Ombi langu kwa Viongozi wa CHADEMA

Ombi langu kwa Viongozi wa CHADEMA

Kamanda Francis

JF-Expert Member
Joined
Nov 30, 2013
Posts
834
Reaction score
140
Viongozi wa Chama Changu awali ya yote napenda Kusema Poleni Kwa Majukumu ya Kupambana Kwa niaba yetu Wanyonge wa Taifa hili. Kwa Majina naitwa "Francis Boniface" (24yrs) ni Mkazi wa Kijiji cha Nyansurura hapa Serengeti Mara, pia Mimi ni Katibu Mwenezi wa Chama changu (CHADEMA) ndani ya Kata yetu ya Nyansurura Inayoongozwa na Chadema.

Kabla Sijaeleza Ombi langu, Kwanza natoa Pongezi za Dhati Kwa Viongozi wangu wa Chama Ngazi ya Taifa Kwa Upendo, Hekima, Busara, Umoja na Mshikamano wao Katika Kuijenga na Kuieneza Taasisi hii Iliyobeba Matumaini ya Wanyonge wa Taifa hili. Lakini Kubwa zaidi natoa Pongezi Kwa Mhe.Mbowe Kwa Jinsi anavyoepukana na Wabaya wake Wanaomchoma Mikuki ya Maumivu Ili Kumkatisha tamaa.

OMBI:Viongozi wangu wa Chama, nawaomba sana, Kwanza:Mhe.Mbowe aendelee Kuwa Mwenyekiti Uchaguzi ujao. Pili:Hakikisheni Mnajikita zaidi Kupambana na Maswala ya Kitaifa, huku Mkizipa Kisogo Propaganda za akina "Mwigulu" ambao Wanasumbuliwa na tatizo la Presha ya Kumwona Mhe.Mbowe akiwa Mhimili wa Chama.
 
Naomba Kuwasilisha Makamanda..."TULIANZA NA MUNGU, HAKIKA TUTAMALIZA NA MUNGU" Nayakumbuka Maneno ya Mhe.Mbowe:"Nikianguka Kwa Kupigwa Risasi, Msinililie, Endelezeni Mapambano Kudai haki za Wanyonge Wenzetu" naye Mhe.Lema akiwa Namanga Dar Es Salaam:"CCM na Serikali yao Wanavunga Wahuni, Dawa ni Kuwa Muhuni zaidi yao". KILA LA KHERI MPAKA KIELEWEKE.
 
Tupo nyuma yako jemadari wetu mkuu katika vita hii kuu ya kumng'oa Nduli CCM. Usikubali wakutoe kwenye lengo cz wanaona dili lao na Zitto imekula kwao sasa ndo wamehamia kwako kwa mbinu za kukuchafua mbele ya jamii. Usiwe na wasiwasi ilimradi tu muendelee kushikamana na Dr Slaa na kamati kuu. Sisi na mwendo wa CHADEMA NI MSINGI mpaka kieleweke.
 
CHADEMA ni kama chaka la wabwia unga. Akiingia mgeni lazima wamtilie mashaka
 
Viongozi wa Chama Changu awali ya yote napenda Kusema Poleni Kwa Majukumu ya Kupambana Kwa niaba yetu Wanyonge wa Taifa hili. Kwa Majina naitwa "Francis Boniface" (24yrs) ni Mkazi wa Kijiji cha Nyansurura hapa Serengeti Mara, pia Mimi ni Katibu Mwenezi wa Chama changu (CHADEMA) ndani ya Kata yetu ya Nyansurura Inayoongozwa na Chadema.

Kabla Sijaeleza Ombi langu, Kwanza natoa Pongezi za Dhati Kwa Viongozi wangu wa Chama Ngazi ya Taifa Kwa Upendo, Hekima, Busara, Umoja na Mshikamano wao Katika Kuijenga na Kuieneza Taasisi hii Iliyobeba Matumaini ya Wanyonge wa Taifa hili. Lakini Kubwa zaidi natoa Pongezi Kwa Mhe.Mbowe Kwa Jinsi anavyoepukana na Wabaya wake Wanaomchoma Mikuki ya Maumivu Ili Kumkatisha tamaa.

