Pamoja na pongezi; Maombi kwa Mwenyekiti mpya wa UVCCM na timu yako

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,172
7,428
14e5fcb4f5e03f533c72c194bb8cf4c1--helping-hands-quotes-helping-others-quotes.jpg


Ndugu yangu; kazi ya kiongozi ni kuwasaidia wengine kwa namna yoyote iwezekanayo na naamini uliipigania nafasi hiyo kwa lengo la kuwasaidia vijana kwa vile utakavyoweza.

Comrade mwenyekiti; tukuombe jambo moja ambalo kwa sasa pengine ndio changamoto kubwa zaidi inayowakabili vijana na kwa bahati mbaya si vijana wenyewe wala wazee wetu ambao wameweza kuishughulikia na kuipatia suluhu kikamilifu licha ya jitihada mbali mbali zinazofanyika.Tunaamini wengi wanaliona hili na wangependa litatuliwe lakini mjadala unaweza kuwa juu ya njia bora zaidi ya ku address changamoto hii.

Mkuu; wewe pamoja na timu yako, itapendeza kama mtakaa na kuandaa mkakati mzuri juu ya kutatua changamoto ya ukosefu wa ajira kwa vijana nchini kwani vijana wengi sana wanashindwa kufikia ndoto zao kutokana na changamoto hii.

Mkuu suala hili ni gumu lakini linaweza kushughulikiwa na serikali ya Ccm kama ikitia nia, nanyi mkawaongoza vijana wengine kuweka input za maana katika hilo .

Hata hivyo ni vyema vijana wenyewe wakafanya uchambuzi wa changamoto hii na kuwashauri viongozi wa nchi namna ya kukabiliana zaidi na changamoto hii ambayo inazidi kuongezeka kila Siku. Kimsingi, Wewe na timu yako kama mtaona inafaa na ikiwapendezeni, mnayo nafasi nzuri ya kuwaongoza wengine katika hili.

Kuhusu mahali pakuanzia; mambo mawili yaneweza kuzingatiwa ikionekana inafaa.

Kwanza, mnaweza kuratibu matamasha ambayo mnaweza kuwakutanisha vijana na watu ambao wanaweza kuwapatia elimu juu ya umuhimu wa kuanzisha miradi yao wenyewe kidogo kidogo, kuweza kuwa " inspire" , kuwa "coach" na kuwa "motivate" ili wapate momentum ya kuanza. Jambo hili nimuhimu sana kwani wengi wana saikolojia ya kushindwa na hili ni tatizo kubwa.

Pili, hii ilishashauriwa huko nyuma kuwa muweze kutengeneza vizuri wazo lililotolewa kwamba, badala ya vijana wote kupatiwa mikopo wakasome chuo kikuu , kisha baada ya hapo zaidi ya 90% wakose ajira ya walichosomea, basi mikopo igawanywe mafungu mawili. Moja wapewe wanaopenda sana kuwa na degree na nyingine wakopeshwe wenye ndoto za kuwa na miradi na makampuni yao. Wazo hili limefafanuliwa vyema humu Jf na litazidi kufafanuliwa kwenye Uzi huu na

Tatu, kutengeneza plan yoyote mtakayoona inafaa kusaidia kukabili changamoto hii.

Mkuu, kama mkifanikiwa kulifanyia kazi jambo hili na likafanikiwa, mtakuwa mumewasadia vijana wenzenu wengi na hakika watawashukuruni. Kadhalika mtaacha alama katika uongozi wenu duniani na kwa Mungu mtakuwa na malipo pia. Ni nini basi mnaweza kufanya na kiwaka na faida kwa vijana kuzidi hili? Kama mkiona jambo hili ni jema basi fanyeni na hakuna atakayejutia. Nawatia moyo kuwa mkiamua mnaweza kufanya jambo kubwa ambalo halikutegemewa.
 
Vyuo vyetu vikuu vinazalisha wahitimu maelfu kwa malaki kila mwaka jambo ambalo ni mafanikio makubwa lakini kutokana na udogo wa sekta rasmi nchini ni wachache tu ambao wanaweza kupata ajira rasmi kulingana na walichosomea kwa sasa. asilimia kubwa ya wahitimu Hawa hawapati ajira na kutokana na mazingira, hujikuta elimu walizopata darasani hazilingani na mazingira ya mtaani na hivyo si tu hujikuta wanashindwa kutumia elimu hizo Bali pia hujikuta wakishindwa kujitegemea na kuweza kuzalisha kwa ajili ya kujikimu na kuleta maendeleo kwa taifa kwa ujumla.wengine hujikuta wakiwa tegemezi tena kwa ndugu zao walioishia lanne, la saba au kidato cha nne.
 
Naam naunga mkono hoja yako Azizi, ngoja tuone wazo hili likifanyiwa kazi na jumuiya inayoweza kupata upendeleo kwa serekali. Isije ikawa jukumu lao ni kuhakikisha ccm inashinda uchaguzi tu kwani sasa ni dhahiri ccm haishindani kwa hoja tena bali ukatili unaoratibiwa chini ya jeshi la polisi. Hapa natarajia kuona hiyo ccm mpya kwa vitendo na sio hadithi za majukwaani.
 
