Padre Mapunda: Dk Slaa mwiba unaowatesa wanasiasa wengine

Padre Mapunda: Dk Slaa mwiba unaowatesa wanasiasa wengine

Amesema Yesu Kristo aliandamwa na uongozi wa Kiyahudi siyo kwa sababu alikuwa gaidi au jambazi, bali kwa sababu alikuwa ni tishio kwa mamlaka na vyeo vyao. Amesisitiza Dr. Slaa anaandamwa na CCM kwa sababu ni mwiba kwao na vyama vyenye mrengo wa CCM vinavyoamini katika siasa zisizo na faida. Kama kiongozi wa chama cha upinzani (Chadema) Dk Slaa ana mvuto wa pekee kwa Watanzania bila kujali dini, itikadi, kabila, vyeo wala tabaka la watu.
=================


Chanzo: Mwananchi

Babu amechoka,mpunzisheni
 
Mimi nimeripoti alichokisema Padre Mapunda, huna haja ya kunilaumu mimi. Yawezekana mimi na hao wenzangu uliowataja ni wazembe kama ulivyosema; unaweza kufafanua huo uzembe?

Hana hoja ya kukuelwesha zaidi ya kutumikia mashetani ccm
 
Kwa hiyo kama Slaa ana matendo kama ya Yesu basi panapo mfaa ni kanisani zaidi kuliko Ikulu!

Lakini si shangai Mapadri kupigiana chapuo...nasubiri mpambano kati ya CUF na Chadema!

Nchi hii haito ongozwa na kiongozi wa dini!

Najua mutataka iongozwe na wezi......Kila la kheri.
 
Huyu Bwana ni nguzo muhimu sana kwa CHADEMA na UKAWA. Endapo ataidhinishwa kuwania Uraisi mchuano utakua mkubwa sana na MaCCM ambao mpasuko wa wazi unanukia tayari katikati yao, kama hautatokea kabla utatokea baada ya uchaguzi kutokana na uhasama na kutovumiliana kunakokua sana ndani yao (wenye macho wanajua sana hili).

Iwe isiwe tuendendako alama za kuimba nyimbo mpya za ukombozi wa pili zinaonekana kwa uwazi zaidi kuliko kipicho chochote cha awali.

Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibariki Africa.

100% ok Sahihi lakini Ukweli huu CCM hawataki kabisa Kuusikia. Tunajua chroquine ni Chungu lakini ni lazima Wapewe, Wameze ili wapone kutokana na gonjwa Sugu linaloenda kuwamaliza (Ufisadi)
 
Ritz,

Usipende sana kujitoa ufahamu.Katika Miaka 15 aliyokua Mbunge ameonyesha kuwa mbunge anapaswa kufanya nini

Tatizo la nchi yetu ni mfumo mbovu wa CCM na tunahitaji overhaul na mtu wa kusimamia hili

Kwa namna ambavyo Dr.Slaa amekua akisimamia maswala ya msingi na kuonyesha weledi wa kiwango cha juu na uzalendo ndiye anayeweza kusimamia haya

Sisemi hivi kwa sababu ni kiongozi wangu kiutendaji isipokua wakati mwingine tuwe realistic

Taifa hili limepoteza mwelekeo kisera na kiitikadi


Yote yaliyosemwa na Father Mapunda ni ukweli mtupu

Na mwaka huu tumejipanga kukabiliana na wale watawala wenye hila katika zoezi zima na kilichotokea kwa wale waliochakachua matokeo ya serikali za mtaa ni rasharasha tu.

Tutawakabili kwa nguvu na kila mbinu ambazo hamjawahi kushuhudia tangu tupate uhuru na tutatoa fundisho kwa mamlaka nyingine Afrika

Haki za kiraia na Demokrasia haziwezi kuhujumiwa kisha wahusika wakapona hivihivi

Watanzania wote tungekuwa kama wewe nch yetu ingekuwa kama USA.
 
