Palestina: Hatutaki tena msaada wowote wa Marekani

Papaa Mobimba

JF-Expert Member
Jan 27, 2018
752
3,096
Katibu wa Kamati ya Utendaji ya Harakati ya Ukombozi wa Palestina (PLO) amesema Wapalestina hawataki msaada wowote kutoka kwa Marekani, baada ya Washington kutangaza kuwa itapunguza kiwango cha msaada wake wa kibinadamu kwa wananchi wa Palestina.

Saeb Erekat amesema: "Tumeiandikia barua rasmi Marekani kuitaka isimamishe misaada yake yote kwa Mamlaka ya Ndani ya Palestina, kwa kuwa kukubali misaada hiyo kutakuwa na taathira hasi kwa Wapalestina."

Amesema jambo jingine lililowapelekea kukataa misaada ya Washington ni Sheria ya Kupambana na Ugaidi ya ATCA iliyopasishwa na Rais Donald Trump wa Marekani Oktoba mwaka jana, ambayo inampa uwezo raia yeyote wa Marekani wa kuishtaki taasisi zinazopokea misaada hiyo ya US.

4bps4ec4c034d518vif_800C450.jpg
Shirika la Umoja wa Mataifa la Misaada na Ajira kwa ajili ya Wakimbizi wa Kipalestina UNRWA

Mwaka uliopita, Marekani ilitangaza kukata misaada yake kwa Shirika la Umoja wa Mataifa la Misaada na Ajira kwa ajili ya Wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA), uamuzi ambao ulikosolewa vikali na jamii ya kimataifa, ikiwemo ofisi ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres.

Wadadisi wa mambo wanasema uamuzi wa Marekani wa kukatisha misaada yake kwa Wapalestina ni kujaribu kuwarubuni kimabavu ili wakubaliane na mpango wa "Muamala wa Karne" wa kuitokomeza kikamilifu kadhia ya Palestina.
 
Katibu wa Kamati ya Utendaji ya Harakati ya Ukombozi wa Palestina (PLO) amesema Wapalestina hawataki msaada wowote kutoka kwa Marekani, baada ya Washington kutangaza kuwa itapunguza kiwango cha msaada wake wa kibinadamu kwa wananchi wa Palestina.

Saeb Erekat amesema: "Tumeiandikia barua rasmi Marekani kuitaka isimamishe misaada yake yote kwa Mamlaka ya Ndani ya Palestina, kwa kuwa kukubali misaada hiyo kutakuwa na taathira hasi kwa Wapalestina."

Amesema jambo jingine lililowapelekea kukataa misaada ya Washington ni Sheria ya Kupambana na Ugaidi ya ATCA iliyopasishwa na Rais Donald Trump wa Marekani Oktoba mwaka jana, ambayo inampa uwezo raia yeyote wa Marekani wa kuishtaki taasisi zinazopokea misaada hiyo ya US.

4bps4ec4c034d518vif_800C450.jpg
Shirika la Umoja wa Mataifa la Misaada na Ajira kwa ajili ya Wakimbizi wa Kipalestina UNRWA

Mwaka uliopita, Marekani ilitangaza kukata misaada yake kwa Shirika la Umoja wa Mataifa la Misaada na Ajira kwa ajili ya Wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA), uamuzi ambao ulikosolewa vikali na jamii ya kimataifa, ikiwemo ofisi ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres.

Wadadisi wa mambo wanasema uamuzi wa Marekani wa kukatisha misaada yake kwa Wapalestina ni kujaribu kuwarubuni kimabavu ili wakubaliane na mpango wa "Muamala wa Karne" wa kuitokomeza kikamilifu kadhia ya Palestina.
Kuvuja kwa pakacha nafuu kwa mchuuzi!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna wanaobeza humu kwa kudhani wapalestina wote ni jamii moja kumbe hawajui kuwa ni mchanganyiko wa jamii zaidi moja pole Sana kwao
 
Katibu wa Kamati ya Utendaji ya Harakati ya Ukombozi wa Palestina (PLO) amesema Wapalestina hawataki msaada wowote kutoka kwa Marekani, baada ya Washington kutangaza kuwa itapunguza kiwango cha msaada wake wa kibinadamu kwa wananchi wa Palestina.

