Paul Makonda: Alama ya uongozi uliotufikisha hapa

pepsin

JF-Expert Member
Apr 23, 2015
3,465
6,109
Tanzania hatuna uongozi kwenye wenye maono. Mfano ni Makonda, RC wa Dar.

Viongozi hawatekelezi program zao kabla ya kurukia zingine.

1. Hivi Makonda amemaliza swala la ombaomba Dar? Bado, wapo tele.

2. Makonda amemaliza swala la biashara ya ukahaba Dar? Bado, wapo tele..

3. Makonda amerukia Shisha kabla hajamaliza kusimamia maagizo yake ya nyuma!

Kwa viongozi aina ya Makonda, tusahau kuhusu maendeleo endelevu.
 
kuna maandalizi ya 2020 mkuu!kwahyo zpo njia nying ikiwemo ya mauzo kwny media!umesahau kale kamsemo'nawafunika'hahahaaa... poteza kabsa jina licckike ili bdae iwe mtelezo 2020,na vile hatujuag kutunza kumbukumbu vzur yani wakat ukifika tutababaishwa sana na siasa uchwara!
 
Makonda anatembea na laana ya warioba
Kumshangaa kichaa akitembea uchi ni kujipotezea muda tu
Anatumia style ya mtu mmoja alikuwa RC Arusha Mwanza na akaishia speed zake Mara. Nakumbuka akiwa Arusha aljaribu kwa njia zote Lema asionekane kama ni kiongozi wa watu akamuwekea vizuizi vingi na mwisho akamua yy na policcm wakampeleka mahabusu Kisongo kwa siku 14 sala la wana wa Arusha zikamuandama akapelekwa Mwanza akaanza na wamchinga ati hataki kuwaona. Mwisho akamchongea hata RAS ambae alikuwa na elimu mara mia ua huyo Rc mkuu wa kaya akamuondoa RAS vilio na machozi ya wamachinga na familia ya Ras ikalilia miguuni kwa huyo RC sasa anaisoma number
Makonda elewa ngoma ikivuma sana inakarbia kupasuka. Hatuta shangaa ukawa RC wa kwanza kijana kutumbuliwa. Show off zako hazina muda waheshimu waliochaguliwa na watu.
Kama huna kazi inaingilia jadi kazi za madiwani bora ukae ofisino uongoze kamati ya ulinzi na usalama.
 
Mnamshangaa huyo konda badala ya aliyemteua?
Umenena mkuu! Kwa hakika kabisa, kitendo ambacho Makonda alimfanyia Mzee Warioba kama nchi ingekuwa na uongozi unaotafakari na kuona mbali Makonda alikuwa hastahili kupewa nafasi yoyote ya uongozi. Aliharibu JK kumpa UDCna Magufuli kaharibu zaidi kwa kumpa URC. Makonda anatumikia pigo la kimaadili na kiroho, na ukweli ni kwamba hakuna atakalolifanikisha kiutendaji bali atasababisha mafarakano ambayo yatawashangaza hata wanaomteua!
 
Mnamshangaa huyo konda badala ya aliyemteua?

Pointi.

Na hayo ayasemayo hata bila kuyatekeleza ndiyo yaliyofanya aliyemteua ampandishe cheo kutoka u-DC hadi u-RC, tena kwa

ahadi ya kuwakomoa wanaomkosoa Makonda kwa hayo afanyayo....
 
makonda alinishangaza pale aliposimamisha mikataba ya ujenzi wa barabara na kampuni zngne kuzuia kufanya kazi mkoa wa dar...

ukweli ni kwamba mikataba ya halmashauri, manispaa na jiji haipaswi kuingiliwa na DC wala RC..
 
Tanzania hatuna uongozi kwenye wenye maono. Mfano ni Makonda, RC wa Dar.

Viongozi hawatekelezi program zao kabla ya kurukia zingine.

1. Hivi Makonda amemaliza swala la ombaomba Dar? Bado, wapo tele.

2. Makonda amemaliza swala la biashara ya ukahaba Dar? Bado, wapo tele..

3. Makonda amerukia Shisha kabla hajamaliza kusimamia maagizo yake ya nyuma!

Kwa viongozi aina ya Makonda, tusahau kuhusu maendeleo endelevu.
teh! yuko pale kukwamisha maendeleo ya wananchi ambayo yanaletwa na ukawa .....Jana naskia ametoa ufafanuzi wa kazi ya meya wa jiji
 
makonda alinishangaza pale aliposimamisha mikataba ya ujenzi wa barabara na kampuni zngne kuzuia kufanya kazi mkoa wa dar...

ukweli ni kwamba mikataba ya halmashauri, manispaa na jiji haipaswi kuingiliwa na DC wala RC..
Duuuuuh aiseee hiyo ni zaidi ya aibu.
 
Sijawahi kabisa kumkubali Makonda na aina yake ya uongozi.
Nawashangaa sana wanaomkubali.
Sijawahi kuona lolote la maana kutoka kwake.

Hivi yuko wapi 'pacha' wake Sapi?
Hadi nilishamsahau.
 
Hii ni karata njema kwa upinzani, tangu ateuliwe amekua ni mtu wa kutafuta sifa, hivi ile ishu ya walimu kupanda mabasi bure imeishia wapi? Kila anachoanzisha kinaishia katikati.
 
Mm jmn am serious nimechooka kumuona kwenye media i want to see results,why do u want support for doing ur job which you are not doing? Ni kama mwalimu aite media kumrekodi akiingia darasani ? That is ur job do ur job lets see the results makonda unafeli na unatia aibu vijana daresalaam ni jiji na hatuko kwenye vita sasa ubabe wa nini?wababe wa vita woote lose i know u r loosing but usituekee evidence of how much u r loosing najua hatuja kuchagua but sisi wana daresaalam tuna jua pabaya na pazuri na haupo kwenye ukweli,uzuri,wala utendaji haki so second chance loose this media and get to work let us judge you not ur president.
 
Makonda kuongelea majukumu ya meya wa jiji kwa namna ile ni kama mipasho, pia ni dalili za uoga au kutojiamini (yeye na ccm)....

Kwa nn asingeongelea majukumu na mipaka ya madaraka ya RC ?

itafikia wakati raia watakuwa wanampuuza.
mkuu tumpuuze Mara ngapi
.....mzee wa matukio yule
 
Sasa analalamika kwamba mitandao ya kijamii inamfuatilia aache kulalamika ajifunze busara.Siasa za uccm zitampeleka pabaya akumbuke ni miaka kumi.Atakuja mwingine atapigwa buti kama wengine.
 
Um
Tanzania hatuna uongozi kwenye wenye maono. Mfano ni Makonda, RC wa Dar.

Viongozi hawatekelezi program zao kabla ya kurukia zingine.

1. Hivi Makonda amemaliza swala la ombaomba Dar? Bado, wapo tele.

2. Makonda amemaliza swala la biashara ya ukahaba Dar? Bado, wapo tele..

3. Makonda amerukia Shisha kabla hajamaliza kusimamia maagizo yake ya nyuma!

Kwa viongozi aina ya Makonda, tusahau kuhusu maendeleo endelevu.
Umesahau uhakiki wa Bunduki mkuu!
 
Back
Top Bottom