Nyumba inapangishwa mbezi beach

Nyumba inapangishwa mbezi beach

Kitomai

JF-Expert Member
Joined
May 21, 2009
Posts
1,122
Reaction score
350
Ipo eneo la Samaki. Ina vyumba vitatu vya kulala, sebure, jiko. kodi shs 600,000 kwa mwezi. ruksa kulipa kodi ya miezi sita. Kwa maelezo zaidi piga simu 0717114409
 

Attachments

  • IMG00110-20110601-1341.jpg
    IMG00110-20110601-1341.jpg
    130.3 KB · Views: 119
  • IMG00111-20110601-1342.jpg
    IMG00111-20110601-1342.jpg
    256 KB · Views: 109
  • IMG00112-20110601-1343.jpg
    IMG00112-20110601-1343.jpg
    310.4 KB · Views: 81
  • IMG00115-20110601-1346.jpg
    IMG00115-20110601-1346.jpg
    212 KB · Views: 82
  • IMG00114-20110601-1345.jpg
    IMG00114-20110601-1345.jpg
    145.2 KB · Views: 81
  • IMG00117-20110601-1348.jpg
    IMG00117-20110601-1348.jpg
    175.9 KB · Views: 91
Kwanini mtu alipe kodi ya miezi sita?

Hii kitu siielewi kwa tabia ya kiafrica

Sasa ukipata miezi sita iweje?
Ukichukua deposit ya mwezi mmoja inakaaje?

Nadhani ni bora kuweka min contract ndio miezi 6.

Na je utadai pesa ya miezi 6 baada ya 6 months kuisha?

Ndio maana hongo hazitaisha
 
Kwanini mtu alipe kodi ya miezi sita?

Hili swali ungekua katika nafasi nzuri ya kulipatia majibu mazuri kama ungekua na wewe ni mpangishaji. Una nyumba ya kupangisha wewe? Kama hauna utakuja kupata majibu mazuri utakapokua na nyumba ya kupanga.

Nitakupatia jibu lingine la kudhani. Nadhani ''demand'' is higher than ''supply''.
Si unajua tena, the higher the demand the lower the supply the higher the price.

Mimi ningependa mtu awe analipa kodi mwisho wa mwezi baada kupata mshahara

Hii kitu siielewi kwa tabia ya kiafrica

Sasa ukipata miezi sita iweje?

Tafuta mkopo ofisini kwako au Benk au kwa ndugu na jamaa au kama vipi panga hotelini wao wanachukua kodi ya siku moja. Hacha kulalamika sana tafuta njia mbadara hii ndiyo Africa zaidi ya uijuavyo.
 
Kwanini mtu alipe kodi ya miezi sita?

Hili swali ungekua katika nafasi nzuri ya kulipatia majibu mazuri kama ungekua na wewe ni mpangishaji. Una nyumba ya kupangisha wewe? Kama hauna utakuja kupata majibu mazuri utakapokua na nyumba ya kupanga.

Nitakupatia jibu lingine la kudhani. Nadhani ''demand'' is higher than ''supply''.
Si unajua tena, the higher the demand the lower the supply the higher the price.

Mimi ningependa mtu awe analipa kodi mwisho wa mwezi baada kupata mshahara

Hii kitu siielewi kwa tabia ya kiafrica

Sasa ukipata miezi sita iweje?

Tafuta mkopo ofisini kwako au Benk au kwa ndugu na jamaa au kama vipi panga hotelini wao wanachukua kodi ya siku moja. Hacha kulalamika sana tafuta njia mbadara hii ndiyo Africa zaidi ya uijuavyo.
Mkuu, ukali huu hautakufukizia wateja kweli?
 
Hapana sitawafukuzia. Mimi ni mtu ambaye nipo wazi sana na nadhani hayo ndio maumbile yangu ya asili.
Naomba yeyote ambaye amekwazika kutokana na maoni yangu anisamehe.
 
Hapana sitawafukuzia. Mimi ni mtu ambaye nipo wazi sana na nadhani hayo ndio maumbile yangu ya asili. <br />
Naomba yeyote ambaye amekwazika kutokana na maoni yangu anisamehe.
<br />
Bongo bwana mtu ana poor customer service badala ya kujirekebisha analeta visingizio ndio maumbile yake. Km maumbile yapo hivyo na unajitambue kwanini usifanye kazi nyingine? Kazi ni combination ya skills.
Lakini mkuu kwa udadisi; hiyo law ni ya demand au ni law ya nini ulioweka pake kuzungumzia pricing za property? Halafu hata ingekuwa law ya demand; mbona wewe vitu vyako vyote huwa vipo overpriced? Au ni law ya comission. Am sure yr r nt doing good to yrself through overprice. Why nt trying selling many goods and increase turnover. Hata hao unaowafanyia hiyo biashara mali inakaa sokoni muda mrefu kisa overpricing mwisho wa siku unakosa wateja na wao wanaathirika. Kwahiyo, in one hand unapoteza wateja na pia hao wanaokupa vitu. Tunaweza kukushauri kwenye biashara inakuwaje kuliko unavyofanya kwa kuhitaji commission kubwa.
 
