On a serious note: kutetea umachinga ni ushujaa?

On a serious note: kutetea umachinga ni ushujaa?

masopakyindi

Platinum Member
Joined
Jul 5, 2011
Posts
18,410
Reaction score
14,119
Erosion ya thinking katika safu ya wawakilishi wa wananchi sasa inaelekea kubaya-kwa maoni yangu!

Kwa mtu anayeelewa jinsi dhana nzima ya umachinga ilivyo asingeitetea kama mkombozi wa wananchi wasio na uwezo.
Thinking ni kwamba kwa vile barabara zipo, kwa hiyo kuna wateja barabarani, mtu hakodi cha kuweka tumboni.
Cheap thinking just as it is cheap attempt at appeasing political supporters.

Hebu tuichunguze dhana nzima ya umachinga.
Hii ni outlet of goods bila ya record za aina yoyote, kwa wasomi wa siasa ni kama kutetea anarchy, a political status quo ambayo hakuna control ya aina yoyote.

Kuna ukiukwaaji mkubwa wa kodi katika dhana hii ya umachinga, kwa vile records za bidhaa zilizoingizwa nchini, na ufuatiliaji wake wa kodi huwa hakuna.

Sasa kutetea hali hii inaleta wasiwasi kwa jamii yoyote ile.
Ni vema ikajulikana kuwa kama kuna kulipa kodi basi kila mtu asilipe ili iwe survival for the fittest.
Ni wazi kwa mtindo huu taifa linajinyonga lenyewe.

Tutofautishe kati ya wamachinga na dhana ya umachinga.

Wamachinga , originally kutoka Lindi ni kundi la vijana waliokosa kazi ya kuwapa ajira ya maana.

Hivyo basi ni vema wanasiasa wetu wakajikita katika kutatua tatizo la kuwapa vijana wetu matumainio ya maendeleo kwa kukuanzisha miradi yenye tija na manufaa kwa jamii.

Kutetea vijana kukaa vibarazani mwa wahindi au barabarani kuuza njugu na viatu hadi mitumba ni kujipatia umaarufu usio na tija. Ni kama kuvuta bangi ya kisiasana kutegemea matatizo yatapotea yenyewe.
pHakuna shortcut ya kutatua matatizo ya vijan wa nchi hii, na umachinga siyo solution.
 
Wengine wanatembea na visu viwili mchana kutwa!
 
kwa sasa lazima watetewe maana angalau ni njia yao halali ya kujipatia riziki, umaachinga kwa ujumla ni zao la mfumo mbovu wa utawala hasa mfumo wa elimu na mfumo wa uchumi wa nchi, so hawa machinga ni victims tu hivo ni vema walindwe na wakti huo huo utafutwe mkakati wa muda mfupi na mrefu kuondoa tatizo hili.
 
Mkuu kwanza ninashaka na thinking yako.

Jiulize Kariakoo na maduka mengine hata wanauuza vitu vya thamani kama simu hawatoi receipt?

Je mfumo wa serikali unawatafutaje na kuwachuklia hatua?

Pili kinachofanya machinga waendelee kuwepo kwenye miji ni msongamano wa magani na foleni kiasi kwamba unaenda mjini kwa lengo la kununua bidhaa husika chukulia hapa DSM kariakoo hakuna parking. Pale unapopata parking usalama wa gari ni mdogo sana. One of the solution ni kununua vitu hivyo ukiwa kwenye foleni (wamachinga).

Suala la Kodi ni Rahisi sana polisi/mgambo/TRA kusema kwamba machinga akikutwa hana receipt (genuine) ya bidhaa anazouza zinataifishwa pamoja na kifungo. kodi zitakusanywa za kutosha kupitia huko wanachukua bidhaa

Pili serikali inaweza kuanzisha eneo maalum la wamachinga kununua bidhaa zao kwa ajili ya kwenda kuuza hii ni pamoja na kusema ni bidhaa gani zinaruhusiwa kuuzwa kwenye barabara hizo n.k. Hapa kadi zitakusanywa tu kwa urahisi.

Tatizo ni Hatujawahi kusikia wamachinga wakifukuzwa Dodoma, Tanga, Morogoro, Tabora Shinyanga nk? Je huko hakuna Machinga?

Kama wapo TAFAKARI NA CHUKUA HATUA, Usiropoke tu
 
Ahsante sana Mkuu gambagumu.

kwa sasa lazima watetewe maana angalau ni njia yao halali ya kujipatia riziki, umaachinga kwa ujumla ni zao la mfumo mbovu wa utawala hasa mfumo wa elimu na mfumo wa uchumi wa nchi, so hawa machinga ni victims tu hivo ni vema walindwe na wakti huo huo utafutwe mkakati wa muda mfupi na mrefu kuondoa tatizo hili.
 
