Nyumba inapangishwa 150,000

Nyumba inapangishwa 150,000

...mbona kama unatafuta mlinzi wa kukulindia tu sheikh!
...150,000??
Mkuu ni ndogo au kubwa. Unajua sijawahi kupangisha nyumba na hii nimeijenga kwa ajili hiyo hata hivyo hali ni ngumu, kidogo gawana na mwenzio. Aliyetayari anakaribishwa kuja kuiona. Ila kumbuka tayari jana nimewakabidhi madalali, sasa sijui mpaka wiki hii iishe itakuwa bado ipo.
 
kodi yote hiyo kumbe ukuta hakuna, umeme hakuna, iko mpigi, maji haina. doooooo
Njoo uione, ndio utaamua. Ni kweli umeme haina, bado nahangaika na watu wa umeme, ukuta una msingi bado. Ila maji jirani yetu anayo. Karibu ujionee kitu kipya
 
Mpaka ijumaa kazi zitakuwa zimeisha,unakaribishwa kuja kuiangalia
Biashara ni kazi ngumu sana kama huijui. Yaani nije kuona vague imagination?

Mtu akiona picha, hata kama haijamalizika tayari anao uwezo wa kujenga picha akilini mwake kuwa itakapomalizika itafanana vipi. Mtu pekee anayeweza kuja kuiona kwa maneno tu ya kuambiwa na wewe ni HAMNAZO
 
Biashara ni kazi ngumu sana kama huijui. Yaani nije kuona vague imagination?

Mtu akiona picha, hata kama haijamalizika tayari anao uwezo wa kujenga picha akilini mwake kuwa itakapomalizika itafanana vipi. Mtu pekee anayeweza kuja kuiona kwa maneno tu ya kuambiwa na wewe ni HAMNAZO
Mkuu nimekuelewa. Nitalifanyia kazi. Ila je kwa hali ilivyo hiyo bei nikubwa au ndogo maana kuna mdau kanikatisha tamaa
 
Toa maelezo ya wazi.kujitambulisha sana huku jf kunaweza kukapeleka watu kwenye kale kamsitu.!
 
Mkuu nimekuelewa. Nitalifanyia kazi. Ila je kwa hali ilivyo hiyo bei nikubwa au ndogo maana kuna mdau kanikatisha tamaa
Bei ni nzuri, labda umbali umpe mtu shida. Lakini all in all, kila sehemu ina wakazi wake. SI kila mtu anaamka kwenda mjini daily, hiyo nyumba akiifumania mfanyabiashara au dereva wa masafa kwa hakika atafurahia utulivu.
 
Bei ni nzuri, labda umbali umpe mtu shida. Lakini all in all, kila sehemu ina wakazi wake. SI kila mtu anaamka kwenda mjini daily, hiyo nyumba akiifumania mfanyabiashara au dereva wa masafa kwa hakika atafurahia utulivu.
Nimekupata vyema. Kuna dalali nimempa hii kazi, nadhani kesho atanirudishia majibu,maana nasikia jana alienda na mteja, mimi sikuweza kufika
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom