Panya road wafanya uporaji Yombo Buza

Nadhani hapa pia kuna tatizo kubwa la Malezi,


Mtoto anatoka usiku mnene kama huo mzazi unakua wapi? Wazazi wengi wamekua "Bize" sana na mambo ya kimaisha na kusahau kua na muda wa malezi wa kumfuatilia mwanae hasa vitendo vyake na marafiki anaozunguka nao, kujua marafiki wa mwanao ni jambo la msingi mno ili kuona mwanao ana muelekeo gani,

Pia kuna hili suala la kubeti,hii ni kama kucheza Kamari, mtoto akikosa hela za kubet basi atajaribu kuzitafuta kwa njia yeyote ile ili tu akabeti coz amesha kua addicted na mchezo huo,

Wazazi tujitafakari na malezi ya vijana wetu kabla ya kuvitupia lawama vyombo vya ulinzi,

Malezi ni jukumu la kila mzazi na kila mwalimu na wananchi kwa ujumla.
Tunaomba mtuache walimu, waleeni wenyew watoto Wenu.
 
Kundi kubwa la vijana wanaosadikika kuwa ni zaidi ya 30 usiku wa kuamkia Leo maeneo ya Buza kwa Osama wamevamia nyumba moja na kupora vitu mbalimbali kama TV,computer, simu na pesa kwa mkazi mmoja wa eneo hilo.

Vijana hao kabla ya uvamizi huo walikuwa na mabishano ya kuingia nyumba hiyo au kutokuingia ndipo walipoamua kuanza kuvunja mlango wa ndugu huyo aliyejaribu kuomba msaada kwa majirani bila mafanikio.

Jirani wa ndugu huyo walidai kushindwa kutoka kutokana na wingi wa vijana hao waliokuwa na mapanga,marungu,majambia na baruti walizokuwa wanawatishia kama bunduki.Hata hivyo baada ya kuanza kuondoka ndipo majirani walipotoka kuanza kuwasaka hivyo kusababisha kutupa ovyo TV,radio na computer walizokuwa wamebeba baada ya kuona wananchi wanawfukuza na kutokomea kusikojulikana.
makonda
 
Msisingizie walimu hata kidogo sisi wazazi walimu wakichukua hatua juu ya mienendo mibaya ya watoto wetu ndio tunakua wa kwanza kupayuka hovyo na kutukana! Tuwaache walimu wapumzike malezi yabaki kuwa ni jukumu letu tukishindwa iwe basii
Mkuu nadhani hukunielewa vizuri,sikulaumu mtu yeyote bali nimetoa ushauri tu kua malezi yasimamiwe na wazazi,walimu na wananchi kwa ujumla.
 
Mkuu wa mkoa na yeye pia aitwe ili ahojiwe live, na majibu yakiwa hayajitoshelezi awekwe ndani na yeye. Mkuki kwa nguruwe kwa binadamu mchungu
 
Tunaomba mtuache walimu, waleeni wenyew watoto Wenu.
Mkuu nilimaanisha hivi;

Mtoto akiwa nyumbani ni jukumu la mzazi,akiwa Shuleni kwa kawaida anakua chini ya uangalizi wa Shule "Walimu" akiwa mitaani ni jukumu la kila raia kumkanya au kumuongoza anapoona anafanya jambo lolote baya,

Watoto ndio taifa la kesho, na bila kutengeneza kizazi kijacho kua na maadili mazuri nadhani itakua ni tatizo kubwa huko mbeleni,

Huu ni ushauri tu,najua ni ngumu kiasi but we have no choice kama tunataka amani na kua na taifa bora.
 
Kero za jiji la Dar zilishamalizwa na RC na alishawasambalatisha na ziara yake ya siku 10

Cc Makonda
 
Watoto wote hao mnaowaita panya road wanajulikana wote wanakokaa,wazazi wao,majina yao,na mambo yao mengi tu.

Kama jamii mmeamua kuishi maisha hayo msitegemee mtarekebishiwa na jamii nyingine au Serikali.

Wazazi wenyewe watoto nao wanajuana vizuri sana na ndiyo staili ya maisha ya jamii hiyo.Serikali itaumiza kichwa sana lakini suluhu wanayo wana jamii wenyewe.

Wakiamua kuyakataa maisha hayo na kubadilika na hao panya raod watakuwa historia.

'Mabadiliko huanza na jamii husika na mabadiliko huanza na mimi'
 
Mkuu nilimaanisha hivi;

Mtoto akiwa nyumbani ni jukumu la mzazi,akiwa Shuleni kwa kawaida anakua chini ya uangalizi wa Shule "Walimu" akiwa mitaani ni jukumu la kila raia kumkanya au kumuongoza anapoona anafanya jambo lolote baya,

Watoto ndio taifa la kesho, na bila kutengeneza kizazi kijacho kua na maadili mazuri nadhani itakua ni tatizo kubwa huko mbeleni,

Huu ni ushauri tu,najua ni ngumu kiasi but we have no choice kama tunataka amani na kua na taifa bora.

Kwa maisha ya dsm mtoto akiwa mtaani anajisimamia mwenyewe, nobody cares what he/she does. Selfishness imetawala.
 
Hao mpaka itokee siku wamvamie mtu mwenye bastola awapukutishe watano tu ndiyo watanyooka
 
Back
Top Bottom