Kurunzi
Platinum Member
- Jul 31, 2009
- 10,175
- 11,572
Ni miaka michache kidogo imepita tukiwa chuo, mwanachuo mwenzetu rafiki yetu, alipata mkasa mbaya kabisa.
Siku moja dogo mmoja alimletea pc ili amsadie kuiformat, kumbuka tuliosomea masomo ya electronics tumeishi sana kwa hizi mishe.
Kabla ya kuiformat huyu mwamba aliona kuna docoments muhimu sana kwenye hiyo pc, aliamua kuzi copy kwenye flash yake.
Siku zikawa kidogo zimepita, siku moja mwamba aliamka yupo tee mfukoni, hali tete akamua kujilipua unajua tena maisha ya chuo.
Akaona isiwe taabu, alienda cafe akapitia zile documents ilikuwa kama report ya reseach fulani hivi, kulikuwa na mawasiliano ya simu ya mwenye hiyo report, alikuwa mwanamke, alimpigia simu na kumueleza alikuwa na document zake, alimwambia wakutane ampe.
Baadaye waliendelea kuchat kwa sms ili kupanga mahali pa kukutana ili ampe document zake, mwamba alijua huyo mama atamtoa japo kidogo, lakini pia atamuuzia hiyo flash apate vijisenti vya kujikimu unajua tena maisha ya chuo.
Mipango ilifanyika ili wakutane maeneo ya Mwenge, kweli walikutana kwenye harakati za kuanza kumuonesha zile documents kwenye pc ya yule mama dah polisi hawa hapo, loh wakamwambia yupo chini ya ulinzi kuanzia sasa.
Walimchukuwa mpaka central police, alihojiwa zaidi ya masaa 4, jamaa alihojiwa kwa kesi ya mauaji, kumbe ile pc dogo aliyompelekea ili aiformat ilikuwa imeibwa kwenye ofisi moja, majambazi waliingia usiku na kuiba vitu walimpiga mlinzi wakamuumiza vibaya na baadaye alipoteza maisha.
Jamaa alitahayari sana, hakuamini anayoyasikia, mbaya zaidi hata yule dogo hamjui kwani alielekezwa na yule jamaa aliyemuelekeza alikamatwa baada ya kumhoji akasema hamjui.
Jamaa alikaa ndani miaka 2.3, tunashukuru jamaa waliohusika na lile tukio walikamatwa wakawa ndiyo pona yake na jamaa mwingine, hata hivyo aliendelea kusota ndani.
Ilibidi ifanyike mipango ya kumtoa sitaisema ila jamaa ilimbidi aende moja ya nchi ya Kusini mwa Afrika, ambako alikaa miaka 12.
Ila kwa sasa amerudi yupo nchini, anapambana na mishe zake.
Siku moja dogo mmoja alimletea pc ili amsadie kuiformat, kumbuka tuliosomea masomo ya electronics tumeishi sana kwa hizi mishe.
Kabla ya kuiformat huyu mwamba aliona kuna docoments muhimu sana kwenye hiyo pc, aliamua kuzi copy kwenye flash yake.
Siku zikawa kidogo zimepita, siku moja mwamba aliamka yupo tee mfukoni, hali tete akamua kujilipua unajua tena maisha ya chuo.
Akaona isiwe taabu, alienda cafe akapitia zile documents ilikuwa kama report ya reseach fulani hivi, kulikuwa na mawasiliano ya simu ya mwenye hiyo report, alikuwa mwanamke, alimpigia simu na kumueleza alikuwa na document zake, alimwambia wakutane ampe.
Baadaye waliendelea kuchat kwa sms ili kupanga mahali pa kukutana ili ampe document zake, mwamba alijua huyo mama atamtoa japo kidogo, lakini pia atamuuzia hiyo flash apate vijisenti vya kujikimu unajua tena maisha ya chuo.
Mipango ilifanyika ili wakutane maeneo ya Mwenge, kweli walikutana kwenye harakati za kuanza kumuonesha zile documents kwenye pc ya yule mama dah polisi hawa hapo, loh wakamwambia yupo chini ya ulinzi kuanzia sasa.
Walimchukuwa mpaka central police, alihojiwa zaidi ya masaa 4, jamaa alihojiwa kwa kesi ya mauaji, kumbe ile pc dogo aliyompelekea ili aiformat ilikuwa imeibwa kwenye ofisi moja, majambazi waliingia usiku na kuiba vitu walimpiga mlinzi wakamuumiza vibaya na baadaye alipoteza maisha.
Jamaa alitahayari sana, hakuamini anayoyasikia, mbaya zaidi hata yule dogo hamjui kwani alielekezwa na yule jamaa aliyemuelekeza alikamatwa baada ya kumhoji akasema hamjui.
Jamaa alikaa ndani miaka 2.3, tunashukuru jamaa waliohusika na lile tukio walikamatwa wakawa ndiyo pona yake na jamaa mwingine, hata hivyo aliendelea kusota ndani.
Ilibidi ifanyike mipango ya kumtoa sitaisema ila jamaa ilimbidi aende moja ya nchi ya Kusini mwa Afrika, ambako alikaa miaka 12.
Ila kwa sasa amerudi yupo nchini, anapambana na mishe zake.