Saeb Erekat amesema: "Tumeiandikia barua rasmi Marekani kuitaka isimamishe misaada yake yote kwa Mamlaka ya Ndani ya Palestina, kwa kuwa kukubali misaada hiyo kutakuwa na taathira hasi kwa Wapalestina."

Amesema jambo jingine lililowapelekea kukataa misaada ya Washington ni Sheria ya Kupambana na Ugaidi ya ATCA iliyopasishwa na Rais Donald Trump wa Marekani Oktoba mwaka jana, ambayo inampa uwezo raia yeyote wa Marekani wa kuishtaki taasisi zinazopokea misaada hiyo ya US.

4bps4ec4c034d518vif_800C450.jpg
Shirika la Umoja wa Mataifa la Misaada na Ajira kwa ajili ya Wakimbizi wa Kipalestina UNRWA

Mwaka uliopita, Marekani ilitangaza kukata misaada yake kwa Shirika la Umoja wa Mataifa la Misaada na Ajira kwa ajili ya Wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA), uamuzi ambao ulikosolewa vikali na jamii ya kimataifa, ikiwemo ofisi ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres.

Wadadisi wa mambo wanasema uamuzi wa Marekani wa kukatisha misaada yake kwa Wapalestina ni kujaribu kuwarubuni kimabavu ili wakubaliane na mpango wa "Muamala wa Karne" wa kuitokomeza kikamilifu kadhia ya Palestina.

Shabbash, Nawapongeza sana Palestina kwa hili, marekani wanataka waabudiwe ni nchi za kiislamu ili kutokomeza uislamu lakini pia nchi za kiislamu zionekane nchi dhalili sana duniani.
 
Wanakwepa misaada ya masharti.

Ningependa Mungu anipe miaka 200 hapa duniani ili nije nishuhudie conclusion ya huu mgogoro,
lakini ndo hivyo haiwezekani,tutaondoka duniani na kuuacha huu mgogoro ukiendelea
 
Unapojiangalia kwenye kiyoo unaweza jiona simba gumu kumbe ni paka tu.
Wanaokataa misaada unakuta ni viongozi ambao wanakula Kodi za wanyonge misaada isipokuja wanyonge ndio wanatembelea Ringi la Gari kwenye Barbara ya vumbi yenye mashimo na spring zake ni mbavu badala ya coil.
Watanyolewa bila maji
 
  • Thanks
Reactions: PNC
Wengi hapa tunachangia lakini michango yetu inaonesha wazi hatujui kinachoendelea kule Gaza.Ili kuwa na maoni mazuri, uyaishi yale maisha ya Palestina VS Israel.Hapo utajua jema ni lipi na baya ni lipi.
 
Shabbash, Nawapongeza sana Palestina kwa hili, marekani wanataka waabudiwe ni nchi za kiislamu ili kutokomeza uislamu lakini pia nchi za kiislamu zionekane nchi dhalili sana duniani.
Mkuu Mmarekani yupo Kimaslahi zaidi angekuwa we endelea kuamini tu anataka kuipoteze dini fulani. Halafu angeshaipoteza anafaidika nini? Na angekuwa na mpango huo si angepiga marufuku Uislam ndani ya ardhi ya Marekani?
 
Mkuu Mmarekani yupo Kimaslahi zaidi angekuwa we endelea kuamini tu anataka kuipoteze dini fulani. Halafu angeshaipoteza anafaidika nini? Na angekuwa na mpango huo si angepiga marufuku Uislam ndani ya ardhi ya Marekani?

Marufuku ipi unayotaka?? wanawake wa kiislamu mara kadhaa washavuliwa hijabu hadharan, kwenye ndege waislamu washashushwa mara ngapi, wanabaguliwa na kupigwa mara ngap, nadhan hufuatilii ata wakimbizi waislamu toka nchi za kiislamu wamepigwa marufuku kukanyaga ardhi ya marekani nk. nchi karibu 7 za kiislamu duniani zimezuiliwa visa kuingia marekani.

