Passport 600 zimekaa Uhamiaji Kurasini, zingine ziliombwa tangu mwaka 2005

Richard

JF-Expert Member
Oct 23, 2006
14,939
20,400
Tanzania-passport-1.png


Passport zaidi ya 600 zipo makao makuu ya uhamiaji Kurasini na hazijachukuliwa na wenyewe.

Pasi hizo pamoja na zile za Afrika Mashariki nyingi ziliombwa kati ya mwaka 2005 na mwaka 2015.

Katika siku za hivi karibuni idara ya uhamiaji imetisitsha zoezi la utoaji pasi hadi hii "backlog" ya hizi zilizo tayari ziweze kuhakikiwa na kujulikana nani ni wamiliki wake.

Hivyo kama una mtu unamfahamu au ndugu, jamaa au rafiki , basi unaweza kumjulisha utakapoona jina lake katika orodha iliyo katika link hii- http://immigration.go.tz/PASIPOTI DSM.pdf

Pia ipo orodha ya passport 17 za waombaji wa kutoka mkoa wa Mbeya ambazo inapatikana hapa: http://immigration.go.tz/ORODHA YA PASIPOTI MBEYA.pdf
 
watakuwa wamesumbuliwa sana kuzipata hizo passport mwishowe wakaamua kuzira,sasa wanahangaika kuwatafuta na visingizio kibao vya kukosekana vitabu
 
Kwa nchi ya watu 50Milion, passport 600 sio kitu.
Utakuta wengi ya walioomba ni wagonjwa na waliopata safari za ghafla. Baada ya kuzikosa wameamua kuzikaushia..
Wazichome moto, mchakato uanze upya..
 
Back
Top Bottom