Ombi: HESLB ongezeni muda wa kuomba mkopo

jiwe angavu

JF-Expert Member
Aug 28, 2015
19,058
35,838
Habari za asubuhi wakuu.

Naomba niende moja kwa moja kwenye dukuduku langu.

Katika kufuatilia na kufanya michakato mbalimbali katika uombaji wa mkopo nimekumbana na changamoto nyingi ambazo naamini wengi wetu waliofanya huu mchakato wamekutana nazo.

Kupitia mfumo mpya wa uombaji mkopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu kwa njia ya mtandao (OLAMS), kuna changamoto nyingi zilizojitokeza katika kufanikisha mchakato huu kwa urahisi na kwa wakati, baadhi ya changamoto ambazo naamini wengi wetu wamekumbana nazo na wanaendelea kukumbana nazo ni kama zifuatazo.

  • Mtandao kuwa chini(networks Problems), hii ni changamoto kubwa sana, kuna kipindi cha siku mbili ama tatu mtandao wa website ya bodi na ule wa OLAMS haukupatikana kabisa.
  • Ucheleweshwaji wa kupewa control number kwa jili ya malipo, hii kuna baadhi ya watu imewachukua zaidi ya wiki 2 hadi tatu tangu wafanye ombi la kuomba control number.
  • Kushindwa kuprint au ku-apload forms kwa ajili ya kuzifanyia kazi au kuzituima kwenye mfumo.
  • Kushindwa kufanya marekebisho endapo kwa namna moja ama nyingine mwombaji kakosea kujaza taarifa zake kwa usahihi.
Hizi ni baadhi kati ya changamoto nyingi waomba wa mkopo kwa ajili ya kusoma elimu ya juu 2017/2017 wanazo kumbana nazo.

Hivyo kupelekea wengi kushindwa kutuma maombi yao kwa wakati, sidhani kama ni lengo la serikali kuwasumbua na kuwahangaisha hangaisha wananchi wake hasa vijana wanaohitaji kujipatia elimu ya juu ili waweze kutimiza malengo yao kielimu.

hivyo kama nilengo la serikali kupitia bodi ya mikopo kuwawezesha viijana wa kitanzania kufikia malengo yao ya kusoma elimu ya juu,ni vyema suala la kuongezewa muda wa kuomba mkopo ungeongezwa ili kuwawezesha wengi kukamilisha huu mchakato kwa wakati kutokana na usumbufu mwingi uliojitokeza kupitia mfumo mpya wa OLAMS.

nawatakieni utekelezaji mwema wa majukumu yenu.

waziri wa elimu
Katibu mkuu wizara ya elimu
Mkurugenzi bodi ya mikopo
 
Kuna uzi nilichangia na kutahadharisha kuwa kama muda haukuongezwa tunaweza kuwa na majanga mwaka huu. Mifumo yote ya HESLB na RITA imechukua muda kutengamaa na kueleweka. Tulichukua si chini ya siku 10 kutatua tatizo la malipo kuambiwa hatuja lipa. Unatoka kijijini, malipo yanakataa, yakiwa sawa baada ya siku kadha, RITA wanakuelekeza uende Dar unafunga safari wanakuambia uhakiki wa cheti baada ya wiki ukachukue, unarudi kijijini ukapate signature za mzazi na kijiji, unawahi tena Dar kusubiri RITA. Tarehe 1.9.2017 sikukuu, u-scan na kuprint halafu utume board na viambatanisho hata kama uli vi-upload. Changanya na maelekezo magumu na yasiyo kamili. Na bodi wanasema 4.9.2017 ndio siku ya mwisho kupokea, sasa kama uko mbali na Dar inaweza kuwa kasheshe. Wangesema post-date ya mwisho iwe 04.09.2017 ingekuwa haki sawa. Tuombe wawe wasikivu. Kitu kingine gharama la zoezi mwaka huu limekuwa kubwa zaidi ukilinganisha na miaka iliyopita hasa kwa wale wa vijijini.
 
Itabidi waongeze tu hakuna namna vinginevyo hawaeleweka kabisa na itaonekana kuwa makusudi , wanafunzi walioko JKT ni wengi sana walipewa wiki moja kuja kuomba vyuo na kuomba mikopo cha ajabu muda wote huo systems za bodi ya mikopo zilikuwa hazifanyi kazi kabisa, ikabidi warudi JKT kwenda kumalizia mafunzo , halafu tena likaja swala la kwenda kuhakiki vyeti vya Kuzaliwa RITA wao wakiwa tayari wamesha rudi mafunzoni Kwa mujibu! Kwa hiyo swala la ku extend muda wa maombi ya mikopo ni la lazima Kama wanataka tuone kuwa wamewatendea Watu wote haki ya kuomba Kwa kuanzia kisha kupata mkopo! Mara system down Mara uhakiki wa vyeti huko Rita kenyewe balaaa
 
Itabidi waongeze tu hakuna namna vinginevyo hawaeleweka kabisa na itaonekana kuwa makusudi , wanafunzi walioko JKT ni wengi sana walipewa wiki moja kuja kuomba vyuo na kuomba mikopo cha ajabu muda wote huo systems za bodi ya mikopo zilikuwa hazifanyi kazi kabisa, ikabidi warudi JKT kwenda kumalizia mafunzo , halafu tena likaja swala la kwenda kuhakiki vyeti vya Kuzaliwa RITA wao wakiwa tayari wamesha rudi mafunzoni Kwa mujibu! Kwa hiyo swala la ku extend muda wa maombi ya mikopo ni la lazima Kama wanataka tuone kuwa wamewatendea Watu wote haki ya kuomba Kwa kuanzia kisha kupata mkopo! Mara system down Mara uhakiki wa vyeti huko Rita kenyewe balaaa
Wakiongeza muda nitaacha kuita serikali dhalimu.
 
Back
Top Bottom