Operation UKUTA: Hit n run tactic

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,461
Reaction score
829,860
Kwenye uwanja wa vita kuna mbinu nyingi za kumshinda adui...ukiona adui yako analeta ubabe unabadili mbinu....hapa unaachana na ile ya piga nikupige
Vita ya mtaa kwa mtaa ndio vita ngumu zaidi kwakuwa hapa silaha nzito zile za kwenye uwanja wa vita hazitumiki tena.

Vita ya mtaa kwa mtaa ni vita inayohitaji werevu na mbinu makini..wengi hushindiwa hapa....Kwenye ulingi wa kisiasa nako kuna vita...Kuna vita ya
Sera, Propaganda, Vipaumbele, Kukosoana, Vita ya kumchosha mpinzani wako nk nk

DHIMA YA UKUTA

Dhima ya UKUTA ni kujijenga kisiasa, kujitangaza zaidi, kusikika zaidi na kumpoteza mpinzani
Ni neno lililoandaliwa kimitego, likiwa na utata fulani kwa tafsiri za kihuni, na mpinzani bila kujitambua akanasa kwenye huo mtego

Kwa kukosoa operation nzima na kukekeli neno UKUTA mpinzani hajui kuwa anasaidia kukitangaza chama buuuree...mkakati wa operation nzima umetolewa hadharani karibia miezi miwili kabla ya kufanyika..miezi miwili ni kipindi mkakati kisiasa kummaliza mpinzani

Sasa hivi ni UKUTA kila kona, mpinzani baada ya kufanya yake ni yeye na UKUTA kila uchao...Operation UKUTA imemlazimisha mpinzani akajinadi upya kwa wananchi kama yuko kwenye kampeni, mbinu ya kumchosha na kummaliza nguvu na kumpotezea muda

Operation UKUTA imevuta hisia za wengi na kuwaingiza wengi kwenye mjadala wakiwemo taasisi mbalimbali za serikali na NGOS tofauti
Sasa hivi mpinzani hasikiki tena, bali bila kujitambua amekuta anachezeshwa ngoma juani huku mwenzake akiwa pembeni kivulini kajaa vicheko

Operation UKUTA hata isipofanyika lakini kwenye medani za siasa na propaganda itakuwa imefanikiwa sana. ..
 
Inawezekana kuwa imefanikiwa kujijenga ila kumbuka imepunguza imani ya jeshi la polisi/vyombo vya ulinzi kwa wapinzani. Ndiyo maana tundu lissu alisema mahabusu si pahala pazuri. Nyie mashabiki mtaona sawa ila viongozi wenu wanakipata cha moto.
 
Inawezekana kuwa imefanikiwa kujijenga ila kumbuka imepunguza imani ya jeshi la polisi/vyombo vya ulinzi kwa wapinzani. Ndiyo maana tundu lissu alisema mahabusu si pahala pazuri. Nyie mashabiki mtaona sawa ila viongozi wenu wanakipata cha moto.
Mudawote jitahidi sana kumuelewa Lissu, jifunze kumuelewa yule mtu...angalia mwisho wa siku alivyoibwaga serikali na jopo lake lote na wanasheria wake wote
Jeshi la polisi Na hizo organs nyingine zitatamba mitaani na kujeruhi miili lakini sio dhima, nia na focus ya kile kilichokusudiwa...
Niumize mtaani kwa virungu ila nakusubiri kwenye sheria
 
Hakika lengo limekwishafanikiwa kwa asilimia kubwa kabisa. Nakumbuka vijana kadhaa tu hapo July waliketi mezani, wakaongea na wanahabari, hakika tulishuhudia namna jeshi letu ka polisi lilivyo imara, namna jeshi lilivyosheni vifaa lukuki! Tulishuhudia pia namna jeshi letu lilivyosheni watoa kauli kali kweli kweli!

Sasa wakaketi wakubwa wa wale vijana katika kikao chao. Hapo wakatoka hadharani na kutangaza operation UKUTA. Tangazo lililowachukua dakika kadhaa tu. Hakika tumeshuhudia kuanzia state house, Ma-RC, Ma-DC, wakuu mbalimbali wa jeshi letu la polisi kwa hakika hawalalii!

