Aliyekuwa mbunge wa viti maalumu Mkoa wa Arusha, Cecilia Paresso, amewataka wananchi wa Kilimanjaro kumpa kura za kishindo mgombea urais wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Samia Suluhu Hassan, ifikapo Oktoba 29, akisema ameweka mazingira bora kwa wafanyabiashara nchini.
Akizungumza jana Jumatatu, Septemba 8, 2025, katika uzinduzi wa kampeni za CCM uliofanyika Kata ya Pasua, Manispaa ya Moshi, Paresso amesema kabla ya Samia kuingia madarakani wafanyabiashara walikuwa na hofu kubwa, kiasi cha baadhi yao kuhamisha mitaji nje ya nchi.
“ Samia alipoingia madarakani aliboresha mahusiano na wafanyabiashara, hasa kwenye mifumo ya kodi. Leo hii mazingira yamebadilika na wafanyabiashara wanafanya shughuli zao bila hofu,” amesema Paresso.
Uzinduzi huo umehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa chama hicho pamoja na wananchi. Mgombea ubunge wa Jimbo la Moshi Mjini, Ibrahim Shayo maarufu Ibra Line, aliyeahidi kushirikiana na Serikali katika ujenzi wa stendi ya mabasi, miundombinu ya barabara na ukusanyaji wa taka ngumu
Soma pia
Chanzo: Mwananchi_official
Akizungumza jana Jumatatu, Septemba 8, 2025, katika uzinduzi wa kampeni za CCM uliofanyika Kata ya Pasua, Manispaa ya Moshi, Paresso amesema kabla ya Samia kuingia madarakani wafanyabiashara walikuwa na hofu kubwa, kiasi cha baadhi yao kuhamisha mitaji nje ya nchi.
“ Samia alipoingia madarakani aliboresha mahusiano na wafanyabiashara, hasa kwenye mifumo ya kodi. Leo hii mazingira yamebadilika na wafanyabiashara wanafanya shughuli zao bila hofu,” amesema Paresso.
Uzinduzi huo umehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa chama hicho pamoja na wananchi. Mgombea ubunge wa Jimbo la Moshi Mjini, Ibrahim Shayo maarufu Ibra Line, aliyeahidi kushirikiana na Serikali katika ujenzi wa stendi ya mabasi, miundombinu ya barabara na ukusanyaji wa taka ngumu
Soma pia
- GE2025 - Paresso: Reforms tulizozitaka tukiwa CHADEMA zimefanyika CCM
- GE2025 - Cecilia Paresso achukua fomu ya kuomba CCM kugombea Ubunge Jimbo la Karatu Mkoani Arusha
- GE2025 - Cecilia Paresso aeleza sababu za kujiunga CCM ambazo ni pamoja na kuvutiwa na sera pamoja na siasa za maridhiano
Chanzo: Mwananchi_official