Hii habari japo nimeisoma leo lakini imenikumbusha mbali sana, huyo mzee sikuwahi kumfahamu lakini nimepata kumfahamu mke wake mkubwa alikuwa meneja katika benki ya NBC miaka ya 1980 na tukafahamiana na familia yake(huyo mama) ikiwa ni pamoja na kaka yake wakati huo alikuwa mhadhiri Udsm na baadaye akawa kiongozi mkubwa tu katika wizara mbalimbali(nisingependa kumtaja) na mama yao na ndugu wengine walikuwa wakiishi mbeya na kupitia yeye wengi wetu tulienda kusoma sekondari mbeya kule tukuyu ambapo ndio chimbuko la familia yao,nilikuwa sijui yule mama kama alifiwa na mumewe miaka mingi kutokana na sisi pia baada ya mzee wetu kufariki mawasiliano yalipungua