Naam naunga mkono hoja yako Azizi, ngoja tuone wazo hili likifanyiwa kazi na jumuiya inayoweza kupata upendeleo kwa serekali. Isije ikawa jukumu lao ni kuhakikisha ccm inashinda uchaguzi tu kwani sasa ni dhahiri ccm haishindani kwa hoja tena bali ukatili unaoratibiwa chini ya jeshi la polisi. Hapa natarajia kuona hiyo ccm mpya kwa vitendo na sio hadithi za majukwaani.
Mkuu, nikuombe usiingize habari za uxhaguzi kwenye mada hii maana mada itapoteza muelekeo na kukosa maana. Hapa tujadili ni kwa vipi UVCCM inaweza kusaidia kwa namna moja ama nyingine kukabili changamoto ya ajira kwa vijana. Tukiweka input kwa hili itapendeza zaidi.
 
Kutokana na kushindwa kupata ajira, changamoto tatu hujitokeza.

1. Wanashindwa kujitegemea na hivyo ndoto zao kufifia na pengine kupotea.

2. Kushindwa kurejesha mikopo kwa kuwa hawana kazi na hawana ajira na hawana ajira maana kimsingi hazipo nafasi za kutosha kuwaajiri wote. Na


3. Kushindwa kutoa mchango kwenye ujenzi wa uchumi wa nchi licha ya kuwa ni vijana na ndio wanaotegemewa zaidi.
 
Sasa ndugu zangu, miongoni kwa njia za kutatua hili, ni pamoja na kufanya diversifications kwenye mafunzo na mikondo ambayo vijana hukulia. Yaani vijana wote wasipite njia moja halafu wakikwama wanakwama wote Bali tutengeneze redundancy, watawanyike mapema ili kuokoa muda na rasilimali lakini kupunguza concentration kwenye eneo moja.
 
Mkuu, nikuombe usiingize habari za uxhaguzi kwenye mada hii maana mada itapoteza muelekeo na kukosa maana. Hapa tujadili ni kwa vipi UVCCM inaweza kusaidia kwa namna moja ama nyingine kukabili changamoto ya ajira kwa vijana. Tukiweka input kwa hili itapendeza zaidi.

Mkuu ikishakuwa ni mada ya wazi tutachangia kwa kuweka maangalizo muhimu kutokana na uhalisia wa mambo, vinginevyo kama ni ya uvccm tu unaweza kuwaomba wakakupa nafasi kwenye vikao vyao vya ndani ukatoa huu ushauri mzuri. Sipingi kwamba ni ushauri mzuri ila kitakachofanyika ni wazo lako kutekelezwa kichama na sio kitaifa.
 
fc5fd938b43099f14553d47ab27b896f.jpg

Ndugu James, nakupongeza kwa kupata fursa ya kuiongoza UVCCM, jumuia ambayo ndio yenye vijana wengi na pengine ushawishi zaidi ya jumuiya nyingine yoyote nchini.

Ndugu yangu, kazi ya kiongozi ni kuwasaidia wengine kwa namna yoyote iwezekanayo na naamini uliipigania nafasi hiyo kwa lengo la kuwasaidia vijana kwa vile utakavyoweza.

Comrade mwenyekiti: tukuombe jambo moja ambalo kwa sasa pengine ndio changamoto kubwa zaidi inayowakabili vijana na kwa bahati mbaya si vijana wenyewe wala wazee wetu ambao wameweza kuishughulikia na kuipatia suluhu kikamilifu licha ya jitihada mbali mbali zinazofanyika.

Mkuu; wewe pamoja na timu yako, itapendeza kama mtakaa na kuandaa mkakati mzuri juu ya kutatua changamoto ya ukosefu wa ajira kwa vijana nchini kwani vijana wengi sana wanashindwa kufikia ndoto zao kutokana na changamoto hii.

Mkuu suala hili ni gumu ila linaweza kushughulikiwa na serikali ya Ccm kama ikitia nia nanyi mkawaongoza vijana wengine kuweka input za maana .

Hata hivyo ni vyema vijana wenyewe wakafanya uchambuzi wa changamoto hii na kuwashauri viongozi wa nchi namna ya kukabiliana zaidi na changamoto hii ambayo inazidi kuongezeka kila Siku. Kimsingi, Wewe na timu yako kama ikiwapendezeni, mnayo nafasi nzuri ya kuwaongoza wengine katika hili.

Kuhusu mahali pakuanzia: mambo mawili yaneweza kuzingatiwa ikionekana inafaa.

Kwanza mnaweza kuratibu matamasha ambayo mnaweza kuwakutanisha vijana na watu ambao wanaweza kuwapatia elimu juu ya umuhimu wa kuanzisha miradi yao wenyewe kidogo kidogo, kuweza kuwa " inspire" , kuwa "coach" na kuwa "motivate" ili wapate momentum ya kuanza. Jambo hili nimuhimu sana kwani wengi wana saikolojia ya kushindwa na hili ni tatizo kubwa.

