Orodha ya diss tracks za kibongo, Sehemu ya Kwanza

Orodha ya diss tracks za kibongo, Sehemu ya Kwanza

LIKUD

JF-Expert Member
Joined
Dec 26, 2012
Posts
19,349
Reaction score
36,304
A diss track or diss song is a song primarily intended to disparage or insult another person or group. While musical parodies and attacks have always existed, the trend became increasingly common in the hip hop genre as part of the hip hop rivalry phenomenon.

Ninakuletea orodha ya DISS TRACKS za kibongo kuanzia mwaka 1999/2000 to date. Katika diss tracks hizo zipo tracks ambazo msanii fulani ana mdiss msanii mwingine katika wimbo mzima ama katika baadhi ya mistari iliyomo katika wimbo huo. Na inaweza kuwa diss ya moja kwa moja au subliminal. Inaweza kuwa diss kwa msanii wa muziki, msanii wa maigizo , kiongozi au mtu yoyote maarufu.

1. MTULIZE : MABAGA FRESH DISSING INSPECTOR HAROUN & GANGWE MOBB.

Kwanza nianze kwa kuelezea chanzo cha beef kati ya Mabaga Fresh na Inspector Haroun.Sometimes in 1999 Mabaga Fresh waliandaa show katika ukumbi mmoja wa burudani uliopo Temeke. Waliwaalika Gangwe Mobb kipindi hicho wanawika na ngoma kadhaa kama Ngangari, Mauzauza na MtuBee. Makubaliano yalikuwa malipo yatategemea na idadi ya watu watakao ingia kwenye show. Show ilitema, mtu kibao zilihudhuria show, ila kwenye malipo, Mabaga Fresh wakawaambia Gangwe Mobb , wamepata hasara, hela yote iliyo ingia wamelipia ukumbi na mambo mengine, so wakawatoa jamaa shilingi Mia Tano ( Jero). Gangwe Mobb walimind sana na hawakuwa na uwezo wa kuwapiga jamaa kwa sababu jamaa ni walemavu and all that. Kuanzia siku hiyo Mabaga Fresh wakawa Paka na Chui na Gangwe Mobb ingawa wote walikuwa kwenye koo la WALUMENDAGO.

Katika wimbo Mtulize ambao Mabaga Fresh waliurekodi kwa mara ya mwisho (Walishaurekodi zaidi ya mara mbili ) mwaka 2000 kuna mistari inasema;

J.B (Yule mwenye sauti nyembamba ) anasema " MBELE YA CHOMBO CHA DOLA HAKUNA CHA NGANGARI"…………Hapa ana diss wimbo Ngangari wa Gangwe Mobb.

Mstari mwingine, DJ SNOXX ( Yule mwenye sauti nene ), anasema; "NGEDERE NIAZIME SURA YAKO NIMTISHIE MWANANGU".

Hapa DJ SNOXX ana mock muonekano wa sura ya Inspector Haroun kwa kumfananisha na ngedere.

2. NIPO GADO ORIGINAL ( INSPECTOR HAROUN DISSING JB WA MABAGA FRESH VIA ZAY B ).

https://rubega.com/index.php?a=track&id=503 sikiliza hapa wimbo wa NIPO GADO REMIX, ZAY B FEAT INSPECTOR HAROUN

Katika wimbo huu, kuna mstari Zay B anasema " KUBWA ZIMA KIKOJOZI, UKIULIZWA OOH NIMEPITIWA NA NJOZI "

Kwenye wimbo MTULIZE (ambao waliurekodi kwa mara ya kwanza), kuna mstari JB anasema " MI SIO KIKOJOZI, ILA TU NILIPITWA NA NJOZI "

So hapa Inspector Haroun alikuwa ana mdiss JB kwa kumtumia Zay B kwenye wimbo huu. Vile vile katika wimbo huu kuna mistari Inspector anasema " MI NDO NYANI , WA MWITUNI, PORINI, STERING………….". Hapa Inspector alikuwa anamjibu DJ SNOXX kwa kumwambia kuwa yeye NI NYANI akiwa na lengo la kumuonyesha kuwa hata tatizo na yeye kuitwa Ngedere.

