Pendekezo: ITV iwe TV ya Taifa badala ya TBC.

Pendekezo: ITV iwe TV ya Taifa badala ya TBC.

Sodoku

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2016
Posts
1,277
Reaction score
2,933
Nashauri kwa dhati kabisa toka kwenye uvungu wa moyo wangu.pasipo kuwa na mawaa au madoa katika ubongo wangu.nikiwa na akili timamu kabisa. ITV iwe ndo TV ya Taifa.

Kiukweli hii TV ambayo kwa kiasi kikubwa sana imekuwa ikijitahidi kuwarushia matangazo wa Tanzania kwa wakati muafaka. Tumeona mara nyingi kunapotokea majanga au habari ambzo taifa linatakiwa kuzipata kwa wakati huo TBC wamekuwa wakituwekea muziki au kuendelea na matangazo mengine kama kawaida.
TBC imekuwa ni TV ya serikali.

Imekua ikijikita zaidi kwenye kurusha matangazo ya dhifa na mikutano ya kiserikali zaidi kuliko habari nyingne ambazo nazo ni muhimu kwa wananchi.
 
Msemali kweli ni mpenzi wa Mungu wewe ni msemakweli hata unaangalia taarifa ya habari kwa utasikia weka ITV
 
kweli Ndalichako ana kazi kubwa, sekta binafsi iliruhusiwa ili iipe changamoto serikali hiyo tv unayopigia debe ni ya mtu binafsi utamnyang'anyaje uigeuze ya taifa.Isitoshe sijaona uwezo wake wakati inashindwa kutuonyesha vitu vingi duniani kama mashindano ya olympic
 
kweli Ndalichako ana kazi kubwa, sekta binafsi iliruhusiwa ili iipe changamoto serikali hiyo tv unayopigia debe ni ya mtu binafsi utamnyang'anyaje uigeuze ya taifa.Isitoshe sijaona uwezo wake wakati inashindwa kutuonyesha vitu vingi duniani kama mashindano ya olympic
TBC imeonyesha nini mpaka sasa? Halafu kwani TBC ipo hewani kweli maana sa mbili asilimia kubwa ya watazamaji huangalia itv.
 
Kwa sasa hapana

ITV ilikua kabla ya awamu hii,naona inapoelekea tutaiona kama TBC nayo

Sijui TCRA wameiathiri au ni vitisho vya NAPE au baada ya MENGI kuoa miss Tz,kwa hapa nashindwa kuelewa
 
Back
Top Bottom