Trump anataka kuizima serikali ya marekani apate hela ajenge ukuta baina ya marekani na mexico lengo ni kudhibiti waislamu,
wewe sijuwi unaishi dunia ipi.
 
Marufuku ipi unayotaka?? wanawake wa kiislamu mara kadhaa washavuliwa hijabu hadharan, kwenye ndege waislamu washashushwa mara ngapi, wanabaguliwa na kupigwa mara ngap, nadhan hufuatilii ata wakimbizi waislamu toka nchi za kiislamu wamepigwa marufuku kukanyaga ardhi ya marekani nk. nchi karibu 7 za kiislamu duniani zimezuiliwa visa kuingia marekani.

Trump anataka kuizima serikali ya marekani apate hela ajenge ukuta baina ya marekani na mexico lengo ni kudhibiti waislamu,
wewe sijuwi unaishi dunia ipi.


Ukitaka kuchangia hoja kama hizi, hakikisha unaufahamu ulimwengu vizuri.Unaweza kuwa na hoja lakini nimechunguza unavyowasilisha mawazo yako unaonekana huujui ulimwengu , hujui historia wala mifumo ya kiuchumi , siasa na utamaduni.

Mabepari hawana urafiki wala uadui na jambo, jamii, mtu ama dini yeyote hapa ulimwenguni. Wao jambo kubwa ni kujilimbikizia mali kwa halali au njia isiyo halali.Ukimtazama Trump, utasema anaua uilslam ili ukristo utamalaki? Kweli unamuona Trump ni mkirsto kabisaa?

Nilipokuona hujui, ni pale unaposema eti ukuta baina ya Mexico na Us ni kwa ajili ya kudhibiti uislam. Hivi unaijua Mexico wewe? Laiti Trump angekuwa mtetezi wa ukristo angewabagua hao walatino kweli? Walatino kihistoria ni wakatoliki kwa 99%, hiyo asilimia moja pengine ni wageni na imani za asili.Sasa uwapi huo ukristo wa Trump?

Kwa kifupi, Trump anapiga vita uislam si kwakuwa yeye ni mkristo maana hana sifa za ukristo, hata baadhi ya wakristo wanajua hili. Hata wakristo wapo wanaoilaumu US kwa vitendo vyake vya kukiuka maadili na kuangamiza imani za watu ikiwemo ukristo.

Tukifuata mtazamo wako, tutaihukumu vip Saudiarabia? Katika uislam nayo si kama marekani tu? Unaiona inachofanya pale uarabuni? Anashirikiana na huyohuyo US kuhujumu waarabu wenzake.Sasa kwanini Trump asiwapulizie nyuklia Saudia?

Kwa kifupi, mabepari ni adui wa kila mtu.Utakuwa rafiki yao pale tu utakapokubaliana nao au kuwafaidisha.Leo wanataka ulimwengu mzima tuukubali ushoga, kwani watu wote duniani ni waislamu?Wakati huohuo Trump amekataa watu wanaobadili jinsi zao wasihudumu kwenye jeshi lao.Sisi tumewaka ushoga juzijuzi uliona balaa lake, kwani Tz ni serikali ya kiislamu?

Tafakari, chukua hatua
 
Marufuku ipi unayotaka?? wanawake wa kiislamu mara kadhaa washavuliwa hijabu hadharan, kwenye ndege waislamu washashushwa mara ngapi, wanabaguliwa na kupigwa mara ngap, nadhan hufuatilii ata wakimbizi waislamu toka nchi za kiislamu wamepigwa marufuku kukanyaga ardhi ya marekani nk. nchi karibu 7 za kiislamu duniani zimezuiliwa visa kuingia marekani.

Trump anataka kuizima serikali ya marekani apate hela ajenge ukuta baina ya marekani na mexico lengo ni kudhibiti waislamu,
wewe sijuwi unaishi dunia ipi.
Vile vile wakristo wananyanyaswa sana ktk nchi zenye waislamu wengi kama Pakistan, Iraq, Iran, Misri, Sudan nk, au hili wewe hulifahamu.
 
Back
Top Bottom