3. NIPO GADO REMIX …………ZAY B & JUMA NATURE DISSING INSPECTOR HAROUN.

Sehemu kubwa ya wimbo huu, anasikika msanii Zay B akimdiss Inspector, baadhi ya mistari maarufu ambayo Zay B anamdiss Babu katika wimbo huu ni pamoja na;

i. " DOMO KA CHAI JABA" …Hapa Zay B ana mock muonekano wa Inspector Haroun.
ii. " KILA UKIPITA SEHEMU ZA WATU KUJICHEKELESHA"…..Hapa Zay B ana mock tabia ya Inspekta kupenda kucheka cheka.
iii. " WATU HAWACHOKI WAMENUNA, WAMECHOSHWA NA UREMBO WA SANAA, UNAAAMBUKIZA KINYAA "….Hapa Zay B anaponda style ya kurap ya Inspekta.
iv. ‘MI NAHISI WENZAKO WANAKUGONGA" …Hapa Zay B anamtukana Inspekta matusi ambayo wanwake huwa wanawatukana wanaume pindi wanapo kosana.

images

Inspector Haroun.

1224788589_nature_haroun.jpg

Inspector Haroun akiwa na Juma Nature.

Katika wimbo huu huu kuna mstari anasikika Juma Nature akisema " SUMBUA AKILI KIJANA USINIIGE MIMI , UTALOST , SI MTU KAWAIDA NIPO JELA NA SHIDA"…….Hili lilikuwa ni dongo kwa Inspector Haroun kuhusiana na beef lao kwamba nani kamuiga mwenzake (Ikumbukwe kuwa Juma Nature na Inspector walikuwa wana beef la kugombea staili yao ya kuchana iliyokuwa inafanana sana huku watu wakijiuliza nani kamuiga mwenzake).

zay_4%5B1%5D.jpg

Zay B.

4. COMPLEX ( R.I.P ) DISSING GANGWE MOBB ;

Katika wimbo wake ( Jina limenitoka ) anasikika Complex akisema " Nimekwisha pita vyeo vyote, Uinspekta, na Uluteni now am a field marshall so u better salute me ".

Kulikuwa na kutokuelewana kati ya Inspector Haroun na Complex kwa sababu Complex alikuwa anashirikiana na Zay B ambaye alikuwa na beef na Inspekta.

COMING UP NEXT;

5. Gangwe Mobb Dissing Zay B & Juma Nature.
6. Juma Nature dissing Inspector Haroun.
7. East Coast dissing TMK Artsists.
8. GWM dissing East Coast.
9. Inspector Haroun dissing East Coast.
10. Wanaume family dissing Inspector haroun.

11. Chege Chigunda dissing Inspector Haroun.
12. Kikosi cha Mizinga dissing Fid Q, Profesa Jay, Bamboo, Chid benz, P.funk, Ving'oko, Langa (RIP), Babuu, Miraji Kikwete, Dudubaya and TMK Artsists.
13. Profesa jay dissing Kalapina.
14. Mangwea ( r.i.p) dissing Kalapina.
15. Chid benz dissing Kalapina.
16. Luteni kalama dissing Inspectpor Haroun.
17. Inspector haroun dissing Luteni kalama.
18. Inspector haroun dissing TMK Wanaume.
19. Juma nature respond to a Inspector haroun dissing Luteni Kalama (Juma nature dissing Inspector haroun on behalf of luteni kalama )
20. Langa (RIP) dissing Kalapina & Kikosi cha Mizinga.

21. Piggy black dissing Dudu baya.
22. Nyandu Tozzy & Chidy benz dissing Dudubaya.
23. Dudubaya dissing Nyandu Tozzy.
24. Rado dissing Fid q.
25. Joh makini dissing Fid q.
26. Fid Q dissing Joh Makini.
27. Ibra da hustler dissing Mapacha.
28. Nako 2 nako dissing Watengwa.
29. Umbwa lutuno wa watengwa ( dissing all hiphop artists from Dar es salaaam )
30. Roma dissing Joh makini.

