Aliyekuwa mgombea ubunge wa viti maalumu kupitia Umoja wa Wazazi wa CCM, Olivia Chagula, amewataka Watanzania kujitokeza kwa wingi Oktoba 29 kushiriki uchaguzi mkuu kwa kupiga kura bila hofu akisisitiza kuwa usalama umehakikishwa kama alivyoeleza Amiri Jeshi Mkuu, Rais Samia Suluhu Hassan, katika mkutano wa kampeni uliofanyika jana Oktoba 21, katika viwanja vya Leaders Club, jijini Dar es Salaam
Chagula amesema, “Kama Dkt. Samia alivyosema, yeye ndiye Rais wa nchi (na Amiri Jeshi Mkuu), hivyo wananchi na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi wajitokeze kwa wingi Oktoba 29, kwani usalama upo wa kutosha.”
Aidha, amesifu jitihada mbalimbali zinazotekelezwa na Dkt. Samia kupitia Ilani ya CCM, na amewataka Watanzania wenye nia ya kuandamana wasithubutu kufanya hivyo, kwani muda huu ni wa amani na maendeleo, si wa kushaabikia machafuko
Akizungumza Pktoba 21, 2025 na wakazi Dar es Salaam, Rais Samia ambaye pia ni Mgombea urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), aliwataka Watanzania kujitokeza kwa wingi kupiga kura Oktoba 29 huku akieleza kuwa vyombo vya usalama nchini vimejipanga kuhakikisha zoezi hilo linafanyika kwa amani na utulivu
Alisisitiza kuwa maandamano yatakayokuwepo ni ya watu kupiga kura pekee na si mengineyo
Chanzo: TBC DIGITAL
Chagula amesema, “Kama Dkt. Samia alivyosema, yeye ndiye Rais wa nchi (na Amiri Jeshi Mkuu), hivyo wananchi na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi wajitokeze kwa wingi Oktoba 29, kwani usalama upo wa kutosha.”
Aidha, amesifu jitihada mbalimbali zinazotekelezwa na Dkt. Samia kupitia Ilani ya CCM, na amewataka Watanzania wenye nia ya kuandamana wasithubutu kufanya hivyo, kwani muda huu ni wa amani na maendeleo, si wa kushaabikia machafuko
Akizungumza Pktoba 21, 2025 na wakazi Dar es Salaam, Rais Samia ambaye pia ni Mgombea urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), aliwataka Watanzania kujitokeza kwa wingi kupiga kura Oktoba 29 huku akieleza kuwa vyombo vya usalama nchini vimejipanga kuhakikisha zoezi hilo linafanyika kwa amani na utulivu
Alisisitiza kuwa maandamano yatakayokuwepo ni ya watu kupiga kura pekee na si mengineyo
Chanzo: TBC DIGITAL