Mzizi wa Mbuyu
JF-Expert Member
- May 15, 2009
- 7,467
- 7,257
Bunge la Mchana siku ya Jumamosi wakati akihitimisha Hotuba ya Wizara ya Nishati na Madini mh Prof Muhongo alimuita Sendeka kuwa ni muongo kwa kutaka kumlisha Mh Rais Maneno ambayo hakuyasema. Hii ni baada ya Mh Sendeka wakati akichangia hotuba hiyo alisema kua Rais hajatimiza Ahadi aliyowahi kutoa kuwa baada ya kuisha kwa Mkataba wa kampuni ya Tanzaniteone serikali itatwaa Mgodi huo na kumilikisha Wachimbaji wadogo wadogo.
Migodi hiyo ipo Mererani wilayani Simanjiro mkoaniManyara.
Akimjibu Sendeka Mh Waziri alisema kua siku moja aliwahi kumuuliza swala hilo na yeye waziri alienda kwa Mh Rais na kumuuliza lakini Mh rais alisema kua hayo maneno hakuwahi kuzungumza isipo kua Sendeka anamsingizia.
Mh waziri alionya wale wote wenye tabia ya kuzungumza vitu vya uongo na kumlisha Rais maneno ambayo hakusema.
Mh Waziri Muhongo Wakati akikamilisha kujibu hoja za Wabunge ndipo Mh Sendeka akaomba Muongozo lakini Spika alimkatalia.
Je Spika kumnyima Sendeka nafasi ya kuwasilisha Muongozo ni Demokrasia au anabalance mambo ili na wabunge wa Upinzani wakiomba muongozo awanyime kama tulivyoona?
Sendeka ni mnafiki sssana, kama Sitta tu na Kilango....walijifanya wapapmbanaji wa ufisadi wakawapaka matope kina kina Lowassa..then anajidai kujirudi ...wenzie bado wanakinyongo sana nae!!!
Wamemkomesha!!