31. Mansu-li dissing Hermy b.
32. Dully sykes dissing Mwana FA.
33. Sister P dissing Mwana FA.
34. Wandago dissing Mwana FA.
35. Inspector Haroun dissing Mwana FA.
36. Mwana FA dissing Inspector Haroun.
37. Profesa Jay dissing Fid Q.
38. Sister P. Dissing Zay B.
39. TMK Wanaume Halisi dissing TMK Wanaume Halisi.
40. TMK Halisi dissing TMK Wanaume.

41. Inspector Haroun dissing Mh. Temba.
42. Juma Nature dissing Sintah.
43. Bwana Misosi dissing Sugu.
44. Sugu dissing Mwana FA.
45. Dani msimamo dissing Mwana FA.
46. Neck brakers dissing Solid Ground Family.
47. Da Jo dissing Zay B.
48. Profesa Jay dissing Piggy Black.
49. Profesa Jay dissing Inspector Haroun.
50. Gangwe Mobb dissing Profesa Jay, Solo Thang, Mike Tee & Other artists.
51. Solo thang dissing inspector haroun, luteni kalama, k.r. And juma nature.
52. Juma nature, k.r, and mangwea (r.i.p) dissing kalapina & kikosi cha mizinga.
53. Bou nako & fidoo dissing kalapina.
54. Fido & vatoloco dissing kalapina & joh makini.
55. Ibra da hustler dissing joh makini ( in the interview ).
56. Nako 2 nako & other artists dissing kikosi cha mizinga.
57. Kalapina dissing wema sepetu & lulu.
58. Juma nature dissing sintah.
59. Solo thang dissing Farida Wanjara & Wema Sepetu.
60. Lady jay dee & Profesa jay dissing Ruge & Kusaga.

61. Chid benz dissing kala pina.
62. Jay moe dissing zaharani.
63. Sugu dissing inspector haroun.
64. Bwana misosi dissing Sugu.
65. Roma mkatoliki dissing Augu.
66. Pablo wa Daz nundaz dissing Ferooz wa Daz nundaz
67. Daz nundaz dissing Daz baba wa daz nundaz.
68. Other artist , blue & geeez mabovu dissing Diamond & Ommy dimpoz.
69. Lord eyez dissing Ommy dimpoz.
70. Profesa Jay dissing Fanani.

Na nyingine nyingi…..

WAPENZI Wa muziki wa Bongofleva/Bongo Hip hop, endelea kufuatilia uzi huu..........
 
Kilio changu - wimbo wa solothang,kuna mistari alikuwa anamdiss shigongo .....pale aliposema ''wengine wanirubuni eti nashindania gari/kumbe wameshapanga wampe nani toka awali..........sintorudia kosa hata zawadi waweke meli,waongeze ghorofa mbili wanikabidhi na shell
 
Dis la roma 2 sugu ni lip hlo!

Kwenye wimbo wa Roma 2030 kuna mstari anasema " Pesa ndo ilimaliza vita ya Ruge na Sugu", hapa Roma anamaanisha kuwa harakati zote alizokuwa akizifanya SUGU kwenye Anti-Virus na Vinega ilikuwa ni kwa sababu ya njaa. Roma ana tuambia kuwa Sugu alikuwa akipigania maslahi yake binafsi na sio ya wasanii wengine wa Tz ndo maana alikubali kumaliza beef baada ya kulipwa pesa na Ruge. Hapa kwa maana nyingine, Roma anatuambia kuwa Sugu ni mtu anayeweza kununulika. Ndio maana, SUGU took offence on this, alipokuwa anahojiwa na Sam Misago kwenye FNL aliuponda sana mstari huu wa Roma na kumuita Roma sio emcee.
 