Last edited by a moderator:
Amesema Yesu Kristo aliandamwa na uongozi wa Kiyahudi siyo kwa sababu alikuwa gaidi au jambazi, bali kwa sababu alikuwa ni tishio kwa mamlaka na vyeo vyao. Amesisitiza Dr. Slaa anaandamwa na CCM kwa sababu ni mwiba kwao na vyama vyenye mrengo wa CCM vinavyoamini katika siasa zisizo na faida. Kama kiongozi wa chama cha upinzani (Chadema) Dk Slaa ana mvuto wa pekee kwa Watanzania bila kujali dini, itikadi, kabila, vyeo wala tabaka la watu.
=================


Chanzo: Mwananchi

- Chanzo ni lile gazeti lililofungiwa hivi karibuni na Serikali au

Le Mutuz
 
Hoja imetolewa na imeungwa mkono na sasa nitawahoji, wanaoafiki waseme ndiyo, NDIYOOOOOOOOOOOOOOOOOO. Wasioafiki waseme siyo, SIYOO. Walioafiki wameshinda na sasa nawatakia kazi njema mawaziri mkatekeleze hayo.
 
Ritz,

Usipende sana kujitoa ufahamu.Katika Miaka 15 aliyokua Mbunge ameonyesha kuwa mbunge anapaswa kufanya nini.

Tatizo la nchi yetu ni mfumo mbovu wa CCM na tunahitaji overhaul na mtu wa kusimamia hili

Kwa namna ambavyo Dr.Slaa amekua akisimamia maswala ya msingi na kuonyesha weledi wa kiwango cha juu na uzalendo ndiye anayeweza kusimamia haya

Sisemi hivi kwa sababu ni kiongozi wangu kiutendaji isipokua wakati mwingine tuwe realistic

Taifa hili limepoteza mwelekeo kisera na kiitikadi


Yote yaliyosemwa na Father Mapunda ni ukweli mtupu

Na mwaka huu tumejipanga kukabiliana na wale watawala wenye hila katika zoezi zima na kilichotokea kwa wale waliochakachua matokeo ya serikali za mtaa ni rasharasha tu.

Tutawakabili kwa nguvu na kila mbinu ambazo hamjawahi kushuhudia tangu tupate uhuru na tutatoa fundisho kwa mamlaka nyingine Afrika

Haki za kiraia na Demokrasia haziwezi kuhujumiwa kisha wahusika wakapona hivihivi

Kamanda BEN.Kama hiyo mikakati ambayo hujaiweka wazi ya kuwadhibiti wezi wa kura na wavuruga uchaguzi ni mipango ya chama umenifariji sana yasiwe maneno matupu.Na kama ni maneno yako binafsi nakushauri yawasilishe kwa ngazi za maamuzi za CHADEMA na UKAWA ili sisi wapenda mageuzi tujipange kulinda haki zetu.UMENIFARIJI SANA.
 
Last edited by a moderator:
hivi ccm imewatuma kutetea dini gani? Ccm imewatuma kupinga dini gani? Hivi ccm inapigania dini gani? Mnataka kusema chochote kinachofanywa ndani ya ccm tukiangalie kwa jicho la kidini?

Bila shaka CCM ni freemason maana wanakosoa ukristo na uislam
 
huo udini utakufikisha wapi? Tuna waislam na hata wasiokua na dini ndani ya chadema

mlisema chadema ni cha wakristo kisha cuf ya waislamu sasa cuf na chadema vyama vya wakristu na waislam wameungana ina maana ccm ni chama cha wapagani?

Achana na siasa hizi kaka.nigeria hali tete kwa sababu ya ujinga huu

wanaipenda hii kitu ile mbaya
 

Attachments

  • 10336612_545165245628195_3467653945436958435_n.jpg
    10336612_545165245628195_3467653945436958435_n.jpg
    47.9 KB · Views: 107
Back
Top Bottom