Original komedy kwishiney

Status
Not open for further replies.
Ndiyo maana wengi wanajihusisha na masuala ya muziki like Joti(mchakamchaka) na Mpoki(shangazi)...na tayari single zao ziko sokoni...ukute walishajua kwamba kikinuka huku wataibukia kule...si tayari washakuwa maarufu.
Na Masanja ni mtangazaji wa Times FM..
 

hahahahahaha! Hiyo kali.
 
Hawa walijisahau wakatema bigijii kwa karanga za kuonjeshwa!!!
 
Ni vibaya kuwaombea vijana wenzako mabaya!

Ila wenyewe walivyokuwa wanawaombea na kuwasanifu watu wenzao kila kukicha?
Ni wao ndio walitunga habari ya kufulia kwa kuwaonyesha watu wenzao na kuwacheka kuwa wamefulia au tumesahau sasa?
 
ni trend kwa wasanii wa bongo.. inasikitisha wakipata majina wanabadilika na kuwa na dharau.. sio hawa tu.. mnakumbuka Hasheem Thabeet nae alipokuja hapa na kuchonga kwamba hakuna aliemsaidia kufika huko alikofika..? matokeo yake na huko NBA akashindwa kucheza na kushushwa daraja.. my take ni wasanii kujenga nidhamu ya kuwa na heshima kwenye jamii.. hata kama wameudhiwa.. waweke uungwana katika kushughulika na maudhi..
 
Mzee mengi atawasamehe tu wakitubu maana hawajua watendalo!
 
wamefuliiiiaaaa........... kula la leki..... back to the street.
walikuwa na dharau sana hawa. sipendi hata kukumbuka.
japokuwa napenda japo waoneshe kipindi cha umefulia....
kikiwahusu wao.
 

hahaha aisee mi wameshaniabisha zaidi ya mara tatu kwa kukaa kwa ndugu mpaka naogopa kipindi chao,sheee.nz taip
 
Hawa vijana walikosea sana kumtukana mzee Mengi, watubu na waombe msamaha.
 
Hawa vijana walikosea sana kumtukana mzee Mengi, watubu na waombe msamaha.


who is Mengi bana?? nchi hii mtamfanya kila mtu mtume sasa

wale wana maisha yao, hata wasipoonekana kwenye TV,

nani asiyeogopa maisha?? nani ana hakika ya siku zijazo?

Nishindwe kusema ukweli leo ili nikiharibikiwa nirudi kwa aliyenikosea??

chai hizi mnajianika na pumba zenu, ndiyo akina Lamwai, kabourou, n.k wanafanya kama nyie mnavyosema yet mnawaita wasaliti!
 
Waberoya......Umemaliza aisee
 
Kama kweli walimtukana Mengi hata kama hawataenda kumuomba kazi,waende kumuomba radhi kwawalilofanya.Lasivyo watapotea kabisa kwenye fani!
 

Mkuu unajua wengi hatujui kwa nini waliamua kumdharau yule mzee hadharani vile'lakini walikosea bana'labda hawana washauri'tatizo letu watanzania hatuna vision kama wakenya wanavyodai'walikuwa na nafasi nzuri sana ya kufika mbali yaani ilikuwa iwe kazi ya kudumu forever'aaah lakini Mkuu wale jamaa hawana elimu bana!
 
hahaha aisee mi wameshaniabisha zaidi ya mara tatu kwa kukaa kwa ndugu mpaka naogopa kipindi chao,sheee.nz taip

Hawa jamaa hautakiwi kuangalia kipindi ukiwa umeenda kwa:
1.Shemeji'ko
2. Mjomba'ko
3. Ukiwa na mkwe wako
4. Unaangalia kipindi kwa jirani'ko
5. Ma house girl/boy ndo walikuwa wanapondwa kinoma af bado walikuwa wanakipenda kweli hcho kipindi.
La sivyo utatoka kuangalia kipindi na aibu kibao ka una roho nyepesi
 

Uko sawa kabisa vituko show ya channel ten inakimbiza mbaya. Akina king majuto, sharo milionare, na yule teja wananiacha hoi.
 
Last edited by a moderator:

Mkuu mimi simtetei Mengi wala siwachukii hawa vijana ila nilimaanisha kuwanasihi watu wote kua tunapokua na mgogoro na mtu ni vizuri kuyamaliza kibinadam badala ya kutoka nje na kuanza kumtusi mwenzio. BTW "OK" bado wanapendwa na watu wengi, hivyo wafanye hima kukilinda kikundi chao ili kisipotee kabisa aidha kwa kutafuta channel nyingine au ku-renew mkataba wao pale tbc. Na watakapo renew mkataba au kupata channel nyingine basi wajitahidi kubalance stori zao wasiegemee upande mmoja maana pamoja na kuburudisha wanaelimisha pia, Asante kwa maoni yako, nimeelewa.
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…