Operation "Delete CUF" Dar es Salaam imeanza, Jengo la Wabunge wa CUF limekuwa Ofisi ndogo ya ACT-Wazalendo

Quinine

JF-Expert Member
Jul 26, 2010
21,271
47,271
pic+CUF.jpg

Zilizokuwa ofisi za wabunge wa CUF Magomeni Dar es Salaam.

Wakati wanachama wa CUF wakiendelea kumfuata Maalim Seif Sharif Hamad aliyehamia ACT-Wazalendo, ofisi za wabunge wa CUF zilizopo Magomeni jijini Dar es Salaam zimebadilishwa na kuwa ofisi za chama hicho.

Akizungumzia mabadiliko hayo, mwanachama mpya wa ACT-Wazalendo Mbarara Maharagande amesema jengo hilo sasa ni ofisi ndogo za ACT -Wazalendo na zitafanya shughuli za chama hicho.

“Ofisi hizi zilipangishwa na wabunge wanane wa CUF ambao walitimuliwa, sasa wao pia wamehamia ACT-Wazalendo na wametoa kibali kwamba zitumike kwa chama hiki,” amesema Maharagande ambaye alikuwa naibu mkurugenzi wa habari wa CUF.

Amesema ofisi nyingi za matawi ya CUF ni nyumba za watu binafsi ambao walikuwa wanachama na baadhi yao wameamua kuhamia ACT-Wazalendo na kuzifanya nyumba zao kuwa ofisi za ACT-Wazalendo.

“Hii ni operesheni inayofanyika Dar es Salaam nzima, matawi yote ya CUF yatakuwa ya ACT-Wazalendo kwa sababu wananchi wameamua kumfuata Maalim Seif katika chama cha ACT- Wazalendo,” amesema Maharagande.

Kwa mwendo huu Lipumba na msajili watabaki wamiliki wa jina tu la CUF. Hawakutegemea itakuwa hivi.
 
Haya sasa! ule usemi wa jino kwa jino, naona umetimia. Lipumba kaamua kumwaga mboga, na Maalim naye amemwaga ugali. Mwisho wa siku, CUF nayo imefuata nyendo za Nccr-Mageuzi na TLP.

Chadema ambaye ndiye "most wanted" namuona tu jinsi anavyoendelea kukwepa kila aina ya mishale iliyoelekezwa kwake. Sijui ni lini na yeye atanaswa!!
 
Wandugu,Mimi sielewi,hivi mtu kujiunga na chama Cha siasa unafuata nini
1 Utashi wako
2 Kufuuata kiongozi
3 Itikadi ya chama unachojiunga nacho
4 Au Nini kinakusukuma kujiunga na chama.
Vyama vya upinzani vina itikadi na sera nzuri sana, tatizo viongozi wake hawaishi kwenye hizo sera na itikadi zake.

Ndio maana wananchi wanaamua kufuata mtu badala ya Chama.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wandugu,Mimi sielewi,hivi mtu kujiunga na chama Cha siasa unafuata nini
1 Utashi wako
2 Kufuuata kiongozi
3 Itikadi ya chama unachojiunga nacho
4 Au Nini kinakusukuma kujiunga na chama.
Swali linamfaa Lowasa hili! Lakini kuna wale waliojiunga CCM kuunga mkono juhudi sijaona ukiweka hiyo option hapo
 
Wandugu,Mimi sielewi,hivi mtu kujiunga na chama Cha siasa unafuata nini
1 Utashi wako
2 Kufuuata kiongozi
3 Itikadi ya chama unachojiunga nacho
4 Au Nini kinakusukuma kujiunga na chama.
Itikadi ni imani mkuu........ Na imani yoyote ina mtu anayeiongoza ndio maana CCM wanamtaja Nyerere hadi kesho!
 
Wandugu,Mimi sielewi,hivi mtu kujiunga na chama Cha siasa unafuata nini
1 Utashi wako
2 Kufuuata kiongozi
3 Itikadi ya chama unachojiunga nacho
4 Au Nini kinakusukuma kujiunga na chama.
swala la chama kila mtu anabaki kuwa na uamuzi pengne mwingine anafata hata rangi za nguo ya chama fulani coz anapenda rangi, ndo maana ata katiba ipo wazi kuwa mtu anaamua mwenyew kwa utashi wake na upendeleo wake haijaweka sababu za mtu kuchagua chama.final

Sent using Jamii Forums mobile app
 
View attachment 1049805
Zilizokuwa ofisi za wabunge wa CUF Magomeni Dar es Salaam.

Wakati wanachama wa CUF wakiendelea kumfuata Maalim Seif Sharif Hamad aliyehamia ACT-Wazalendo, ofisi za wabunge wa CUF zilizopo Magomeni jijini Dar es Salaam zimebadilishwa na kuwa ofisi za chama hicho.

Akizungumzia mabadiliko hayo, mwanachama mpya wa ACT-Wazalendo Mbarara Maharagande amesema jengo hilo sasa ni ofisi ndogo za ACT -Wazalendo na zitafanya shughuli za chama hicho.

“Ofisi hizi zilipangishwa na wabunge wanane wa CUF ambao walitimuliwa, sasa wao pia wamehamia ACT-Wazalendo na wametoa kibali kwamba zitumike kwa chama hiki,” amesema Maharagande ambaye alikuwa naibu mkurugenzi wa habari wa CUF.

Amesema ofisi nyingi za matawi ya CUF ni nyumba za watu binafsi ambao walikuwa wanachama na baadhi yao wameamua kuhamia ACT-Wazalendo na kuzifanya nyumba zao kuwa ofisi za ACT-Wazalendo.

“Hii ni operesheni inayofanyika Dar es Salaam nzima, matawi yote ya CUF yatakuwa ya ACT-Wazalendo kwa sababu wananchi wameamua kumfuata Maalim Seif katika chama cha ACT- Wazalendo,” amesema Maharagande.

Kwa mwendo huu Lipumba na msajili watabaki wamiliki wa jina tu la CUF. Hawakutegemea itakuwa hivi.
delete cuf futaa kabisa,baada ya hapo infuata ccm
 
Back
Top Bottom