Ni wazo zuri na kila mtu baada ya kupiga kura ahakikishe kuwa anaweka mkakati wa kupata chakula chake na kukaa katika kituo cha kupigia kura. Ni lazima mwende na tochi kwani hawa jamaa watazima umeme ili kufanya uchakachuaji wao. Mtu asitii amri ya kuondoka karibu na kituo na vilevile ni lazima kupeleleza nyumba au maeneo ambayo watakuwa wameficha kura bandia. Mawakala wasikubali kula au kuchangia chakula na wasimamizi au mawakala wengine kwani kitakuwa kimewekewa dawa za kulevya au kimeharibiwa ili waendeshe kama gari bovu.