OFISI YA UTUMISHI MISUNGWI IMULIKWE

OFISI YA UTUMISHI MISUNGWI IMULIKWE

daianosus

Senior Member
Joined
Dec 9, 2018
Posts
193
Reaction score
303
Katika ofisi ya utumishi halmashauri ya wilaya ya misungwi kumekuwa na uzembe na kutojali kwa kiwango cha juu kwa baadhi ya watumishi. Nitatolea mfano eneo moja tu kwa leo, nalo ni kuhusu upandishaji wa madaraja kwa watumishi katika halmashauri hii.
Mnamo tarehe 1/4/2018 watumishi wenye sifa walipandishwa vyeo na bodi ya ajira ya halmashauri hiyo. Lakini mpaka leo tunamalizia mwaka [miezi 8] hakuna mabadiliko yoyote katika mshahara wa watumishi hawa.
Wanapofatilia sababu zinazotolewa ni kuwa hakuna mtandao au muhusika hayupo, na kuambiwa uache nakala ya barua yako ya kupandishwa cheo.
Kumekuwa na ufuatiliaji wa bila mafanikio katika ngazi mbalimbali kuhusu suala hili.
Maswali ya kujiuliza ni kwamba;
  • Ni kwanini wawapandishe watu vyeo ilhali wanajua mtandao hautakuwepo kwa miezi minane?
  • Ni kwanini wawapandishe watu vyeo ilhali wanajua wahusika hawatakuwepo kwa miezi minane?
  • Na kama hizo ndiyo sababu za msingi je kuna uwezekano ofisi ya serikali kusiwe na mtandao au watumishi wenye dhamana na jambo hili kwa miezi minane?
  • Kama jambo liko nje ya uwezo wao kwa nini wasiseme ukweli?
Ni afadhali usimpe mtumishi barua ya kumpandisha kazi kama unajua hautabadilisha mshahara wake, inaumiza.
Wito wangu kwa wenye mamlaka;
  • Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri tunaomba uitishe mafaili yote ya watumishi waliopandishwa vyeo na uombe maelezo ya kutosha kwa wote ambao hawajabadilishiwa mishahara yao.
  • Ofisi ya TAKUKURU fuatilieni hapo kuna viashiria vya rushwa, tunaomba mchunguze.
  • Katibu tawala wa mkoa wa mwanza, halmashauri hii iko chini yako, tunaomba uwaulize
  • Waziri/katibu mkuu haya mambo yanawavunja moyo watumishi uwezo wa kuomba taarifa hizi mnao tunaomba fatilieni.
Mpeni mtumishi haki yake msimfanye kuwa mnyonge ndani ya nchi yake.
 
Katika ofisi ya utumishi halmashauri ya wilaya ya misungwi kumekuwa na uzembe na kutojali kwa kiwango cha juu kwa baadhi ya watumishi. Nitatolea mfano eneo moja tu kwa leo, nalo ni kuhusu upandishaji wa madaraja kwa watumishi katika halmashauri hii.
Mnamo tarehe 1/4/2018 watumishi wenye sifa walipandishwa vyeo na bodi ya ajira ya halmashauri hiyo. Lakini mpaka leo tunamalizia mwaka [miezi 8] hakuna mabadiliko yoyote katika mshahara wa watumishi hawa.
Wanapofatilia sababu zinazotolewa ni kuwa hakuna mtandao au muhusika hayupo, na kuambiwa uache nakala ya barua yako ya kupandishwa cheo.
Kumekuwa na ufuatiliaji wa bila mafanikio katika ngazi mbalimbali kuhusu suala hili.
Maswali ya kujiuliza ni kwamba;
  • Ni kwanini wawapandishe watu vyeo ilhali wanajua mtandao hautakuwepo kwa miezi minane?
  • Ni kwanini wawapandishe watu vyeo ilhali wanajua wahusika hawatakuwepo kwa miezi minane?
  • Na kama hizo ndiyo sababu za msingi je kuna uwezekano ofisi ya serikali kusiwe na mtandao au watumishi wenye dhamana na jambo hili kwa miezi minane?
  • Kama jambo liko nje ya uwezo wao kwa nini wasiseme ukweli?
Ni afadhali usimpe mtumishi barua ya kumpandisha kazi kama unajua hautabadilisha mshahara wake, inaumiza.
Wito wangu kwa wenye mamlaka;
  • Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri tunaomba uitishe mafaili yote ya watumishi waliopandishwa vyeo na uombe maelezo ya kutosha kwa wote ambao hawajabadilishiwa mishahara yao.
  • Ofisi ya TAKUKURU fuatilieni hapo kuna viashiria vya rushwa, tunaomba mchunguze.
  • Katibu tawala wa mkoa wa mwanza, halmashauri hii iko chini yako, tunaomba uwaulize
  • Waziri/katibu mkuu haya mambo yanawavunja moyo watumishi uwezo wa kuomba taarifa hizi mnao tunaomba fatilieni.
Mpeni mtumishi haki yake msimfanye kuwa mnyonge ndani ya nchi yake.
Mkuu zoezi la kupandishwa madaraja lilisimamishwa na Katibu Mkuu utumishi, mie nilipandishwa June 2016 lakini nina barua ya kubadilisha tarehe ya kupandishwa leo nina barua ya kuonyesha nimepandishwa April 2018 na ni mwezi uliopitwa nimerekebishiwa mshahara.Nakushauri uwe mtulivu .CCM oyeeee
 
