Panya road waibukia Bunju

Panya road waibukia Bunju

Polisi wako njia panda. Hawa madogo wanafahamika na ni wakorofi sana sana, manunda! Hawa kuwakamata na kuwapeleka mahakamani ni usumbufu maana raia pia hawana muda na hayo makesi.

Yuko askari aliniambia hao dawa yao ni chuma tu, wakitandikwa wa mfano wanaufyata huwasikii. Lakini sasa hivi maagizo ni wakamatwe na kufikishwa mahakamani hata kubinywa kidogo ni kinyume na haki za binadamu.

Shortly anasema raia mjipange na hao watu wenyewe, hata polisi wakiingilia watakimbia kwa muda watarejea siku nyingine!

Majuzi wamesumbua huko temeke kadhaa wakala chuma ikaleta kasheshe na watu wa haki za binadamu lakini palitulia. Polisi bila sisi raia tutawalaumu bure. Hata Bunju tafuta wakongwe wa ulinzi shirikishi wanajua mitaa yote yenye watoto wa kihuni.

Sent from my SM-A315F using JamiiForums mobile app
 

Hawa wahuni dawa yao ni moja tu, sema hizi kelele za haki za binadamu ndio kikwazo.

Ni wakatili sana, na kama tukiendelea kuwafuga hapo baadae tutakuja kuwa na magaidi nchini.
 
Wale vijana wapiga mapanga usiku maarufu kama panya Road wameibukia Bunju ambapo Jumamosi iliyopita walitinga Bunju B mitaa ya KIHONZILE na kuumiza watu zaidi ya 8 na kuiba vitu kadhaa zikiwepo TV na simu za mikononi na fedha.

Tukio hilo ambalo halikutangazwa popote kutokana na OCD wa Kawe kulifunika na hivyo wananchi kutopata habari na kujiweka ktk tahadhari limepelekea usiku wa kuamkia leo panya road wameibukia mitaa ya maarufu kama kwa Mama Munuo na kuendeleza ubabe huohuo.

Katika matukio yote mawili Polisi walipigiwa simu ila hawakupokea na pia Polisi wa dharura wanaokaa maeneo ya barabarani walipofuatwa hawakuwepo eneo hilo.

Tunaomba Serikali kupitia Bunge lake linalofanya vikao vyake kijini Dodoma kwa dharura wajadili kadhia hii siku ya leo na kupeleka askari wa kutosha eneo hilo.
Hawa ni pandikizi
 
Kwa Sasa wajiandae watu.

TABATA SEGEREA HADI KINYEREZI.

UBUNGO KIBANGU KUELEKEA MAJICHUMVI HADI BONYOKWA.

ULIZLNZI SHIRIKISHI UIMARISHWE.

SAMIA S.H

Tafadhali mama
 
Yaani bunge lijadili panya road? Acha masihara hayo, hivi vitoto mnavifuga wenyewe ndio bunge liache kazi zake kuwajadili?

Ningekuona wa maana ungesema bunge lijadili ukali wa maisha.
Kwani Bunge wanajadili nini cha maana kule mpaka unaona hawawezi kujadili panya Road swala la usalama wa raia ni muhimu mno mno...
 
Yaani bunge lijadili panya road? Acha masihara hayo, hivi vitoto mnavifuga wenyewe ndio bunge liache kazi zake kuwajadili?

Ningekuona wa maana ungesema bunge lijadili ukali wa maisha.
Kwani bunge linafanyaga kazi gani, zaidi majigambo ya kinyiramba na kuzodoana.
 
Wale vijana wapiga mapanga usiku maarufu kama panya Road wameibukia Bunju ambapo Jumamosi iliyopita walitinga Bunju B mitaa ya KIHONZILE na kuumiza watu zaidi ya 8 na kuiba vitu kadhaa zikiwepo TV na simu za mikononi na fedha.

Tukio hilo ambalo halikutangazwa popote kutokana na OCD wa Kawe kulifunika na hivyo wananchi kutopata habari na kujiweka ktk tahadhari limepelekea usiku wa kuamkia leo panya road wameibukia mitaa ya maarufu kama kwa Mama Munuo na kuendeleza ubabe huohuo.

Katika matukio yote mawili Polisi walipigiwa simu ila hawakupokea na pia Polisi wa dharura wanaokaa maeneo ya barabarani walipofuatwa hawakuwepo eneo hilo.

Tunaomba Serikali kupitia Bunge lake linalofanya vikao vyake kijini Dodoma kwa dharura wajadili kadhia hii siku ya leo na kupeleka askari wa kutosha eneo hilo.
polisi wetu kwenye matukio ya kushutukiza usiwaite labda iwepo hela
 
Update: Panya road washauawa wote walioshiriki kuleta taharuki bunju na boko.
 
Back
Top Bottom