OCD Tabora, Askari aliyefatwa na baba wa mapacha waliouawa na kutobolewa macho akamshauri ujinga kwanini yupo kazini mpaka leo?

sifi leo

JF-Expert Member
Mar 30, 2012
5,013
8,369
1684696213024.png

Afande OCD mkoa wa Tabora tafadhali naomba unijibu swali hili.

Kama kijana Kisaka baada ya kubaini watoto wake mapacha wamefia mikononi mwa watoa huduma wa afya, kabla ya kukabidhiwa miili alienda kituo cha polisi kilicho karibu na hosptali hiyo na kukutana na askari ambaye hajamtaja kwa vyombo vya habari, amedai alikutana na mpelelezi wa kituo hicho cha polisi akamweleza jinsi wanae walivyo fia mikononi mwa watoa huduma afya.

Akadai kufa sio ishu ila alikuta marehemu wametobolewa macho, zaidi ya hapo alikuta mtoto mmoja amechunwa ngozi na kutobolwe na kutolewa mfupa mmoja.

Kwa majibu ya Kisaka anadai yule afande alimuuliza hivi, "Kwenu hamna mambo ya kishirikina kweli?" Mwisho akamwambia, "We toka hapa nenda hapo Kituo cha Afya mkamalizane na manesi."

Mh. Afande OCD, huyu askari anafanya nini kazini? Halafu ndio mpelelezi anaetegemewa huyo?
 
Kuna ushahidi? Maana serikali haiwezi fanyia kazi maneno matupu, japo Siungi mkono huo ufedhuli
 
Aisee Hapa bongo wapelelezi Ni washenzi Sana nilishawah kutana na mpelelezi mmoja mshenzi zaidi ya Huyo kituo cha polisi Karibu na temeke Hosp ila all in all hata Kama Huku wanajiona miungu watu Ila Mungu wa haki siku zote Yupo sisi tunamlilia Mungu tu atajibu kwa haki...
 
Asante sana. Na nakumbea usife leo bali uishi umri mrefu na maisha yenye baraka. Hii ndiyo ilitakiwa iwe habari muhimu sana kwenye vyombo vyetu vya habari.

Inaonekana kabisa kuna mtandao wa kuuza viungo vya binadamu. Je, polisi nao wanahusika? Kwa nini kosa la mauaji polisi analichukulia kimzaha mzaha tena kwa kufukuza mlalamikaji?
 
Aisee Hapa bongo wapelelezi Ni washenzi Sana nilishawah kutana na mpelelezi mmoja mshenzi zaidi ya Huyo kituo cha polisi Karibu na temeke Hosp ila all in all hata Kama Huku wanajiona miungu watu Ila Mungu wa haki siku zote Yupo sisi tunamlilia Mungu tu atajibu kwa haki...
Mungu alitupa akili na maarifa. Unamlilia tena afanye nini? Una wajibu wa kutumia ulivyopewa.
 
Asante sana. Na nakumbea usife leo bali uishi umri mrefu na maisha yenye baraka. Hii ndiyo ilitakiwa iwe habari muhimu sana kwenye vyombo vyetu vya habari. Inaonekana kabisa kuna mtandao wa kuuza viungo vya binadamu. Je, polisi nao wanahusika? Kwa nini kosa la mauaji polisi analichukulia kimzaha mzaha tena kwa kufukuza mlalamikaji?
Naomba unibeapo jiombee na Wewe.
 
Naitwa Kisaka Mtoisenga, mkazi wa Ushikola, Kaliua, Tabora. Tarehe 9/05/2023 saa 4 usiku mke wangu alijifungua watoto wawili mapacha kituo cha afya Kaliua. Watoto walizaliwa njiti (premature) na miezi 7 lakini tunamshukuru Mungu walizaliwa salama.

Kwa kuwa kituo cha afya Kaliua hakina uwezo wa kuhudumia watoto njiti wakatupa rufaa kwenda hospitali teule ya wilaya (Mission) yenye mashine za kuatamia watoto njiti (Incubators). Kituo hakina gari la wagonjwa, hivyo wakatuambia tukatafute usafiri.

