Ona haya maajabu ya BVR sasa

Ona haya maajabu ya BVR sasa

Wa kusoma

JF-Expert Member
Joined
Jul 30, 2011
Posts
3,454
Reaction score
2,984
Jamani naombeeni msaada juu ya hili. Hili zoezi la kujiandikisha kupiga kura limenikuta nje ya mkoa wangu maana nilisafiri kikazi nikaja mkoani Kagera. Sasa kule kwetu zoezi linaendelea sawa na hapa Kagera.

Sasa tumeshauliwa eti tukajiandikishe popote pale hivi vitambulisho vitatuwezesha kupiga kura eneo lolote lile Tz.

Sasa baada ya kwenda kujiandikisha huku nilipo watu wananiambia eti kura yangu imeshapotea sitaweza kupiga kura nikiwa nje ya mkoa/kituo nilichojiandikishia.

Sasa nawaza hapa si ndio nishapoteza haki yangu? Maana mm sina shida na kitambuslisho vitambulisho ninavyo vingi nachotaka haki ya kupiga kura.

Halafu walichonishangaza ni kwamba unaandikwa bila kukuuliza document yoyote hii inamaanisha wahamiaji haramu ni rahisi sana kujichomeka hapa.

Ushauri katika hili wataalamu vp nitapiga kura kweli?
 
Nimejiandikishia Kagera lkn kituo changu cha kazi ni Kigoma hii ina maana ya kwamba hata siku ya uchaguzi nitakuwa Kigoma
 
Are you serious mkuu?

Mm mwenyewe nilikuwa nataka nikirudi nyumbani nipeleke hiki kitambulisho kirekebishwe lkn nimeambia hizi toolkit hazina mawasiliano.

It's only and best way...so if you are serious need to vote do it..
 
Iko ivi.
Kwa ww uliyejiandikisha mahali ambapo sio makazi yako ya kudumu utapata haki ya kupiga kura kwa Rais.
Vinginevyo hata ukija kurudia kujiandikisha uku mashine zitakutema na kusema umesha exist kwenye systerm.
Ushauri kwa mda huu maana kutakuwa na marekebisho kwenye daftari labda usubiri mda huo ili urekebishe ukiwa eneo lako
 
Iko ivi.
Kwa ww uliyejiandikisha mahali ambapo sio makazi yako ya kudumu utapata haki ya kupiga kura kwa Rais.
Vinginevyo hata ukija kurudia kujiandikisha uku mashine zitakutema na kusema umesha exist kwenye systerm.
Ushauri kwa mda huu maana kutakuwa na marekebisho kwenye daftari labda usubiri mda huo ili urekebishe ukiwa eneo lako

Sio kweli mashine hazitemi tena za hovyooo mfano uliwekwa hapa jf kuna mtu alijiandikisha mara mbili system imeshindwa kutambua
 
kwa kifupi tumeumia hili zoezi linaloendelea ni magumashi kuna kesi inaendelea wilaya ya ruangwa mtu alijiandikisha kata mbili tofauti lakini mashine haikumtambua kwakua mungu hamfichi mnafiki jamaa alikamatwa kwa kosa lingine wakati anakabidhi alichonacho aingie selo pochi ikakutwa na vitamburisho viwili,kwa stahili hii kuna uwezekano wapo waliojiandikisha mara mbili au zaidi na wakaweza kupiga kura mara mbili pia.ingawa sheria inatamka kutakua na marekebisho kabla ya uchaguzi na kwa zoezi hili maelekezo ya tume litafanyika mwezi wa nane.
 
unatakiwa kujiandikisha eneo ambalo utapiga kura,, kwahiyo kama umejiandikusha huko ndiko utakapo piga kura,, vinginevyo subiri uboreshaji wa daftari ndipo utabadili
 
Sio kweli mashine hazitemi tena za hovyooo mfano uliwekwa hapa jf kuna mtu alijiandikisha mara mbili system imeshindwa kutambua

lakini kwa mashine ile ile inakataa ..ila ukitumia mashine nyingine inakubali... lakini huruhusiwi kujiandikisha mara mbili
 
