saini za mioyo (Cardiac Signatures) ambapo itahitajika kuandaliwa na kuendelezwa ili kuweza kuendana na mapigo ya moyo husika ama kinyume chake.
Licha ya hivyo, Teknolojia hii inaweza pia kutambua watu kutokana na matendo yao. Mfano, rekodi za mapigo ya moyo zinaweza kutumika kumtambua mhusika aliyetoka kufanya jambo fulani la kihalifu kama vile, kupandikiza bomu, ujambazi n.k. baada ya kukamatwa.
Unaweza kujibadili sura kwa kufanya 'Plastic Surgery' ama unaweza kuunguza 'Finger Prints' zako ila itakuwa ngumu sana kuiepuka aina hii ya Teknolojia ya utambuzi wa mapigo ya moyo pale itakapoanza kutumika hususan na vyombo vya ulinzi na usalama nchini Marekani.
Prepared by: FRANC THE GREAT
Sources: Forbes | Extreme Tech | Army-Technology | IFL Science | Getty Images
Teknolojia iliyoandaliwa na Idara ya Ulinzi ya Marekani (DOD) imefungua uwezekano wa kutambua watu kutokana na mapigo ya mioyo yao. Teknolojia hiyo inajulikana kama Jetson, ambayo hutumia laser (Laser Vibrometry) kusoma mapigo ya moyo wa mtu (Cardiac Signatures).
Teknolojia hii ni ya kipekee kama ilivyo ile ya alama za vidole, yenye madhumuni ya kufanya utambuzi. Teknolojia hii ya utambuzi ni ngumu zaidi kuepukika tofauti na zingine ambazo kwa namna moja ama nyingine zinaweza kuepukika mfano, 'Face Recognition' ambayo unaweza kuiepuka kwa kuvalia kifunika uso (Mask) ama ndevu bandia.
Teknolojia hii imepewa uwezo wa kutambua mtu kutoka hadi umbali wa mita 200 kwa kuchunguza harakati za dakika juu ya uso wa ngozi dhidi ya mapigo yake ya moyo. Hi ni njia bora zaidi ya utambuzi sababu inaweza kutambua mtu akiwa umbali mrefu zaidi kuliko kuchunguza sura yake ama kuvikaribia vidole vyake kwa ajili ya 'Finger Prints' ambapo itahitajika mlengwa awe karibu.
Teknolojia hii imeundwa kutokana na maombi mbalimbali kutoka katika vitengo maalumu vya kijeshi nchini Marekani kuja na mbinu bora zaidi zenye kufanya utambuzi kwa usahihi zaidi na kwa umbali mrefu zaidi.
Makao makuu ya Idara ya Ulinzi nchini Marekani, Pentagon.
Meneja wa Programu ya Ofisi ya Usaidizi wa Kiufundi ya Kupambana na Ugaidi ya Pentagon, Stewart Remaly akitolea ufafanuzi kuhusiana na Teknolojia hii, alisema kuwa Teknolojia hii ina usahihi wa asilimia 95 na kwa nadharia inaweza kutumika kwa umbali mrefu zaidi.
Remaly alisema "siwezi kusema kwamba unaweza kutambua mapigo ya moyo kutokea anga za mbali lakini kwa umbali mrefu na wa kawaida hilo linawezekana kabisa".
Utambuzi kwa kutumia Teknolojia hii unaweza kutumia hadi sekunde thelathini (30) huku mlegwa husika akiwa mahali pamoja. Mara baada ya taarifa kukusanywa zinaweza kutumika kufuatilia magaidi wanaofikiriwa au watu wengine wenye maslahi binafsi.
Pamoja na kwamba Teknolojia hii ina usahihi kwa kiwango kikubwa lakini kutokana na upya wake na pia baadhi ya changamoto itahitajika zaidi kuhakiki majibu yake kwa kutumia teknolojia nyinginezo zilizo thibitishwa zaidi kama vile, Teknolojia ya utambuzi wa sura (Face Recognition).
Changamoto nyingine pia ni kutokana na upungufu wa taarifa za kutosha (Database) za za saini za mioyo (Cardiac Signatures) ambapo itahitajika kuandaliwa na kuendelezwa ili kuweza kuendana na mapigo ya moyo husika ama kinyume chake.
Licha ya hivyo, Teknolojia hii inaweza pia kutambua watu kutokana na matendo yao. Mfano, rekodi za mapigo ya moyo zinaweza kutumika kumtambua mhusika aliyetoka kufanya jambo fulani la kihalifu kama vile, kupandikiza bomu, ujambazi n.k. baada ya kukamatwa.
Unaweza kujibadili sura kwa kufanya 'Plastic Surgery' ama unaweza kuunguza 'Finger Prints' zako ila itakuwa ngumu sana kuiepuka aina hii ya Teknolojia ya utambuzi wa mapigo ya moyo pale itakapoanza kutumika hususan na vyombo vya ulinzi na usalama nchini Marekani.
Prepared by: FRANC THE GREAT
Sources: Forbes | Extreme Tech | Army-Technology | IFL Science | Getty Images