Pili: hii ilishashauriwa huko nyuma kuwa muweze kutengeneza vizuri wazo lililotolewa kuwa, badala ya vijana wote kupatiwa mikopo wakasome chuo kikuu , kisha baada ya hapo zaidi ya 90% wakose ajira ya walichosomea, basi mikopo igawanywe mafungu mawili. Moja wapewe wanaopenda sana kuwa na degree na nyingine wakopeshwe wenye ndoto za kuwa na miradi na makampuni yao. Wazo hili limefafanuliwa vyema humu Jf na litazidi kufafanuliwa kwenye Uzi huu na

Tatu, kutengeneza plan yoyote mtakayoona inafaa kusaidia kukabili changamoto hii.

Mkuu, kama mkifanikiwa kulifanyia kazi jambo hili na likafanikiwa, mtakuwa mumewasadia vijana wenzenu wengi na hakika watawashukuruni. Kadhalika mtaacha alama katika uongozi wenu duniani na kwa Mungu mtakuwa na malipo pia. Ni nini basi mnaweza kufanya na kiwaka na faida kwa vijana kuzidi hili? Kama mkiona jambo hili ni jema basi fanyeni na hakuna atakayejutia. Nawatia moyo kuwa mkiamua mnaweza kufanya jambo kubwa ambalo halikutegemewa.
mapunga mnapongezana hii hatari
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Vyuo vyetu vikuu vinazalisha wahitimu maelfu kwa malaki kila mwaka jambo ambalo ni mafanikio makubwa lakini kutokana na udogo wa sekta rasmi nchini ni wachache tu ambao wanaweza kupata ajira rasmi kulingana na walichosomea kwa sasa. asilimia kubwa ya wahitimu Hawa hawapati ajira na kutokana na mazingira, hujikuta elimu walizopata darasani hazilingani na mazingira ya mtaani na hivyo si tu hujikuta wanashindwa kutumia elimu hizo Bali pia hujikuta wakishindwa kujitegemea na kuweza kuzalisha kwa ajili ya kujikimu na kuleta maendeleo kwa taifa kwa ujumla.wengine hujikuta wakiwa tegemezi tena kwa ndugu zao walioishia lanne, la saba au kidato cha nne.
we we ni kijana mmojawapo jobless sidhani kama unaweza jimudu kimaisha bila kujipendekeza kwa maccm
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Mkuu ikishakuwa ni mada ya wazi tutachangia kwa kuweka maangalizo muhimu kutokana na uhalisia wa mambo, vinginevyo kama ni ya uvccm tu unaweza kuwaomba wakakupa nafasi kwenye vikao vyao vya ndani ukatoa huu ushauri mzuri. Sipingi kwamba ni ushauri mzuri ila kitakachofanyika ni wazo lako kutekelezwa kichama na sio kitaifa.
Mkuu, ilikuwa ni angalizo tu, suala la unawaza nini na unachangia nini linabakia kuwa nivile unavyofikiri mwenyewe
 
Umeandika mambo muhimu sana lkn subiri kwanza arudishe fedha zake alizotoa kumwezesha kushinda.
Mkuu, usiwe unawaza negative kila kitu na usimchukulie mtu vibaya bila kukufanyia ubaya wowote na hata akikufanyia vibaya usiwe mwepesi wa kumwelewa vibaya mtu kwani inawezekana lile afanyalo anafanya kwa dhamira njema.

Kuwa too negative hakuwezi kukusaidia mwenyewe wala kumsaidia mtu mwingine na unapoona jambo halikusaidii na vile vile haliwasaidii wengine, inashauriwa kuachana nalo.
 
Mkuu, nikuombe usiingize habari za uxhaguzi kwenye mada hii maana mada itapoteza muelekeo na kukosa maana. Hapa tujadili ni kwa vipi UVCCM inaweza kusaidia kwa namna moja ama nyingine kukabili changamoto ya ajira kwa vijana. Tukiweka input kwa hili itapendeza zaidi.
Dhumuni/lengo namba moja la CCM ni kushinda uchaguzi kasome katiba yao
 
Dhumuni/lengo namba moja la CCM ni kushinda uchaguzi kasome katiba yao
kwa hiyo wakishashinda uchaguzi hawana tena cha kufanya kama ninyi chadema ambao mnasema eti mnataka kuitoa ccm, mkiulizwa mkishaitoa? hamna maelezo ya maana. Na kama ishu ni kushinda na washashinda mnalia nini sasa? si mtulie! Watu wa jamiii yako ni wakupuuzwa tu.

hamuelewi mnakwenda ama mnarudi.
 
Kwa gharama yoyote ile ikiwemo kupora ushindi kwa kutumia marungu, visu, mapanga na mitutu ya bunduki kama mashambulizi haya yatasababisha vifo vya Watanzania wasio na hatia hawa wahuni na wauaji hawajali.

Dhumuni/lengo namba moja la CCM ni kushinda uchaguzi kasome katiba yao
 
Back
Top Bottom