Katoe taarifa kwa mkurugenzi wako wa uchaguzi, yaani mkurugenzi wa wilaya huko kigoma. Yeye ataandika barua kwenda kwa tume aki quote namba yako ya kadi, kituo ulichojiandikishia na kituo kipya utakacho pigia kura. Halafu tume itabadilisha na utapiga kura. Usi panic
 
kwa kifupi tumeumia hili zoezi linaloendelea ni magumashi kuna kesi inaendelea wilaya ya ruangwa mtu alijiandikisha kata mbili tofauti lakini mashine haikumtambua kwakua mungu hamfichi mnafiki jamaa alikamatwa kwa kosa lingine wakati anakabidhi alichonacho aingie selo pochi ikakutwa na vitamburisho viwili,kwa stahili hii kuna uwezekano wapo waliojiandikisha mara mbili au zaidi na wakaweza kupiga kura mara mbili pia.ingawa sheria inatamka kutakua na marekebisho kabla ya uchaguzi na kwa zoezi hili maelekezo ya tume litafanyika mwezi wa nane.

Kuna threads nyingi sana hapa zinazoelezea jinsi mfumo wa BVR unavyofanya kazi.
 
Ndugu zangu nimejiandikisha na katika kujiandikisha huko nilimuuliza muandikishaji juu ya uchaguzi kunikutia mahali ambapo sijajiandikishia amenijibu hivi
Unaweza kumchagua rais popote pale utakapokuwepo Tanzania lakini Mbunge na Diwani hutaweza lazima urudi pale ulipojiandikishia ukitaka kuchagua mbunge na diwani' lakini kwa rais ni popote utakapokuwepo
 
Are you serious mkuu?

Mm mwenyewe nilikuwa nataka nikirudi nyumbani nipeleke hiki kitambulisho kirekebishwe lkn nimeambia hizi toolkit hazina mawasiliano.

Kajiandikishe kwako mkuu hawana uwezo wa kujua duplicate!
Wanadanganyika sana tu!

Ofcn tulikuwa tunabisha, dogo mmoja kajitosa, mpaka ninavyokwambia anavitambulisho viwili tayar, alichofanya ni kubadilisha vituo tu!

Kwa BVR tutachemka sana tumekurupuka
 
Nimejiandikishia Kagera lkn kituo changu cha kazi ni Kigoma hii ina maana ya kwamba hata siku ya uchaguzi nitakuwa Kigoma


Msihangaike kutakuwa na kipindi maalum cha uboreshaji daftari kabla ya uchaguzi. Utakwenda kwa msimamizi wa uchaguzi na utabadilishiwa kituo tena sasa ni rahisi kwa kuwa maelezo yote yako kwenye kadi ya kura. Tume ilikwisha kutoa Maelezo haya.
 
Iko ivi.
Kwa ww uliyejiandikisha mahali ambapo sio makazi yako ya kudumu utapata haki ya kupiga kura kwa Rais.
Vinginevyo hata ukija kurudia kujiandikisha uku mashine zitakutema na kusema umesha exist kwenye systerm.
Ushauri kwa mda huu maana kutakuwa na marekebisho kwenye daftari labda usubiri mda huo ili urekebishe ukiwa eneo lako

huu uongo wa kupiga kura ya rais mnautoa wapi?
 
Msihangaike kutakuwa na kipindi maalum cha uboreshaji daftari kabla ya uchaguzi. Utakwenda kwa msimamizi wa uchaguzi na utabadilishiwa kituo tena sasa ni rahisi kwa kuwa maelezo yote yako kwenye kadi ya kura. Tume ilikwisha kutoa Maelezo haya.

hutakiwi kuamini hili.

bado unaweza kukosa kupiga kura. amini mpaka siku ya kupiga kura kutakuwa na mapungufu kwa waliobadili taarifa.
 
Back
Top Bottom