Kuna jamaa mmoja ombaomba barabara ya morocco -mwenge -tegeta; huwa anashangaza sana na staili yake ya kuomba!
Haya nimaneno yake namnukuu; "Ndugu zangu mwenzenu naomba msaada, mke wangu aligongwa na gari kalazwa mhimbili tulivambiwa akakatwakatwa na mapanga, mimi hapa naumwa sana malaria, presha, U.T.I na typhoid, watoto wamefukuzwa ada shule hawajala siku tatu Leo, naombeni msaada wenu,napokea chochote mwenye mia hata mia mbili!"; mwisho Wa kunukuu!
Huyo jamaa anaomba sanasana kwenye madaladala tena huwa anapanda kwa kugombania,;
Ukitafakali juu ya huyo jamaa kama kweli ni mgonjwa basi kwa magonjwa yake alitakiwa atembee na dripu katundikwa!
anadai watoto wamefukuzwa shule kwa ada, shule gani wakati elimu ni bure?
mke wake kama aligongwa na Gari ailivamiwaje na majambazi akiwa mgonjwa?
Ni maswali yanayoumiza kichwa mwisho mtu unaweza ukaamua kumzaba kibao badala ya kutoa msaada!
Siyo huyo tu, wapo na wengine wengi tu mijini tunakutana nao,
Haiingii akilini saa 11 alfajili unamkuta ombaomba asiye na miguu au mikono kafika madaraja ya mwendokasi juu akiomba tena kwenye wheelchair, unashindwa kuelewa huyu kapaa au kafikaje pale!
ipo haja ya kukamata watu wote wanaofanya biashara hizi! hususani wanaodhamini hii biashara haram ya ombaomba!
Haya nimaneno yake namnukuu; "Ndugu zangu mwenzenu naomba msaada, mke wangu aligongwa na gari kalazwa mhimbili tulivambiwa akakatwakatwa na mapanga, mimi hapa naumwa sana malaria, presha, U.T.I na typhoid, watoto wamefukuzwa ada shule hawajala siku tatu Leo, naombeni msaada wenu,napokea chochote mwenye mia hata mia mbili!"; mwisho Wa kunukuu!
Huyo jamaa anaomba sanasana kwenye madaladala tena huwa anapanda kwa kugombania,;
Ukitafakali juu ya huyo jamaa kama kweli ni mgonjwa basi kwa magonjwa yake alitakiwa atembee na dripu katundikwa!
anadai watoto wamefukuzwa shule kwa ada, shule gani wakati elimu ni bure?
mke wake kama aligongwa na Gari ailivamiwaje na majambazi akiwa mgonjwa?
Ni maswali yanayoumiza kichwa mwisho mtu unaweza ukaamua kumzaba kibao badala ya kutoa msaada!
Siyo huyo tu, wapo na wengine wengi tu mijini tunakutana nao,
- Wapo wanaoomba nauli ukiwaambia uwape lifti huwa hawataki,
- wapo wanaoomba hela ya kula ukiwanunulia chakula wanachokita wanakimwaga! n.k
Haiingii akilini saa 11 alfajili unamkuta ombaomba asiye na miguu au mikono kafika madaraja ya mwendokasi juu akiomba tena kwenye wheelchair, unashindwa kuelewa huyu kapaa au kafikaje pale!
- kuna wale ombaomba wanaotembea wamebeba watoto mgongoni wakidai wametelekezwa na wanaume kumbe maskini hata hao watoto huwa wanakodi.
- pale kariakoo kuna jamaa huwa anavizia magari kwenye foleni, akiona dreva anachezea simu anajichomeka ili gari imguse aonekane kagongwa ili mwenye gari alipe;
- wako watu wametengeneza hadi fomu za hospitali kubwa kubwa kama mhimbili,Ccbrt na aghakan wakidai zimegoma kuwatibia n.k
ipo haja ya kukamata watu wote wanaofanya biashara hizi! hususani wanaodhamini hii biashara haram ya ombaomba!