Oparesheni 255: CHADEMA yazuiliwa kufanya mikutano baadhi ya maeneo ya Tabora

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,741
218,332
Taarifa iliyosomwa na Makamu Mwenyekiti wa Chadema mbele ya maelfu ya wananchi huko Tabora , ambayo imetoka Jeshi la Polisi , imeeleza kwamba Chadema hairuhusiwi kufanya mikutano ya hadhara kwenye baadhi ya maeneo ya Majimbo ya Kaliua na Bulyankulu .

Moja ya kata zilizozuiliwa ni Kata ya Milambo , kwenye kijiji cha Kasuveta , kwa madai kwamba hicho ni kijiji wanachokaa Wakimbizi ambao hawahusiki na siasa za Tanzania .

Hata hivyo, Lissu amefichua kwamba kwenye kijiji hicho kuna vituo kadhaa vya kupigia kura, ambavyo vinatumika wakati wa Uchaguzi Mkuu , kura ya Mbunge na Rais hupigwa kwenye kijiji hicho , sasa kama ni cha Wakimbizi , hao wanaopiga kura za Mbunge na Rais ni akina nani ?

Lissu amefichua kwamba Vijiji hivi vinavyosingiziwa kuwa vya Wakimbizi ndio machimbo ya Wizi wa kura yanayotumika kuwasaidia Wagombea wa ccm .

Toa maoni yako
 
Naimani Hakuna Mgogoro baina ya mwenyekiti na makamu wake, isn't it?
 
Naimani Hakuna Mgogoro baina ya mwenyekiti na makamu wake, isn't it?
Kama Tundu Lissu ndio alikuwa anasoma barua iliyo andikwa na polisi na Mbowe akiwepo jukwaani wapo leo Tabora mjini huo mgogoro uchwara unatoka wapi.
Ccm wameshikwa mbupu zao wanahangaika lujinasua hali ni tete watu wanataka Katiba mpya wao wanaleta porojo za abunuasi majizi nguruwe haya.
 
Kusema ukwel hapo Ulyankulu hata usalama wake ni tia maji tia maji sana.

Sidhan kama ni hujuma.
 
Mkuu Ulyankulu sio salama kwa namna nyingi.. hilo la wakimbizi ni kubwa kuliko unavyofikir...

Lakini zaidi kufanya siasa maeneo ya wakimbizi sio sawa. .. na Lissu anajua na ndio maana anachokoza hiyo mada ili CCM kama wanafanya nao waache.
Ulyankulu hakuna Wakimbiz Kwa Sasa. Walipewa Uraia tangu 2013 na JK

Ndio maana Ulyankulu sio sawa na Kambi kama ya Nduta ambako wanaoishi huko Wana refugee status na Bado hawalimi Wala kuwa na nyumba. Ulyankulu watu wanalima, wanafuga na Wanashiriki shughuli zote za kijamii.
 
Mkuu Ulyankulu sio salama kwa namna nyingi.. hilo la wakimbizi ni kubwa kuliko unavyofikir...

Lakini zaidi kufanya siasa maeneo ya wakimbizi sio sawa. .. na Lissu anajua na ndio maana anachokoza hiyo mada ili CCM kama wanafanya nao waache.
Kura zinapigwaje eneo hilo ?
 
Taarifa iliyosomwa na Makamu Mwenyekiti wa Chadema mbele ya maelfu ya wananchi huko Tabora , ambayo imetoka Jeshi la Polisi , imeeleza kwamba Chadema hairuhusiwi kufanya mikutano ya hadhara kwenye baadhi ya maeneo ya Majimbo ya Kaliua na Bulyankulu .

Moja ya kata zilizozuiliwa ni Kata ya Milambo , kwenye kijiji cha Kasuveta , kwa madai kwamba hicho ni kijiji wanachokaa Wakimbizi ambao hawahusiki na siasa za Tanzania .

Hata hivyo, Lissu amefichua kwamba kwenye kijiji hicho kuna vituo kadhaa vya kupigia kura, ambavyo vinatumika wakati wa Uchaguzi Mkuu , kura ya Mbunge na Rais hupigwa kwenye kijiji hicho , sasa kama ni cha Wakimbizi , hao wanaopiga kura za Mbunge na Rais ni akina nani ?

Lissu amefichua kwamba Vijiji hivi vinavyosingiziwa kuwa vya Wakimbizi ndio machimbo ya Wizi wa kura yanayotumika kuwasaidia Wagombea wa ccm .

Toa maoni yako
Lissu amefichua kwamba Vijiji hivi vinavyosingiziwa kuwa vya Wakimbizi ndio machimbo ya Wizi wa kura yanayotumika kuwasaidia Wagombea wa ccm .


Sent using Jamii Forums mobile app
 
..Polisi wanatafuta sababu ya kuzuia mikutano yote ya Chadema.

..Wamepima na wameona hoja za Chadema ni mwiba kwa watawala.

..sitashangaa misafara au mikutano ya Chadema ikianza kushambuliwa na Polisi.
Ngoja tuone
 
Mkuu Ulyankulu sio salama kwa namna nyingi.. hilo la wakimbizi ni kubwa kuliko unavyofikir...

Lakini zaidi kufanya siasa maeneo ya wakimbizi sio sawa. .. na Lissu anajua na ndio maana anachokoza hiyo mada ili CCM kama wanafanya nao waache.
Kwa hiyo hakutakuwepo na vituo vya kupigia kura?

Hizo sababu ni za uwongo. Kambi ya wakimbizi haiwezi kuwa kijiji cha Tanzania kilichokuwa registered. Kambi ya wakimbizi, inaweza kuwepo kijiji fulani, wilaya fulani lakini kambi yenyewe ya wakimbizi haiwezi kuwa kijiji wala wilaya.

Wanakijiji wa kijiji hicho hawawezi kunyimwa haki yao yoyote kwa sababu tu ndani ya kijiji hicho kuna kambi ya wakimbizi. Akina Lisu na wanasiasa wengine, mahali ambako hawaruhusiwi kwenda kufanya siasa ni kwenye kambi ya wakimbizi na siyo kwenye vijiji ambavyo ndani ya maeneo yao Serikali imejenga kambi za wakimbizi.
 
Ulyankulu hakuna Wakimbiz Kwa Sasa. Walipewa Uraia tangu 2013 na JK

Ndio maana Ulyankulu sio sawa na Kambi kama ya Nduta ambako wanaoishi huko Wana refugee status na Bado hawalimi Wala kuwa na nyumba. Ulyankulu watu wanalima, wanafuga na Wanashiriki shughuli zote za kijamii.

Upo sahihi. Nimewahi kufika maeneo hayo, na kukaa siku 3.
 
Mama avumilie maumivu ya muda tu ya nyundo za kisiasa za Lissu lakini yanamjengea heshima na legacy njema mbele ya wananchi.

Nchi kwa sasa imetulia, na heshima yake iko juu ukilinganisha na kipindi kile Mbowe yuko ndani

Ajizuie na presha ya wahafidhina ya kutaka kurudi nyuma baada ya mafanikio makubwa na heshima tunayoanza kumpa kwa kurejesha demokrasia
 
..Polisi wanatafuta sababu ya kuzuia mikutano yote ya Chadema.

..Wamepima na wameona hoja za Chadema ni mwiba kwa watawala.

..sitashangaa misafara au mikutano ya Chadema ikianza kushambuliwa na Polisi.

Na inaweza kuwa ni uelewa mdogo wa OCD. Polisi wengi mambo mengi ya kisheria na logical thinking, hawana.
 
Back
Top Bottom