Pendekezo: Mafisadi na wala Rushwa wanyongwe hadharani..!!

magode

JF-Expert Member
Oct 2, 2014
2,201
3,322
Wanabodi,
Salaam;

Tangu awaamu hii ya 5 iingie madarakani,imekuwa ikiibua ufisadi mkubwa kila mahali. Ukimsikiliza Rais ktk hotuba zake anavyosikitika utadhani nchi haikuwa na uongozi kabisa huko nyuma.

Kwa hali jinsi ilivyo ktk nchi yetu,ili kujenga nidhamu ya kweli ya kuzuia ubadhirifu wa mali za umma,napendekeza adhabu ya kifo kwa mafisadi na wala rushwa. Kwa bahati nzuri sheria ya kunyonga watu bado tunayo ni kitendo tu cha serikali kupeleka muswada bungeni kuongeza idadi ya wanaotakiwa kunyongwa.

Lengo hapa siyo kuua watu,lengo ni kuweka adhabu kali ili watu wasiibe mali ya umma au kupoka haki za wengine kwa kupokea rushwa. Wale wa haki za binadamu tafadhali mkae kimya ktk hili nchi imeharibika sana hii..!

Kule korea kaskazini hivi karibuni wamemnyonga mkuu wa majeshi kuonyesha hakuna aliye juu ya sheria. Bila kuwanyonga hawa watu watazidi kunyonya nchi.

Nawasilisha!!
 
"Tena wanyongwe mbele ya makaburi yao wakifa tu wanateremshwa kuzikwa tena bila ya ibada!!" China haikuendelea kwa kunyonga watu bali kwa kuwekeza kwenye elimu ya watu wake na kutunza nidhamu ya kazi!!
 
Ingeanza na mtangulizi aliyetumbua mabilion ya bunge la katiba halafu mwisho wa siku imetupiwa kapuni.
 
Na tukirudi awamu tatu nyuma ingeanzia kwa Mzee ruksa, Lodi Lofa na Msoga Tansport.
 
"Tena wanyongwe mbele ya makaburi yao wakifa tu wanateremshwa kuzikwa tena bila ya ibada!!" China haikuendelea kwa kunyonga watu bali kwa kuwekeza kwenye elimu ya watu wake na kutunza nidhamu ya kazi!!
Hata sisi tutalazimika kutoa kwanza elimu kwa umma,ili kuondoa ile dhana ya kuvunja haki za binadamu. Wote tunapaswa kutetea na kuzilinda rasilimali zetu,atakayefanya kwa ujeuri au tamaa,akithibitishwa apigwe kitanzi mbele ya umma!
 
Back
Top Bottom