Last edited by a moderator:
Wewe you are such a boostiful person,i dont think if you had lived that kind of life you would have spoken so carelessly like this, please do your home work before u speak unreasonably
 
Serikali ya CCM imelifuga hili tatizo, vijana hawana ajira rasmi, wanahitaji kuishi kwa kufanya shughuli zilizopo UMACHINGA ili waishi, Bunge limetega Bil 3 kwenye bajeti hii, vijana wako takribani Mil 16, inamaana ni Tshs 187 kwa kila kijana, kwa mtaji huu unategemea Machinga wasiwepo, unategemea Msigwa asiwatetee wapiga kura wake?
 
Mleta mada utakuwa KULA KULALA hujui kitu kinaitwa SHIDA wala hujawahi kupata hiyo kitu ndiyo maana huwezi hata kujiuliza Wamachinga walitokeaje sehemu za mijini chimbuko lao ni nini??
Ulishawahi kujiuliza hicho kitu?
Kwanini vijana hawalimi, hawafugi hawazslishi tena huko vijijini wanakimbilia mijini kuna nini, hujiulizi wala huwezi jiuliza ukapata jibu au ndiyo umekuja kutafuta majibu jf kwa aina hii ya mada yako??
 
MACHINGA MNG'ARISHA VYATU BARABARA YA INDEPENDENCE LEO HII NI MILIONEA MZALENDO ANAYECHANGI BAJETI YA SERIKALI YA TAIFA LETU - KAMA UNAFIKIRI UMACHINGA NI 'USHETANI' KWANZA KAMTAZAME NDG AZAM NA SAFARI YAKE ALIKOTOKA

Naam, kutetea 'Umachinga' hakika ni USHUJAA wa hali ya juu sana kwa kuwa ni chanzo muhimu ajabu wa Ujasiriamali nchini.

Mimi ni mmoja kati ya watu ninayejitokeza kuhesabiwa hapa kuwa ni mtetezi wa Wamachinga tena bila aibu isipokua katu siungi mkono hata tone ama kitu gani au mfumo uliowafikisha katika kujichagulia maisha ya umachinga kama njia ya kujikinga na umasikini unaotudhalilisha mno kimaisha kila kona ya nchi hii.

Ni kutokana na msimamo huu ndio maana napinga mtu yeyote kuchota gesi kusini BILA YA KUIONGEZEA KWANZA THAMANI pale pale penye chanzo cha mavuno ili wakazi wa maeneo husika wapate faida ya moja kwa moja ya (1) ajira, (2) kuuza bidhaa zao, pamoja na (3) serikali zao za wilaya kujipatia kodi kwa ajili ya maendeleo.

Kati ya yote mema mengine ni pamoja na; (4) kupata fursa pekee kuchota teknolojia toka kwa wawekezaji, (5) kampuni husika kuwekeza pia kuendeleza katika miradi jamii kama vile shule bora, hospitali na kisha CHANGAMOTO LA UMACHINGA ama kukauka au kupata mguso ulio bora zaidi.

Ukweli huu unapata nguvu kutokana na ushahidi hai miongoni mwetu kwa picha Milionea Azam ambaye alianza tu kama Machinga na kisha kujifungulia kijiwe cha kung'arishia watu vyatu vyao pale Barabara ya Independence na leo hii ni mtoa msaada wa ndani ya nchi kwa serikali yetu.
 
Kuna Rais mmoja alisema "vijana wetu wamachinga jinsi walivyojazana hata ukipita barabarani mzazi wao wanaweza kukutia kidole.."

watu wakaanza kuguna.

Rais akaacha gap halafu akamalizia sentensi yake "... cha machoni"

Je, unakumbuka huyo alikuwa Rais gani? na je, unakumbuka aliwahimiza watu wa Bukoba wafanye nini?
 
Wengine wanatembea na visu viwili mchana kutwa!

Ndo ujue ni kiasi gani cha umasikini serikali ya ccm imewafikisha. Si kitu cha serikali kujivunia. Kwa hiyo kuwa na visu viwili si kama amependa, nao walipenda wawe na maghorofa kama Rizi-one, walipenda wawe na vituo vya mafuta kama Lake oil na kununua hisa Tanzanite One, ila serikali ya ccm ndiyo iliyowanyima uwezo.
 
Mkuu kwanza ninashaka na thinking yako.