Diss y N2N to Watengwa? Hapana..iko mashaka hapo! Sidhan kama wanako kama kundi waliweza kuwa diss watengwa kama kundi. Labda artist mmoja mmoja within they group.

Mnamo mwanzoni mwa miaka ya 2000, tasnia ya muziki wa Hiphop jijini Arusha ilishuhudia ugomvi mkubwa kati ya kundi la Nako 2 Nako lenye maskani yake Kaloleni ( Ololoo ) dhidi ya kundi la muziki wa Hiphop la Watengwa lenye maskani yake katika eneo la Kijenge Juu kipindi hicho likiongozwa na Umbwa Lutuno. Nitaelezea kwa kinaga ubaga chanzo cha ugomvi huu hapo baadaye. Moja kati ya hooks zilizokuwa zinawatumbilisha watengwa ni " huuuuuuuuuuu! katika nyimbo zao/ freestyles zao na live shows zao..Kwenye wimbo Hawatuwezi by N2N kuna mistari Lord EYEZ anasema " Game ngumu, nabadilikia humuhumu, nasukuma hiphop gurudumu nakomaa humu humu, nazidi kutema sumu, game ngumu, commercial niggaz wana pumu, mistari inawahukumu, hawajui wanachosema, kwenye show wanahema, wamechoka mapema, flows zao za KIHUUUUUUUU"

Hii ilikuwa ni diss kwa Watengwa.
 
Mnamo mwanzoni mwa miaka ya 2000, tasnia ya muziki wa Hiphop jijini Arusha ilishuhudia ugomvi mkubwa kati ya kundi la Nako 2 Nako lenye maskani yake Kaloleni ( Ololoo ) dhidi ya kundi la muziki wa Hiphop la Watengwa lenye maskani yake katika eneo la Kijenge Juu kipindi hicho likiongozwa na Umbwa Lutuno. Nitaelezea kwa kinaga ubaga chanzo cha ugomvi huu hapo baadaye. Moja kati ya hooks zilizokuwa zinawatumbilisha watengwa ni " huuuuuuuuuuu! katika nyimbo zao/ freestyles zao na live shows zao..Kwenye wimbo Hawatuwezi by N2N kuna mistari Lord EYEZ anasema " Game ngumu, nabadilikia humuhumu, nasukuma hiphop gurudumu nakomaa humu humu, nazidi kutema sumu, game ngumu, commercial niggaz wana pumu, mistari inawahukumu, hawajui wanachosema, kwenye show wanahema, wamechoka mapema, flows zao za KIHUUUUUUUU"

Hii ilikuwa ni diss kwa Watengwa.

Kabla ya nako 2 nako na watengwa kulikuwa na hardical unit. Lord eyez na Jcb wakiwakilisha. Then chindo katoka nairob huko ndo akaanzisha watengwa na jcb, lord akaja na n2n. Hapakuwa na bifu coz wote ni washkaj.

kipind hicho walikuwa wanashindana ku freestyle 2 na ubabe wa kila kundi na territory yao..viwanja kama crystal na b.o.t club ndo ilikuwa kilingine.

Sasa hyo bifu yao ilizimwa vip manake kipindi kikosi wamewazingua nako, watengwa waliwapa support nako japo watengwa walikuwa washapiga track na kikosi.
 
5. GANGWE MOBB DISSING ZAY BE & JUMA NATURE:

Katika wimbo " VIDONGE VYAO " walio mshirikisha marehemu Nasma Khamis Kidogo, Gangwe Mobb wanasikika waki wadiss wasanii na watu kibao ambao kwa mujibu wa Gangwe mobb, walikuwa wana wafanyia fitna. Wasanii walio disiwa katika wimbo huu ni pamoja na Zay B na Juma Nature.

" Kupanda chati kwa jina la Inspeector Haroun watu wana anza kuponda " mstari huu wa Inspketa unawalenga Zay B na Juma Nature. Zay B kama inavo eleweka kwa watu wengi alifahamika kwa watanzania baada ya kufanya collabo na Inspekta kwenye wimbo NIPO GADO ( Original ), na Juma Nature, kwa mujibu wa Inspekta alijulikana kwa sababu alikuwa anatumia staili ya Inspekta kurap, so Inspekta alikuwa anaamini kuwa Juma Nature amejulikana kwa sababu ya kutumia staili yake. Akifanyiwa mahojiano na gazeti moja mnamo mwaka 2001 na kuulizwa anamzungumziaje Juma Nature, Inspkta alisema anamjua Juma Nature kama msanii mwenye uwezo mkubwa wa kuiga sauti yake, na ni msanii aliyefanikiwa kutangaza sanaa yake kwa kutumia jina staili ya Inspekta. Kwa ufupi huo mstari ulikuwa ni majibu kwa wimbo " Nipo Gado Remix " wa Zay B na Juma Nature..
 
6. JUMA NATURE DISSING INSPECTOR HAROUN KWENYE WIMBO " JINSI KIJANA "

Wimbo wa Jinsi Kijana ulitoka mnamo mwaka 2001 mwishoni, kipindi hicho beef kati ya Juma Nature na Inspekta Haroun ndo lilikuwa limepamba moto. Wasanii hawa walikuwa wanatoleana maneno ya kutambiana kwenye vyombo mbalimbali vya habari kama vile redio na magazeti. Wimbo wa Jinsi Kijana una muonya kijana wa kitanzania mweny tabia zilizo kinyume na maadili ya mtanzania, lakini hata hivyo ndani ya wimbo huo, kuna mistari inayo mdiss Inspekta " Vurugu zako za siri kuwa ni mtu ubinafsi,........." Hapa Juma Nature anaponda tabia ya Inspekta ya ubinafsi kwenye sanaa, ( Habari zilizokuwepo miongoni mwa wasanii wa muziki wa bongo fleva kipindi hicho ni kwamba Inspekta alikuwa mbinafsi sana kwenye gemu, alikuwa anataka asikike na kuonekana yeye tu, hata kwenye kundi lake la Gangwe Mobb, verse nyingi alikuwa anaimba yeye, rejea wimbo kama Mtoto wa Geti Kali, Luteni karama anasikika tu akiitikia " Kachumbari".

Mstari mwingine Juma Nature anasikika akisema " Na palipo na watu wengi hakosi kuwa adui, adui mfano wa nduli kakosa tabia nzuri " .

Hapa Juma Nature alikuwa anamponda Inspekta kuhusu tabia yake ya kutoelewena na wasanii wenzake wengi na ubinafsi, asilimia kubwa ya wasanii wa bongofleva walikuwa na beef na Inspekta.

Vilevile Juma NATURE anamalizia kwa kumwambia Inspekta" Najua inakuuma moyo unapo sikiliza hili song,unatamani uzime redio usisikilize mi sichongi"
 
Hebu nifafanulie dis ya profsa jay na fid q

Kwenye wimbo " Hapo Vipi" , kuna mstari Profesa Jay anasema " Huu ni muhimili, wangapi mmewabashiri nakuwavisha mataji kwa vina vya TAFSIRI"... Hii ni subliminal diss kwa Fid Q kwa sababu yeye ndio mfalme wa mistari ya kutafsiri. Anacho kifanya Fid Q huwa ni kusoma vitabu, halafu ana pick punch lines kwenye hivyo vitabu, kutifasiri kwa kiswahili na kuvitengenezea vina. Ukiungalia kwa haraka haraka huu mstari unaweza kudhani Profesa Jay anawadiss Shigongo na Afande Sele, lakini kiuhalisia hii ni sublminil diss kwa Fid Q kwa sababu, Afande Sele huwa hatafsiri mashairi. Muulize Joh Makini, and he will tell u u dat
 
dah Likud,thanks mkuu,umenifurahisha sana una knoweledge ya kufa mtu nikipata muda nitakuuliza maswali fulani kuhusu baadhi ya wanamuziki na beef zao
 
