JF na Puppets!. Kumbe Humu Jukwaa la Siasa, Tunao "Puppets" Wengi Kuliko Tunavyojidhania!.Wanabodi,
Ukoloni mbaya kabisa kuliko hata ukoloni wenyewe, ni ukoloni wa fikra!. Ukoloni huu, ni ule wa kufikiri na kuamini kila kisemachwo na Wamarekani ndicho sahihi!.
Watanzania wenzetu ambao mnajidhania kuwa ni wazalendo wa kweli wa nchi hii, lakini mnawaaminia sana Wamarekani kila wasemacho wao ndio right, mnijue bado mnaishi kwenye ukoloni wa ki fikra na you are not better than "American Puppets"!.
Nimeyasema haya kufuatia baadhi ya wenzetu kuwaaminia sana Wamarekani na kuwa kila kinachosemwa na Wamarekani kwao ndio uthibitisho wa ukweli wao!.
Hali hii ya kuwaaminia Wamarekani kuliko hata vyombo vyetu wenyewe, iliwahi kujitokeza huko nyuma, pale Wamarekani walipodai, Rais Jakaya Kikwete, alihongwa suti na tajiri fulani, na uwongo mwingine mwingi, ikiwemo kuhongwa pesa za kampeni na kuitumia hoteli fulani jijini kwa mapumziko mafupi "short time"!.
Japo Ikulu, iliukanusha vikali uwongo huo, lakini kuna wenzetu wengi tuu ambao wanajiaminisha wao ni wazalendo zaidi wa taifa hili, bado wanaamini ukweli ni ule waliosema Wamarekani na uwongo ni lile kanusho la Ikulu!. Hawa ni puppets!.
Hivi sasa kuna mjadala mkubwa kuhusu Wanzanzibari kujitoa katika muungano, ndani ya mjadala huo, mimi nimesema mahali, "Muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar, uliridhiwa (ratified), na upande mmoja tuu wa muungano, upande wa Tanganyika, lakini kwa Zanzibar, haukuwa ridhiwa!".
Tena nikasema kuridhia (ratification), ni process na hufanywa kwa maandishi (in writings) na sio kwa kauli!.
Nikasisitiza, msingi wa muungano ni kauli za Nyerere na Karume, lakini kauli hizo, haziwezi kusimama bila maandishi!, ndipo zikaandaliwa "Articles of Union" aizombalo ndilo andishi au msahafu wa muungano!. Baada ya Articles hizo za muungano kusainiwa, sheria za "international treaties", zisisitiza, lazima ziwe "ratified" kwenye nchi husika ili zipate uhalali wa kisheria (legitimacy). Articles zile kwa Tanganyika, zilipitia "ratification process yote ili kuziridhia, na ziliridhiwa kwa maandishi na kutangazwa kwenye GN!. Kwa upande wa Zanzibar, hakuna kilichofanyika zaidi ya kauli ya Karume kuwa BLM limeridhia!. Ratification haifanyiki kwa kauli bali kwa maandishi!. Nikasisitiza, hakuna maandiko yoyote popote yanayothibitisha kuwa muungano ulikuwa ratified Zanzibar!.
Mwana jf mwenzetu leo amekuja na maandiko ya Wamarekani eti huo ndio uthibitisho muungano uliridhiwa Zanzibar!.
Kama mtu anaambiwa "ratification ni nini" na hufanyika kwa maandishi na kuelezwa kuwa hakuna any ratification process iliyofanyika Zanzibar, lakini analazimisha kwa kuwaaminia Wamarekani, jee,huu ndio ule ukoloni wa kifkra aliousema mwalimu Nyerere?.
Jee wewe mwana jf mwenzangu, jee unawaaminia zaidi Wamarekani na kila wasemacho, au angalau unauminia ukweli halisi ambao ndio ukweli wa mambo!.
"Seek the Truth, and the Truth Set You Free"!.
"Emancipate Yourself From Mental Slavery"-Bob Marley!.
Angalizo: "Great Minds" don't discuss people!, hiyo ni kazi ya "Simple Mind" hii thread, hatu discuss watu, tuna discuss idea ya wenzetu humu kuwa puppets chini ya mental slavery ya kuwaaminia sana Wamarekani!, hivyo nawaombeni sana tusianze kutaja taja majina nani ni puppet na nani sio!. Jadili tuu kama unawaamini Wamarekani kuliko tunavyojiamini wenyewe!
Natanguliza shukrani.
Pasco.
Pasco you also seem to be imprisoned by prejudgemental thinking, first know that THE LAW OR STATUTE DO NOT SIT ON THE JUDGEMENT BUT MAN, THE LAW WAS MEANT TO SAVE MAN NOT MAN TO SAVE THE LAW.Your problem is that there is no law to legitimize Muungano, you forget people agreed on this arrangement and you are no better or wise than they were despite how many books you have memorized an d given the paper identifying your qualifucatio, they very much knew what they were doing.
Always dont let any law make you a slave but arise above it and let the real truth rule you.
The Law was created because mankind changes like a shadow, and for people who willingly dont want to think and act honestly and truthfully.