Mbona halmashauri nyingi Bado issue ni Dodoma Wala sio misungwi au sehemu nyingine kwa sababu wao wameposit majina Dodoma hawajaapprove hawawezi fanya lolote kuwa mvumilivu tu
Katika ofisi ya utumishi halmashauri ya wilaya ya misungwi kumekuwa na uzembe na kutojali kwa kiwango cha juu kwa baadhi ya watumishi. Nitatolea mfano eneo moja tu kwa leo, nalo ni kuhusu upandishaji wa madaraja kwa watumishi katika halmashauri hii.
Mnamo tarehe 1/4/2018 watumishi wenye sifa walipandishwa vyeo na bodi ya ajira ya halmashauri hiyo. Lakini mpaka leo tunamalizia mwaka [miezi 8] hakuna mabadiliko yoyote katika mshahara wa watumishi hawa.
Wanapofatilia sababu zinazotolewa ni kuwa hakuna mtandao au muhusika hayupo, na kuambiwa uache nakala ya barua yako ya kupandishwa cheo.
Kumekuwa na ufuatiliaji wa bila mafanikio katika ngazi mbalimbali kuhusu suala hili.
Maswali ya kujiuliza ni kwamba;
  • Ni kwanini wawapandishe watu vyeo ilhali wanajua mtandao hautakuwepo kwa miezi minane?
  • Ni kwanini wawapandishe watu vyeo ilhali wanajua wahusika hawatakuwepo kwa miezi minane?
  • Na kama hizo ndiyo sababu za msingi je kuna uwezekano ofisi ya serikali kusiwe na mtandao au watumishi wenye dhamana na jambo hili kwa miezi minane?
  • Kama jambo liko nje ya uwezo wao kwa nini wasiseme ukweli?
Ni afadhali usimpe mtumishi barua ya kumpandisha kazi kama unajua hautabadilisha mshahara wake, inaumiza.
Wito wangu kwa wenye mamlaka;
  • Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri tunaomba uitishe mafaili yote ya watumishi waliopandishwa vyeo na uombe maelezo ya kutosha kwa wote ambao hawajabadilishiwa mishahara yao.
  • Ofisi ya TAKUKURU fuatilieni hapo kuna viashiria vya rushwa, tunaomba mchunguze.
  • Katibu tawala wa mkoa wa mwanza, halmashauri hii iko chini yako, tunaomba uwaulize
  • Waziri/katibu mkuu haya mambo yanawavunja moyo watumishi uwezo wa kuomba taarifa hizi mnao tunaomba fatilieni.
Mpeni mtumishi haki yake msimfanye kuwa mnyonge ndani ya nchi yake.
 
Back
Top Bottom