Ona alichonifanyia huyu dada

Ona alichonifanyia huyu dada

lukatony

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2011
Posts
689
Reaction score
569
Nimekuwa na mahusiano na dada mmoja kwa miaka minne. Ni msomi tu mzuri na mrembo. Amenifanya boya sana baada ya mimi kumpenda. Tukiwa kwenye mahusiano ya kuelekea kufunga ndoa kanidhalilisha sana baada ya kuniacha.

Mahali anapofanyia kazi ni mbali na anapoishi, wakati mimi napofanyia kazi c mbali sana.Tunavyoishi kuna umbali na mikoa ni tofauti ila tumekuwa tukitembeleana kila mara. Juzi kati, kama miezi sita iliyopita nilinunua gari, basi katika mazingira ya umbali kazini kwake na daladala hazifiki basi akaniomba awe anaitumia hiyo gari.

Kwa moyo mmoja nikampa, huku mimi nikiendelea kutembea kwa miguu. Juzi tukagombana alipokuja kunitembelea kisa kukuta sms kwenye simu yake jamaa anatongoza na yeye ana muentertain vizuri tu. Kwa mtiririko wa sms ni alishakubali. Sasa baada ya kurudi anakofanyia kazi, akaniambia kuanzia sasa mimi na wewe basi, njoo uchukue gari yako.

Sasa mi bado nina hasira, sijaenda kuchukua maana naweza kumdhuru. Sasa katika muktadha huu nifanyeje? Niende, nimtume mtu au? Maana nimemuomba atulie tuyasolve kakataa.
 
Mkuu kachukue gari yako usonge mbele na maisha yandelee. kakuepusha na maswaiba mengi zaidi. Shukuru umegundua na yeye kaamua muachane. Usilazimishe huenda hana upendo tena nawe.
 
Use your senses sometimes. How comes usote kwenye madaladala huku una gari na umelihonga kwa mtu baki tu ambaye huna mkataba naye? Shule yako haijakusaidia rudi kasome tena. Hivi nikuulize, wazazi waliokuwezesha umewanunulia japo bodaboda ya kuwarahisishia shughuli zao au umeishia kuhonga tu? Laana hiyo.
 
mkuu kachukue gari yako kabla hajakuambia imeibiwa...ila atakutafuta baada ya kuichukua...usirudiane naye tena akikutafuta!
 
Learn how to control your anger and emotions...
Kama huwezi kwenda kuchukua gari yako mtume mtu akakuchukulie...
 
Mapenzi yanauma hapo ulipo fikia unaweza ukadata! we chukua tu gari yako utulie ipo siku atarudi mwenyewe! usimtumie msg wala kumpigia sim we tulia!
 
Ukute tangu mwaka uanze hujawahi kumpa mama yako zawadi au hata kumtumia ka 50, leo unahonga gari kwa mtu hata mkataba wa maisha hamna...! Pole sana!!!!!!!
 
Usimuachie usafiri huo, shaur yako.. kachukue usafir wako endelea na maisha yako achna na boya huyo, mseng* bard kabsa huyo asiejua anachohitaji ni nn kwenye maisha yake..!!
 
Mkuu achana nae kashafanya maamuzi huyo ukiendelea kubembeleza hapo yatakukuta makubwa mzee
 
anawa-entertain kivipi? kuna watu ni flirts tu by nature, labda hakuna cha zaidi. Anyway, kama hataki muongee sio issue, kachukue gari yako mwenyewe, ukituma mtu utakua udhaifu.
 
Baada ya kuchukua geri njoo Dar nikupeleke Mwenge Stand asubuhi au jioni.Utapata dem mzuri tu kuliko huyo
 
lukatony

Ili kuepusha kesi usiende na gari muachie!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom