Elias Msuya
Senior Member
- Dec 23, 2011
- 173
- 671
Wakati vikao vya ndani vya wilaya na mikoa vya CCM vinavyochuja wagombea vikiisha mkoani Arusha, taarifa zinadai kuwa aliyekuwa Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka na aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini, Mrisho Gambo wamefyekwa.
Vikao hivyo vilivyoendeshwa kwa usiri mkubwa vimetaja watia wengine waliofyekwa ni pamoja na Noah Lembris (Arumeru Magharibi), John Pallangyo (Arumeru Mashariki), Pauline Gekul (Babati) na Flatey Massey (Mbulu Vijijini).
Kujua nini kinajiri Arusha kwenye Uchaguzi Mkuu soma: Arusha: Matukio Yanayojiri Kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Taarifa zinadai kuwa waliopitishwa katika tatu bora ni pamoja aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Magu, Joshua Nassari, ambaye aliwahi kuwa Mbunge wa Arumeru Magharibi kupitia CHADEMA.
Kwa upande wa Simanjiro, majina yanayotajwa ni panoja na la Jmaes Ole Millya ambaye ni Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA) na wengine wawili.
Taarifa kamili za majina kupitishwa zitatolewa baada ya Kamati Kuu ya CCM kuketi.
Vikao hivyo vilivyoendeshwa kwa usiri mkubwa vimetaja watia wengine waliofyekwa ni pamoja na Noah Lembris (Arumeru Magharibi), John Pallangyo (Arumeru Mashariki), Pauline Gekul (Babati) na Flatey Massey (Mbulu Vijijini).
Kujua nini kinajiri Arusha kwenye Uchaguzi Mkuu soma: Arusha: Matukio Yanayojiri Kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Taarifa zinadai kuwa waliopitishwa katika tatu bora ni pamoja aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Magu, Joshua Nassari, ambaye aliwahi kuwa Mbunge wa Arumeru Magharibi kupitia CHADEMA.
Kwa upande wa Simanjiro, majina yanayotajwa ni panoja na la Jmaes Ole Millya ambaye ni Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA) na wengine wawili.
Taarifa kamili za majina kupitishwa zitatolewa baada ya Kamati Kuu ya CCM kuketi.