mtwa mkulu
JF-Expert Member
- Sep 11, 2013
- 8,585
- 11,260
Mida hii maeneo ya Ubungo Polisi wameamua kusheherekea sikukuu ya wajinga kwa kufukuza Machinga wote. Haikuweza kufahamika maramoja nikosa gani wasakatonge Hawa walilifanya lakini wameonekana Polisi hawa wakiwaswaga kama mbuzi wavujajasho hawa huku wakipora mbao na mabati nakupakia katika gari. Sura ya hapa niyakitumwa wananchi wamezunguka wakiwa hawana comment. Vijana wanakimbia na mizigo mizito vichwani huku wakielekezewa mitutu ya bunduki.
Eneo la darajani mamantilie wamekaa porini wakipika vyakula vyao. Gari la FFU lenye askari limeonekana mlimani likienda kuongeza nguvu.vilio vya uchungu vinasikika pia. Sijui Mnyika yuko wapi asaidie wananchi Hawa wasio na dhambi.
Eneo la darajani mamantilie wamekaa porini wakipika vyakula vyao. Gari la FFU lenye askari limeonekana mlimani likienda kuongeza nguvu.vilio vya uchungu vinasikika pia. Sijui Mnyika yuko wapi asaidie wananchi Hawa wasio na dhambi.