Nikamuacha mke wangu na watoto wakiwa wazima wa afya, nikaenda kutafuta usafiri. Muda huo haikua rahisi kupata gari, nikapata Bajaji. Tulipofika wahuhudu wakasema tusubiri wawaandae watoto. Tukasubiri hadi saa 5 dereva akaanza kulalamika. Wahudumu wakasema tuendelee kusubiri. Ilipofika saa 6 dereva akataka kuondoka. Nikasema akiondoka sitapata Bajaji nyingine usiku huo. Nikawauliza wahudumu wakasema wanamalizia kuwaandaa watoto.

Nimwambia dereva nitamuongezea hela asubiri kidogo. Baadae wahudumu wakatoka na kutuambia bahati mbaya watoto wamefariki. Wakasema watatupa maiti kesho yake asubuhi.

Asubuhi wakatupatia maiti zikiwa ndani ya mabox, kwenye chumba maalumu cha upasuaji, ambacho kina giza. Wakatusisitiza tukazike siku hiyohiyo kwa haraka kwa sababu watoto njiti hawafanyiwi msiba.

Tulipofika nje kabla ya kupanda gari tukafungua mabox. Tukakuta watoto wameng'olewa macho, wamekatwa ulimi na wamechunwa ngozi kwenye paji la uso. Tukahamaki. Tukarudi kuuliza nini kimetokea, hawakutupa majibu ya kuridhisha.

Tukaenda Polisi, lakini wakatuambia tukazike tu maana wao hawashughuliki na ushirikina. Tukaenda kwa Mkuu wa wilaya, alipoona maiti akasema huo ni Ushirikina. Akatushauri tukazike tu maana hata tukienda mahakamani hatuwezi kushinda. Nikamuuliza kwanini ushirikina ufanyike hospitalini? Nikakataa kuzika.

Nikataka uchunguzi ufanyike. DC akaagiza maiti zipelekwe hospitali ya Urambo. Hadi leo zipo huko sijui nini kinaendelea. Naomba unipazie sauti Rais asikie. Watoto wangu wametendewa unyama kwenye kituo cha afya, halafu nanyimwa haki kwa kisingizio cha ushirikina? Naumia sana.

#MyTake
Mtag Mhe.Rais @samia_suluhu_hassan na viongozi wengine wanaohusika ili wachukue hatua.!
FB_IMG_1684436091124.jpg
 
DC pia, hii habari inaumiza sana! Huu uzembe ni wa kutisha. Nitashangaa hatua zisipochukuliwa. Rest in peace watoto wetu, mtusamehe kwa huu ukatili kuwakuta kwenye ardhi ya Taifa letu.
 

Ni kwamba maisha binafsi yanatuchanganya sana?!!!

Ni kwamba kazi zinatuendesha na kutufanya tusijue thamani ya kutoa huduma kwa watanzania wenzetu ?!!

Ni kwamba kwa kuwa tuko maofisini tumeamua kuwageuza wanyonge kuwa ni fuko la kupiga(punching bag) kupunguza mazito yanayokabili nafsi na maisha yetu?!!!

Ni kwamba tulipata "CHILD ABUSE" /TULITESWA SANA MAISHANI/TULIPITIA MAGUMU ,DHIKI ,NJAA,UFUKARA kufikia kuwa na "post-traumatic stress disorders-ptsd" kutupelekea kumuonea na kumshambulia KIHISIA kila aliye dhaifu na mnyonge?!!

Polisi ni mtoa huduma kama ilivyo ofisi nyingine ya umma....

Ni kwamba CPP Moshi hatufundishwi SAIKOLOJIA ?!!!!

Ni kwamba baadhi ya polisi hawajui kuwa hili ni taifa....na si pori la mtu kufanya atakayo ?!!!

Tuna taasisi nyingi nyeti zenye kuthamini watanzania zaidi ya upuuzi wa watu wachache huko polisi wanaojisahaulisha tu WAJIBU WAO KWA WATANZANIA WENZAO.....
 
Back
Top Bottom