<br />
Bongo bwana mtu ana poor customer service badala ya kujirekebisha analeta visingizio ndio maumbile yake. Km maumbile yapo hivyo na unajitambue kwanini usifanye kazi nyingine? Kazi ni combination ya skills.
Lakini mkuu kwa udadisi; hiyo law ni ya demand au ni law ya nini ulioweka pake kuzungumzia pricing za property? Halafu hata ingekuwa law ya demand; mbona wewe vitu vyako vyote huwa vipo overpriced? Au ni law ya comission. Am sure yr r nt doing good to yrself through overprice. Why nt trying selling many goods and increase turnover. Hata hao unaowafanyia hiyo biashara mali inakaa sokoni muda mrefu kisa overpricing mwisho wa siku unakosa wateja na wao wanaathirika. Kwahiyo, in one hand unapoteza wateja na pia hao wanaokupa vitu. Tunaweza kukushauri kwenye biashara inakuwaje kuliko unavyofanya kwa kuhitaji commission kubwa.

Hiyo ndio customer service ya bongo!!
Sehemu nyingi duniani Mteja siku zote hubembelezwa na hupewa lugha nzuri wakati wa kufanya biashara lakini bongo mteja ananyanyaswa!
 
Mkuu, ukali huu hautakufukizia wateja kweli?

Amekuwa mkali for nothing. Tatizo sio mwenye nyumba kwani hata mimi ningekuwa na nyumba ya kupangisha uenda ningependa nilipwe hata kodi ya miaka miwili ili hizo pesa zinisaidie kufanya shughuli nyingine ya maendeleo. Hapa tatizo ni serikali amabayo haijaweka sheria ya kuwalinda wapangaji. Ukienda nchi zenye serikali zenye akili, hicho kitu cha kudai kodi ya zaidi ya mwezi mmoja hakipo. Ni kinyume cha sheria. Kodi inalipwa kila mwezi basi!!! Nchi nyingi za ulaya ndivyo ilivyo. Zaidi utatakiwa kulipa deposit ya mwezi mmoja au miwili kwa ajili ya guarantee ya vyombo na furniture.

Umefika wakati serikali ifikirie kuwalinda raia wake wanyonge kwani tabia hii ya kudai kodi kwa miezi kadhaa inasababisha watu wawe wadokozi na kuomba rushwa!!!!!

Ila nimefurahi kwamba angalau mwenye nyumba anataka kulipwa kwa Tshs. na sio USD kama wengi wanavyofanya. Kwa hilo nampongeza.

Niko interested kupanga hiyo nyumba, je kodi inaweza kushuka kidogo?

Tiba
 
Amekuwa mkali for nothing. Tatizo sio mwenye nyumba kwani hata mimi ningekuwa na nyumba ya kupangisha uenda ningependa nilipwe hata kodi ya miaka miwili ili hizo pesa zinisaidie kufanya shughuli nyingine ya maendeleo. Hapa tatizo ni serikali amabayo haijaweka sheria ya kuwalinda wapangaji. Ukienda nchi zenye serikali zenye akili, hicho kitu cha kudai kodi ya zaidi ya mwezi mmoja hakipo. Ni kinyume cha sheria. Kodi inalipwa kila mwezi basi!!! Nchi nyingi za ulaya ndivyo ilivyo. Zaidi utatakiwa kulipa deposit ya mwezi mmoja au miwili kwa ajili ya guarantee ya vyombo na furniture.

Umefika wakati serikali ifikirie kuwalinda raia wake wanyonge kwani tabia hii ya kudai kodi kwa miezi kadhaa inasababisha watu wawe wadokozi na kuomba rushwa!!!!!

Ila nimefurahi kwamba angalau mwenye nyumba anataka kulipwa kwa Tshs. na sio USD kama wengi wanavyofanya. Kwa hilo nampongeza.

Niko interested kupanga hiyo nyumba, je kodi inaweza kushuka kidogo?

