Jimena
JF-Expert Member
- Jun 10, 2015
- 25,852
- 95,802
Ni sawa kabisa!Leo nikasema acha nikasafishe macho club baada ya kukosa usingizi huku ugenini nikaona niende sehemu yenye kelele karibu na nilipofikia maana nazisikia.
Kufika nikaona kumekucha balaa watu wamejazana kama hakuna zuio la mikusanyiko kwa nchi nzima. Au walimaanisha mikusanyiko ya KATIBA tu???
Anyway nirudi kwenye mada nikiwa hapa club ambapo ndio naandikia uzi huu saivi, Dj anachanganya ngoma za circular na za Dini. Sasa najiuliza hii ni Sawa? Maana naona waliopo club VIBE linazidi kila likipigwa goma la Dini.
Nakumbuka wakati naupokea mwaka huu saa5.59 pia nlikua Bar ikapigwa ngoma ya Nimeuona Mkono wako Bwana by Zablon. Aisee tulishangila balaa
Halafu mwanaume unapata wapi ujasiri wa kucheza juu ya meza?? Huu ni upuuzi sana
Maoni yenu wadau