Kila siku nasema elimu ya uraia kabla ya chaguzi au wakati hakuna uchaguzi ni muhimu sana
Kuwaeleza watu haki zao na umuhimu wa wao kujiandikisha kupiga kura na kuchagua viongozi wao
Asilimia kubwa ya vijana hawana vile vitambulisho vya mpiga kura na hili ni tatizo la kila sehem
wengi hata waliovipoteza bado hawajapata vingine
Tungeviambia vyama vya siasa kuwa wakati hakuna issue yoyote ya uchaguzi waende huko vijijini wakatoe alimu ya uraia kuwaambia wananchi umuhimu wa kupiga kura na kujiandikisha na umuhimu wa kuwachagua watu au viongozi wanaowapenda na watakaoowaletea maendeleo yao na sio bora kiongozi ambaye anaonekana kwenye kampeni tuu akishapata kura ndo ameondoka