Kuna haja ya kufikia huku? (Kutolala against UKUTA) kwa nini "tusikeshe" kupambana na kero mbalimbali kama tulivyojipambanua? Na hii ya kukesha kutatua kero za wananchi si kwamba ingekuwa silaha madhubuti tena ya muda mrefu? UKUTA!!
 
mshana jr, tatizo siasa wanazoendesha upinzani si za kujenga. Hivi wewe unadhani kwa nini lowasa aliwaita chadema ni wanaharakati??? Hivi unadhani lowasa anafurahi hii hali??? Hivi lowasa unadhani anataka kushindana na rais??? Kama ulimsikiliza siku za karibuni alisema rais anafanya vizuri......, ila akina mbowe, lissu etc wao kila kukicha wanamtukana na kumdharau na kutaka kupambana na mamlaka ya rais, ilhali hawajui mamlaka yake, na ndiyo maana uadui umeongezeka kumbuka unapmtukana rais unatukana watanzania na vyombo vyake vyote
 
Inawezekana kuwa imefanikiwa kujijenga ila kumbuka imepunguza imani ya jeshi la polisi/vyombo vya ulinzi kwa wapinzani. Ndiyo maana tundu lissu alisema mahabusu si pahala pazuri. Nyie mashabiki mtaona sawa ila viongozi wenu wanakipata cha moto.
Wewe mtu mudawote, tangu kuumbwa kwa dunia, mahabusu huwa siyo pazuri na wala si kauli ya Lissu, acha uCCM wa kutoweza kufikiri
 


Acheni kutuzuga hapa mmeona siku zinakaribia na kwamba mtaumbuka kama mlivyoumbuka kwenye mambo mengi mnaanza kubadilisha maana taratibu , mlisema kwamba Septemba, Mosi mnaingia barabarani kwa kupenda au kwa kutokukpenda kwa Serikali na basi ibakie hivyo, ingawaje najua kwamba chadema hawana uwezo wa kuingia br.!
 
Halafu wenye UKUTA hawatumii nguvu nyingi kama wapinzani daaa!politics bana ni mchezo wa akili!
 

UKUTA
 
Wewe mtu mudawote, tangu kuumbwa kwa dunia, mahabusu huwa siyo pazuri na wala si kauli ya Lissu, acha uCCM wa kutoweza kufikiri
Mkuu wakipelekwa wao wanapeleka magodoro na tv.
 
Mudawote tuwe wakweli ukiamua kuingia kwenye siasa kubali yote...hebu ona kinachoendelea marekani kwasasa, siasa hazina adabu,hazina staha hazina heshima
Na hili wewe ni mmojawapo umeshawatukana sana hao uliowataja matusi makubwa tu si mara moja bali mara nyingi umewakashifu kuwabeza na kuwakejeli, ni wakubwa zako hawa watu na familia na ndugu na majukumu yao...

Kwasababu tu ya kutofautiana mitazamo ya kisiasa ukaamua kujivua utu wako ukisaidiwa na ID bandia kuwatusi hasa....na shida yako kubwa huzungumzii mfumo, hujadili hoja bali mara zote umepeleka kashfa kejeli na matusi kwa hawa watu...hii pia ni siasa lakini siasa chafu siasa majitaka
Niangalie mimi tunatofautiana mitazamo lakini sijawahi kufanya kama ufanyavyo wewe na kundi lako...

Namkosoa Magufuli lakini simvunjii heshima yake wala utu wake kwakuwa nje ya cheo chake yule ni mkubwa wangu ni kaka yangu nk...nakushauri sana jizuie dhihaka kejeli na matusi tubishane na kupingana kwa hoja tena zenye mashiko...upinzani sio uadui
 
mshana jr, mosi suala la US halinihusu sana kwani najua Trump==Tundu lissu/chadema na atashindwa vibaya mno. Pili, kwa Tz, tunachotofautiana na ninyi ni mfumo/uadilifu. Sisi tunaoamini ktk uadilifu tunawashangaa ninyi mnaosemea mfumo wakati lowasa (kama yeye) alienda akaubadili mfumo wa chadema kwa kutumia pesa na utashi wake, bado na sasa kawaambia waache uanaharakati (hiyo yote ni mifumo ya chadema).

Ina maana mtu binafisi anaweza kubadili mfumo maana kama lowasa alibadili mfumo wa chadema toka uadilifu mpaka kuwa chama cha kifisadi (maana chadema walihonga watu hela, walinunua kura, na wengine kuwaua baada ya kula zile hela pasipo kutumiza ahadi). Na ndivyo sisi tunaoamini uadilifu kuwa Dr Magufuli ataubadili mfumo wa kifisadi wa serikali/CCM na kuwa safi na kitu ambacho mpaka sasa keshaweza.

Angalia kila kona watumishi wa serikali wanajitahidi kuonesha uadilifu. Sasa tatizo wewe na wenzako mnamtukana rais, sisi tuache tu mmtukane???? Maana chadema mlifikia mpaka hatua mnawalipa hela vijana wamtukane rais (ushahidi yule kijana wa arusha mliyemchangia faini kupitia hamasa za viongozi wa chadema).
 
CDM nouma sana!😀😀😀
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…