OMBI:Viongozi wangu wa Chama, nawaomba sana, Kwanza:Mhe.Mbowe aendelee Kuwa Mwenyekiti Uchaguzi ujao. Pili:Hakikisheni Mnajikita zaidi Kupambana na Maswala ya Kitaifa, huku Mkizipa Kisogo Propaganda za akina "Mwigulu" ambao Wanasumbuliwa na tatizo la Presha ya Kumwona Mhe.Mbowe akiwa Mhimili wa Chama.
Ni aibu kwa chama kumtegemea mtu mmoja tu wakati wapo wengi wenye sifa. Ruhusuni siasa za ushindani
 
Naomba Kuwasilisha Makamanda..."TULIANZA NA MUNGU, HAKIKA TUTAMALIZA NA MUNGU" Nayakumbuka Maneno ya Mhe.Mbowe:"Nikianguka Kwa Kupigwa Risasi, Msinililie, Endelezeni Mapambano Kudai haki za Wanyonge Wenzetu" naye Mhe.Lema akiwa Namanga Dar Es Salaam:"CCM na Serikali yao Wanavunga Wahuni, Dawa ni Kuwa Muhuni zaidi yao". KILA LA KHERI MPAKA KIELEWEKE.
Naona umenukuu maneno ya wa wachagga tu
 
Haya maneno ya maana sana kamanda, Mbowe ni Mwamba usiotikisika....
 
Mungu akulinde sana kamanda wetu mkuu Mbowe. Tunakuhitaji sana kwenye chama mpaka 2015 na kuendelea. CHADEMA NI MSINGI ndio kazi yetu kamanda. Ni mwendo wa nyumba kwa nyumba katika kuandikisha wanachama wapya kwa chama.
 
Ninachowaomba viongozi wa chadema ni pamoja na kuanzisha m4c ya nguvu toka kusini mpaka kaskazini, magharibi mpaka mashariki. Pia anzisheni media zenu za chama!
 
Usipate shida kamanda, mawazo yako ni sawa na ya tulio wengi, Mbowe anastahili kuendelea kuongoza jahazi kwa sasa chini ya Dr Slaa, hakuna mwanachadema anayempinga Mbowe kwa jinsi anavyochapa kazi ya kukijenga chama, wanaopinga ni propanganda kutoka ccm, wameona nimwiba kwao, wasivyo na akili eti, waliwekeza kwa kitoto kidogo kama Zitto kiue Chadema, ndio maana tumekipiga chini, mbowe atapumnzika uongozi lakini sio sasa, bado anahitajika, uenyekiti hatupeani kama bagia, tunapima uwezo wa mtu.
 
Peoples............. Mpaka kieleweke. Chadema inapaa ccm chali kama mende kazima network zake.tanzania bila ccm tutaishi kwa amani na upendo
 
Naomba Kuwasilisha Makamanda..."TULIANZA NA MUNGU, HAKIKA TUTAMALIZA NA MUNGU" "Nikianguka Kwa Kupigwa Risasi, Msinililie, Endelezeni Mapambano Kudai haki za Wanyonge Wenzetu"


1)unavitalu vingapi vya bangi?
 
ACHENI UNAFIKI CHAMA cha kijani yanawahusu nini ya CHADEMA. WAJInga msiotumia akili zenu mnaendeshwa tu kama misukule
 
Mimi kama mzee wenu niliye mshauri zi.tto z .ka.bwe awe na tabia njema ya kutokukisaliti chama makini cha chadema akakataa kutokana na tamaa ya fedha!.

"nasema hivi nina imani kubwa na katibu mkuu na m/kiti wa chadema taifa mdogo wangu freemani mbowe hadi mungu ananishangaa!

"hizi ndizo silaha kali kwa mafisadi wa c.c.yem,kila siku wanaomba mbowe na slaa wafe bila kujua maombi yao ni ya kishetani na chadema ni mpango wa mungu"


vijana wangu wa bavicha mpooo, nikisema peoplessss kwa pamoja tunitikia .......
 
Kuanzia sasa freemani mbowe na dk. Slaa nawavika nishani bora ya uongozi uliotukuka.

Mbowe na slaa nawapa heshima ya uchifu wa wagogo wote tanganyika.
 

Attachments

  • PINDA VS J.K.jpg
    PINDA VS J.K.jpg
    74.6 KB · Views: 98
Nilizaliwa kichadema,ninaishi kichadema, na nikifa nizikeni kichadema.
 
hebu tujuane kwanza, wewe mleta mada ni chadema chumbani au sebuleni. Mimi ni chadema sebulen
 
Back
Top Bottom