Jiulize Kariakoo na maduka mengine hata wanauuza vitu vya thamani kama simu hawatoi receipt?

Je mfumo wa serikali unawatafutaje na kuwachuklia hatua?

Pili kinachofanya machinga waendelee kuwepo kwenye miji ni msongamano wa magani na foleni kiasi kwamba unaenda mjini kwa lengo la kununua bidhaa husika chukulia hapa DSM kariakoo hakuna parking. Pale unapopata parking usalama wa gari ni mdogo sana. One of the solution ni kununua vitu hivyo ukiwa kwenye foleni (wamachinga).

Suala la Kodi ni Rahisi sana polisi/mgambo/TRA kusema kwamba machinga akikutwa hana receipt (genuine) ya bidhaa anazouza zinataifishwa pamoja na kifungo. kodi zitakusanywa za kutosha kupitia huko wanachukua bidhaa

Pili serikali inaweza kuanzisha eneo maalum la wamachinga kununua bidhaa zao kwa ajili ya kwenda kuuza hii ni pamoja na kusema ni bidhaa gani zinaruhusiwa kuuzwa kwenye barabara hizo n.k. Hapa kadi zitakusanywa tu kwa urahisi.

Tatizo ni Hatujawahi kusikia wamachinga wakifukuzwa Dodoma, Tanga, Morogoro, Tabora Shinyanga nk? Je huko hakuna Machinga?

Kama wapo TAFAKARI NA CHUKUA HATUA, Usiropoke tu
Mkuu ielewe mada yenyewe, dhana ya umachinga na madhara yake.
Kutete mfumo huu usio na tija ni vile vile kutetea kutolipa kodi kwa wananchi wote.
Sioni mantiki ya mwakikishi wa wananchi kulalama kuwa fulani halipi kodi wakati anatetea kundi fulani la wasiolipa kodi.
Umasikini si kigezo, nchi yoyote iliyositawi kimaendeleo kulipa kodi sio option, bali suala ni kodi kiasi gani na mfumo mzima wa biashara.
 
Serikali ya CCM imelifuga hili tatizo, vijana hawana ajira rasmi, wanahitaji kuishi kwa kufanya shughuli zilizopo UMACHINGA ili waishi, Bunge limetega Bil 3 kwenye bajeti hii, vijana wako takribani Mil 16, inamaana ni Tshs 187 kwa kila kijana, kwa mtaji huu unategemea Machinga wasiwepo, unategemea Msigwa asiwatetee wapiga kura wake?

Ni kweli kabisa serikali iliyo madarakani na serikali zilizipita za CCM zilifumbia mcho tatizo hili.
Vijana hawa machinga wanatumika kama mtaji wa kisiasa na si vinginevyo.
Kwa vile dhana yenyewe ya machinga si endelevu, hata kuwajengea Machinga Complex haikufaa kitu.

Machinga Complex ni kama kutatua ugonjwa ambao hujui chanzo chake, na tumjionea machinga wakilikwepa jengo hilo kwa ajili ya kukwepa kulipa kodi na vile vile kupunguza gharama zao za uendeshaji.
Tatizo la ajira na kujiajiri mikoani ambako ndio chimbuko la vijana Machinga, ndio suluhisho la tatizo hili.
Kinachokera na kuhuzunisha ni watu hata wasomi kushabikia mfumo huu ambao si endelevu na kwa vyovyote una centre kwenye kuwanyonya vijana hawa kwa ajili ya mlo wa siku moja.
 
No one has ever staged a successful 'war' against Umachinga to any level of fruitation. Instead, umachinga is a blessing in diguise that most seriously call for a cool-mind strategic thinking into tapping in the cream for even better Billionaire Azams of tomorrow for the good of our currently feable performing economy.

Mkuu ielewe mada yenyewe, dhana ya umachinga na madhara yake.
Kutete mfumo huu usio na tija ni vile vile kutetea kutolipa kodi kwa wananchi wote.
Sioni mantiki ya mwakikishi wa wananchi kulalama kuwa fulani halipi kodi wakati anatetea kundi fulani la wasiolipa kodi.
Umasikini si kigezo, nchi yoyote iliyositawi kimaendeleo kulipa kodi sio option, bali suala ni kodi kiasi gani na mfumo mzima wa biashara.
 
UFAHARI NA MAJIVUNO YA WASOMI WETU SASA UTOE MAJIBU JINSI GANI TUTAKAVYOWEZA KUGEUZA 'BIASHARA ZA VISU VIWILI' KUWA CHANZO CHA AJIRA YA WATANZANIA WENZETU ZAIDI YA LAKI MBILI KWA MAFANIKIO

Kamwe usiishie katika kutazama VISU VIWILI alivyovibeba MPIGANAJI WETU MACHINGA aliyejichagulia kukataa kata kata kusalimu amri kwa makali ya umasikini nchini (kugeuka Matonya) bali zaidi, kama kweli wewe ni msomi wala usiingize dharau katika kazi hizi zinazotulea sehemu kubwa taifa hili, yafaa ukune zaidi kichwa jinsi gani utakavyoweza kufanya faida za usomi wako kumfikia mtu huyu mwenye maisha ya hali ya chini mno lakini MWENYE UTAYARI WA KUJITUMA ili akapate sasa:

(a) UJUZI wa kutengeneza kabisa visu bora yeye mwenyewe,

(b) eneo murua wa kufanyia shughuli hii,

(c) mtaji wa kusaidia kusukuma shughuli zake mpya hizi,

(d) Kumpa uwezo wa ki-akili wa kuweza kusimamia mtaji, mtandao wake wa kibiashara, na rasilimali watu atakaosaidiana nao,

(e) Kubadilisha akili
'viongozi na wasomi wa kwenye viyoyozi wenye majivuno matupu na kiingereza kingi' wa aina yako wewe ili wapate kuona 'Mema' na wala si 'Ushetani' tu wa Wamachinga.

(f) Kuboresha mazingira ya sera ili kupatikana uwanja chongofu na wasimamizi wenye uchungu na utayari wa kufanya bishara za visu viwili kugeuka kuwa viwanda vya visu vyenye uwezo wa kuwapa ajira vijana wenzetu zaidi ya 200,000

Wengine wanatembea na visu viwili mchana kutwa!
 
Kwa hapa tulipofika umachinga ni 'industry' ya aina yake. Kama ilivyo kwa bodaboda, tukubali tu na kuwawekea mfumo ambao utawasaidia kuwatoa na pia kuleta nidhamu katika utendaji wa shughuli zao. By the way dunia nzima kuna wamachinga kwa maana ya uchuuzi wa mitaani.
 
Masopakyindi bhana ! Nimeamini wewe si Mtu wa aina ya Watz aisee, kwa hiyo tuwatose wamachinga kisa hawako kwenye Mfumo Rasmi ? Kweli nimeamini Aliyeshiba Hamjui mwenye njaa ! Hivi andiko lako lina Msukumo wa kisiasa ( kwa sababu Msigwa yumo ) ? Au lina msukumo wa kijamii au ni shibe tu uliyonayo ndiyo imekusukuma kuandika hivi ?
 
Masopakyindi bhana ! Nimeamini wewe si Mtu wa aina ya Watz aisee, kwa hiyo tuwatose wamachinga kisa hawako kwenye Mfumo Rasmi ? Kweli nimeamini Aliyeshiba Hamjui mwenye njaa ! Hivi andiko lako lina Msukumo wa kisiasa ( kwa sababu Msigwa yumo ) ? Au lina msukumo wa kijamii au ni shibe tu uliyonayo ndiyo imekusukuma kuandika hivi ?
Mkuu reality na philosophers wanatuambia kuwa you can not control history, but you can learn from it!

But you can learn from history and control your future!!
Tukikataa kujifunza from history we are doomed.

Mimi na wewe ingalau tuna ka mbegu ka kujua kuwa makosa yaliyofanyika nyuma ni lazima yasahihishwe!
Suala la Machinga linabebwa na wanasiasa wengi wamaopenda kupata umaarufu wa reja reja.
Na umaarufu huo si kwa chama kimoja,bali wote CCM na hata CDM, Na huko nyuma NCCR.
Msomi na thinker lazima afikiri from abstract, je , ukishapata umaarufu wa kushangiliwa na machinga ndio umetatua matatizo yao?
Far from it!

Na bahati mbaya machinga siyo kwamba hawana akili, wakisha gundua kwamba umewatapeli kisiasa , suala linakuwa baya zaidi.
 
Mkuu, swala hapa siyo kutetea umachinga. Laiti mfumo wetu wa elimu na mfumo wa uchumi isingekuwa inazalisha wamachinga, basi tatizo la wamachinga lisingekuwepo. Wamachinga wapo kwa sababu umachinga umeletwa na mifumo yetu ya elimu na uchumi. Na kwa kuwa wamachnga ni tokeo la kushindwa kufanya kazi kwa mifumo hiyo miwili, ni lazima jamii iwakubali kwamba ni wenzetu ndani ya hiyo jamii. Wana haki ya kuthaminiwa utu wao, kutetewa na kulindwa.
 
Back
Top Bottom