Kwenye wimbo " Hapo Vipi" , kuna mstari Profesa Jay anasema " Huu ni muhimili, wangapi mmewabashiri nakuwavisha mataji kwa vina vya TAFSIRI"... Hii ni subliminal diss kwa Fid Q kwa sababu yeye ndio mfalme wa mistari ya kutafsiri. Anacho kifanya Fid Q huwa ni kusoma vitabu, halafu ana pick punch lines kwenye hivyo vitabu, kutifasiri kwa kiswahili na kuvitengenezea vina. Ukiungalia kwa haraka haraka huu mstari unaweza kudhani Profesa Jay anawadiss Shigongo na Afande Sele, lakini kiuhalisia hii ni sublminil diss kwa Fid Q kwa sababu, Afande Sele huwa hatafsiri mashairi. Muulize Joh Makini, and he will tell u u dat

mi nadhani kutafsiri k2 na kukitengnezea punch line sio kitu kibaya coz kwa mziki wa kisasa hakuna msanii anaekuja na primary data karibia wote wanatumia secondary data iwe kwa namna moja au nyingne. Kwahyo mi sion hatari mzazi fid q kuchukua baadhi ya maandiko vitabuni na kutafsiri. Ingekua anachukua nyimbo za w2 anatafsiri hapo ningemdisi.. Huyo joh makini mwenyewe unayesema anajua namna fid anavotafsiri yeye mwenyewe anaiga style za kina jiga za kuflow... Yote kwa yote dis sio lazima iendane na ugonvi ni namna ya changamoto 2 ktk game. Mfano mzuri fid alivosema hamjui nash mc. Nash akaja na ngoma maswali ya waki akamdisi fid akasema. "wasanii wanaosema hawanijui hawanisumbui hao wakuja, wamekuja mjini na lifti ya lori la pamba".
 
mi nadhani kutafsiri k2 na kukitengnezea punch line sio kitu kibaya coz kwa mziki wa kisasa hakuna msanii anaekuja na primary data karibia wote wanatumia secondary data iwe kwa namna moja au nyingne. Kwahyo mi sion hatari mzazi fid q kuchukua baadhi ya maandiko vitabuni na kutafsiri. Ingekua anachukua nyimbo za w2 anatafsiri hapo ningemdisi.. Huyo joh makini mwenyewe unayesema anajua namna fid anavotafsiri yeye mwenyewe anaiga style za kina jiga za kuflow... Yote kwa yote dis sio lazima iendane na ugonvi ni namna ya changamoto 2 ktk game. Mfano mzuri fid alivosema hamjui nash mc. Nash akaja na ngoma maswali ya waki akamdisi fid akasema. "wasanii wanaosema hawanijui hawanisumbui hao wakuja, wamekuja mjini na lifti ya lori la pamba".

Ila Fid Q amezidi, anakopi sana., hana tofauti na Mwana FA, unajua ni bora kuiga staili ya flow kuliko kuchukua mistari na kuitafsiri ni mbaya sana kaka. Ila nimeipenda sana hiyo diss ya Nash kwa Fid
 
Ipo na ukiskiliza album ya Watengwa FULL ILE LAANA mixtape 3 wamewajb nako hadi kuna sehemu JCB anasema n2n wataenda na chupi za dada zao bafuni

Hata Lord Eyez kuna ngoma moja kafanya, anamwambia Jay, " Umefurahishwa na nini, mazoea ndo kitu sipendi" . Alikuwa anajibu track ya Jay " Nimefurahishwa "
 
Vipi kuhusu M-LAB MUSIC,TAMADUNI MUSIC ikiwakilishwa vyema na SONGA,MOKO WA MIUJIZA,6 O'CLOCK,KAD GO,AZMA,GHETO AMBASSADOR,SHASHOW,CLIFF MITINDO,STEREO,YOUNG KILLA,NIKI MBISHI mbona hawa hujawazungumzia? Esp.Niki wa II VS MBISHI,na bifu ya NAY WA MITEGO VS NIKI MBISHI VS FID Q VS BUMKUBAM WEUSI
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom