Mindi
JF-Expert Member
- Apr 5, 2008
- 3,523
- 4,998
Ilikuwa ni siku ya aibu kubwa sana ambayo ni wachache wenye macho waliona jinsi Tanzania tulivyoaibika.
Tanzania, ambayo ni hivi karibuni tu tumetoka katika uchaguzi unaonuka uvundo mkali, ambapo jitihada za makusudi zilifanywa kupora uchaguzi mchana kweupe kwa mbinu mbalimbali chafu (kufunga ofisi wiki nzima, kukamatwa wagombea wanapochukua fomu, wengine kuenguliwa kwa visingizio na sio vigezo, na mengineyo mengi kama hayo).
Tanzania kupitia kwa Profesa Kabudi, ilidiriki kuitaka Kenya kujifunza kutoka Tanzania!
Profesa Kabudi ambaye amejipatia umaarufu mkubwa kutokana na hotuba yake fupi katika sherehe ya uzinduzi wa Ripoti ya BBI huko Kenya, kwa kweli alikuwa katika ubora wake katika usanii.
Baada ya kuwa-lecture Wakenya kuhusu ukabila (ambao serikali ya Magufuli inajitahidi kwa nguvu zote kuufufua, na kuongeza bonasi ya ukanda juu yake), aliwainua na kuwaimbisha wimbo wa kuwataka waachane na mambo ambayo serikali ya Tanzania aliyoiwakilisha inayaenzi na kuyaimarisha; kuwatenga watu katika imani zao za kisiasa, kwa mfano, wakati tunaimba MAENDELEO HAYANA VYAMA.
Lakini kubwa sana ambalo hata Profesa Kabudi na ubingwa wake katika usanii hakuliona, ni ile tofauti kubwa kati ya Kenya na Tanzania.
Kwamba pale kwenye meza kuu kulikuwa na Rais, Makamu wake, na kiongozi wa upinzani. Yaani tuseme Magufuli ameketi beneti kabisa na Mbowe, halafu pembeni yupo mama Suluhu.
Halafu katika ukumbi wamejaa viongozi mbalimbali, lakini hasa viongozi wa vyama vyote vya siasa. halaiki kama hiyo tu haijawahi kutokea hapa kwetu na wala hatutarajii kwamba Magufuli atakuwa na uthubutu wa kuiitisha, japo angekuwa na ujasiri hata tone tu ya ule ujasiri wa Kikwete, angeweza kabisa.
Magufuli amekutana na viongozi wa dini, wafanyabiashara, na makundi mbalimbali lakini anaogopa kukutana na viongozi wa siasa kutoka upinzani, ambao wapo kisheria kabisa, na anaidhinisha kila mwezi walipwe fedha ya ruzuku kutoka makusanyo ya kodi.
Siwezi kufikiria kitu cha ajabu zaidi ya hiki. mwenyewe anasema kwa kejeli eti watamchinja! Pengine kweli akikutana nao watamchinja. KISIASA.
Lakini Rais Kenyata na Mzee Raila wamediriki kukutana na kupeana mikono, baada ya Raila kujitangazia urais wa watu (People's president).
Kenyata anasema mwenyewe haikuwa rahisi. Dakika 45 za mwanzo hakuna cha maana walichoongea, kila mtu amejaa hasira.
Lakini walijifungia ndani na hawakutoka humo mpaka wamepeana handshake. Hivyo Magufuli asifikiri wale ni wajinga.
Mchambuzi mmoja alipoulizwa mbona kuna ripoti nyingi tu huko Kenya kwa madhara yaliyotokea huko nyuma, alijibu kwamba tofauti ya hizo ripoti na hii ni kwamba hii inatokana na msukumo wa kisiasa.
Hivyo uwezekano mkubwa wa kufanya kazi. ni sawa na ile serikali ya umoja wa kitaifa Zanzibar ambayo iliwezekana pale Maalim Seif na Abeid Karume walipokaa pamoja.
Hii ni habari njema sana kwa wapenda demokrasia, wapenda amani, duniani kote. maridhiano ndiyo kauli mbiu.
Ndicho serikali ya Magufuli ilitakiwa kufanya mara tu baada ya kusikia wapinzani wamesusia uchaguzi.
Maridhiano. Siyo kiburi na ubabe. Eti ukisusa siye twala! huko ni kucheza kamari kwa mambo muhimu ya kitaifa.
Wakenya wamefika hapo kwa historia mbaya sana ya chaguzi zao. Na sisi tunangoja tupite humo humo kwenye machafuko? Vinginevyo basi sisi siyo binadamu, ni robots!
Tanzania, ambayo ni hivi karibuni tu tumetoka katika uchaguzi unaonuka uvundo mkali, ambapo jitihada za makusudi zilifanywa kupora uchaguzi mchana kweupe kwa mbinu mbalimbali chafu (kufunga ofisi wiki nzima, kukamatwa wagombea wanapochukua fomu, wengine kuenguliwa kwa visingizio na sio vigezo, na mengineyo mengi kama hayo).
Tanzania kupitia kwa Profesa Kabudi, ilidiriki kuitaka Kenya kujifunza kutoka Tanzania!
Profesa Kabudi ambaye amejipatia umaarufu mkubwa kutokana na hotuba yake fupi katika sherehe ya uzinduzi wa Ripoti ya BBI huko Kenya, kwa kweli alikuwa katika ubora wake katika usanii.
Baada ya kuwa-lecture Wakenya kuhusu ukabila (ambao serikali ya Magufuli inajitahidi kwa nguvu zote kuufufua, na kuongeza bonasi ya ukanda juu yake), aliwainua na kuwaimbisha wimbo wa kuwataka waachane na mambo ambayo serikali ya Tanzania aliyoiwakilisha inayaenzi na kuyaimarisha; kuwatenga watu katika imani zao za kisiasa, kwa mfano, wakati tunaimba MAENDELEO HAYANA VYAMA.
Lakini kubwa sana ambalo hata Profesa Kabudi na ubingwa wake katika usanii hakuliona, ni ile tofauti kubwa kati ya Kenya na Tanzania.
Kwamba pale kwenye meza kuu kulikuwa na Rais, Makamu wake, na kiongozi wa upinzani. Yaani tuseme Magufuli ameketi beneti kabisa na Mbowe, halafu pembeni yupo mama Suluhu.
Halafu katika ukumbi wamejaa viongozi mbalimbali, lakini hasa viongozi wa vyama vyote vya siasa. halaiki kama hiyo tu haijawahi kutokea hapa kwetu na wala hatutarajii kwamba Magufuli atakuwa na uthubutu wa kuiitisha, japo angekuwa na ujasiri hata tone tu ya ule ujasiri wa Kikwete, angeweza kabisa.
Magufuli amekutana na viongozi wa dini, wafanyabiashara, na makundi mbalimbali lakini anaogopa kukutana na viongozi wa siasa kutoka upinzani, ambao wapo kisheria kabisa, na anaidhinisha kila mwezi walipwe fedha ya ruzuku kutoka makusanyo ya kodi.
Siwezi kufikiria kitu cha ajabu zaidi ya hiki. mwenyewe anasema kwa kejeli eti watamchinja! Pengine kweli akikutana nao watamchinja. KISIASA.
Lakini Rais Kenyata na Mzee Raila wamediriki kukutana na kupeana mikono, baada ya Raila kujitangazia urais wa watu (People's president).
Kenyata anasema mwenyewe haikuwa rahisi. Dakika 45 za mwanzo hakuna cha maana walichoongea, kila mtu amejaa hasira.
Lakini walijifungia ndani na hawakutoka humo mpaka wamepeana handshake. Hivyo Magufuli asifikiri wale ni wajinga.
Mchambuzi mmoja alipoulizwa mbona kuna ripoti nyingi tu huko Kenya kwa madhara yaliyotokea huko nyuma, alijibu kwamba tofauti ya hizo ripoti na hii ni kwamba hii inatokana na msukumo wa kisiasa.
Hivyo uwezekano mkubwa wa kufanya kazi. ni sawa na ile serikali ya umoja wa kitaifa Zanzibar ambayo iliwezekana pale Maalim Seif na Abeid Karume walipokaa pamoja.
Hii ni habari njema sana kwa wapenda demokrasia, wapenda amani, duniani kote. maridhiano ndiyo kauli mbiu.
Ndicho serikali ya Magufuli ilitakiwa kufanya mara tu baada ya kusikia wapinzani wamesusia uchaguzi.
Maridhiano. Siyo kiburi na ubabe. Eti ukisusa siye twala! huko ni kucheza kamari kwa mambo muhimu ya kitaifa.
Wakenya wamefika hapo kwa historia mbaya sana ya chaguzi zao. Na sisi tunangoja tupite humo humo kwenye machafuko? Vinginevyo basi sisi siyo binadamu, ni robots!