Tiba

Hiyo rent ukiangalia hiyo amount imekuwa-pegged to USD!
Kuhusu landlord kulipwa kodi ya mwaka ama hata akitaka miaka 10 that's ok hakatazwi as long as lugha ya kiungwana na kibiashara inakuwa-involved......sio kama huko nyuma jama anasema " Kama hutaki kaa pembeni/au kama unataka kulipa kila mwezi nenda hotel"
Kama nilivyosema mteja bongo ni mtu wa kunyanyaswa na kulazimishwa tofauti na sehemu nyingine duniani ambapo mteja ni mfalme. Aaah anyway, ndio bongo yetu hiyo, kila mahali customer service ni zero, banks, kwenye daladala, bar, hotelini, serikalini, clubs, mpaka makanisani....Labda siku moja tutafika
 
Hapana sitawafukuzia. Mimi ni mtu ambaye nipo wazi sana na nadhani hayo ndio maumbile yangu ya asili.
Naomba yeyote ambaye amekwazika kutokana na maoni yangu anisamehe.
Mkuu upo sahihi,Ukweli apa Tanzania maswala ya estate bado tupo nyuma,uwezi kulinganisha na Kenya au South Afrika,UK or USA.
Nnafikiri haya mambo ya kutoa deposit then unalipa kodi kila mwezi apa Tanzania ni baada ya miaka 5 ijayo due to few apartments na uwingi wa wanazoziitaji
So kwa sas tukubali hali hii
 
mbona ghali hivyo? Mbezi beach ilikuwa zamani, sio siku hizi.
 
Binafsi si-encourage taking offense easily, lecturing on mistake of others, chronic fault- finding, nagging or blaming others for things that goes wrong. Nilichokua najaribu kuelezea hapo ni ''Housing supply and demand in Tanzania briefly''. kila ninapotoa tangazo napokea maoni kutoka kwa wadau mbali mbali. Maoni yanatofautiana kulingana na makundi mbali mbali, kutoka kwa ''young singles'', ''adult singles'', ''semiactive retirees'', ''active retirees'', ''double-income porfessionals, no children'', double-income professionals, one to three children'', ''single-parent households, one to three children''.
Ninayafanyia kazi maoni yenu. Asanteni sana.
 
Binafsi si-encourage taking offense easily, lecturing on mistake of others, chronic fault- finding, nagging or blaming others for things that goes wrong. Nilichokua najaribu kuelezea hapo ni ''Housing supply and demand in Tanzania briefly''. kila ninapotoa tangazo napokea maoni kutoka kwa wadau mbali mbali. Maoni yanatofautiana kulingana na makundi mbali mbali, kutoka kwa ''young singles'', ''adult singles'', ''semiactive retirees'', ''active retirees'', ''double-income porfessionals, no children'', double-income professionals, one to three children'', ''single-parent households, one to three children''.
Ninayafanyia kazi maoni yenu. Asanteni sana.
Sasa unalalamika nini? Watu wanakusaidia kubehave proffesionally wewe unaleta maneno mengi? Ishu si ku-encourage kama unavyotuaminisha, tunakushauri how you can improve business. Kuna watu wanaexposure, skills na wafanyabiashara kwahiyo sikiliza unachoambiwa. Sentensi ya mwisho ilitosha saana bila maelezo mengi. Na wengine hapa ni wateja wako.
 
Kwanza unaonekana hujasomea Estate Agency and Marketing umeona tu kuna potential ukaventure. Umevamia tu fani jua kwamba hiyo ni Profession na inahitaji customer care ya hali ya juu. Nakushauri nipm nikupe free lecture on the practice of Estate Agency and Marketing na pia Estate management as a whole.
 
Kitomai ndio watu kama nyie/wewe mtakuwa mnagombana na wateja wenu

Nimekuuliza maswali unaniuliza maswali? Si lazima kila mtu apangishe nyumba alizonazo extra... mfwuuu kubali umechemsha hata mtoto miaka 7 atajibu vizuri asifukuze wateja.

Kwa hiyo naomba uelewe kuwa sio kila mwenye kuuliza swali hanakuwa hajui mambo

Umeandika mengi kunijibu kwa hasira ulitegemea nini kuweka post yako humu na tusijibu?

Nenda kajifunze mawasiliano na kupunguza asila wakati unategemea ka asilimia fulani ikusaidie na ujifunze kusikiliza ushauri wa wengine

Sijui mambo ya age limit na status ya mtu inaleta utofauti hao wote lazima wanapata income kutoka mahala
 
MAra nyingine sisi customers tunacomplicate mambo pasi lazima; Bongo yetu tunaifahamu, na default za wapangishaji tunazifahamu (miezi6, 12, 24), wengi wetu ama tumepanga, ama tumepangisha; iwe nyumba ya kuishi au ya biashara. Hata kama umeishi sana kwa wenzetu kiasi cha kusahau maisha halisi ya bongo, unauliza kwa mpangishaji au dalali kwa Lugha nzuri tu (mf; Je, siwezi kulipa kwa mwezi?) kwa hakika kama mwenye nyumba akitathmini chanzo chako cha pesa akajiridhisha kuwa kweli utalipa kila ifikapo mwisho wa mwezi bila kukosa (Visingizio) hawezi kataa kukupangisha kwa terms unazotaka (biashara maelewano)!
Ni hayo tu wadau, tunajenga!
 
Nimewasikia wadau.nipo tayari kujifunza zaidi.
 
Kitomai; Nimependa hiii...."Niko tayari kujifunza"...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom