Kada wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Cecilia Paresso amesema kutokana na utekelezaji wa miradi ya maendeleo uliofanywa na CCM, chama hicho kinakuwa chama pekee kinachofaa kuendelea kuongoza nchi
Paresso ambaye alikuwa mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Arusha na kwa muda mrefu kada wa CHADEMA kabla ya kuhamia CCM, amesema Dkt. Samia anastahili kupewa kura kwani kaonesha uwezo wake kiuongozi kwa kipindi cha miaka minne aliyokuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
"hiki chama ambacho kimetuongoza kwa kipindi chote ndiyo chama pekee ambacho kinaweza kutuongoza tena sisi tuliopo leo, watoto wetu na vizazi vijavyo"
Paresso amesema katika kuonyesha uwezo wa kiuongozi, CCM imefanikiwa kuilinda amani ya nchi yetu jambo ambalo ametahadharisha kuwa vyama vingine havitaweza kufanya endapo vikipewa mamlaka
Haya ameyasema Septemba 23, 2025 akiwa katika mwendelezo wa vikao vya kutafuta ushindi wa Dkt Samia, Mgombea ubunge wa jimbo la Muhambwe Dkt Samizi pamoja na madiwani wa jimbo hilo
Akiwa jimbo la Muhambwe Paresso ameshiriki vikao pamoja na kamati za siasa za matawi, kamati za utekelezaji za jumuiya na mabalozi katika matawi ya Nyabitaka, Nyarugusu , Kasana na Kumshwabure
Paresso ambaye alikuwa mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Arusha na kwa muda mrefu kada wa CHADEMA kabla ya kuhamia CCM, amesema Dkt. Samia anastahili kupewa kura kwani kaonesha uwezo wake kiuongozi kwa kipindi cha miaka minne aliyokuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
"hiki chama ambacho kimetuongoza kwa kipindi chote ndiyo chama pekee ambacho kinaweza kutuongoza tena sisi tuliopo leo, watoto wetu na vizazi vijavyo"
Paresso amesema katika kuonyesha uwezo wa kiuongozi, CCM imefanikiwa kuilinda amani ya nchi yetu jambo ambalo ametahadharisha kuwa vyama vingine havitaweza kufanya endapo vikipewa mamlaka
Haya ameyasema Septemba 23, 2025 akiwa katika mwendelezo wa vikao vya kutafuta ushindi wa Dkt Samia, Mgombea ubunge wa jimbo la Muhambwe Dkt Samizi pamoja na madiwani wa jimbo hilo
Akiwa jimbo la Muhambwe Paresso ameshiriki vikao pamoja na kamati za siasa za matawi, kamati za utekelezaji za jumuiya na mabalozi katika matawi ya Nyabitaka, Nyarugusu , Kasana na Kumshwabure