Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,346
- 26,138
Hawa ni waasisi wa Muungano wetu wa Srikali mbili ulioundwa rasmi mnamo tarehe 26 Aprili 1964. Ni hawa ambao walichambua mazingira na hoja zilizokuwepo katika Zanzibar na Tanganyika na kuamua walivyoamua. Ni hawa waliotuwakilisha katika kuuunda Muungano huu jinsi ulivyo. Yaani,Muungano wa Serikali mbili. Waasisi hawa wa Tanzania yetu tunawaheshimu,tunawakumbuka na kuwajali daima.
Lakini, hatupaswi kuyachukulia maamuzi na maneno yao kama Msahafu,kwa maana ya kutobadilika. Muundo huu wa Muungano wa Serikali mbili ulitokana na hekima yao,sababu zao,mazingira waliyoyaona kama viongozi wakuu wa mataifa ya Tanganyika na Zanzibar na kadhalika na kadhalika. Waasisi hawa walitumia kila aina ya ujuzi,ufikiri,mantiki na hoja kufikia hapo kwenye Serikali mbili. Sasa hawapo. Mzee Karume alituacha mwaka 1972 wakati Mwalimu Nyerere alituacha mwaka 1999.
Waliotuacha nasi na Muungano waliouweka ulivyo wao,wametuacha na mazingira tofauti. Mazingira ya kiuchumi,kisiasa,kiutamaduni na kijamii kwa ujumla. Mazingira ya kimaendeleo, ushirikiano na nchi nyingine, nchi kusonga mbele na sayansi na teknolojia. Nchi imebadilika. Hoja za kimuungano haziwezi kubaki vile vile. Lazima zibadilike.
Tume ya Jaji Warioba ilipitia kila ainaya nyaraka ya busara ya Waasisi hawa. Ilitumia nyaraka hizo kama msingi wa kupambanisha ya wakati ule na ya sasa. Wananchi wakasikilizwa na kunukuliwa.Mwisho mwishoni, Tume ya Jaji Warioba ikafika tamati ya kuwa na Serikali tatu. Tume iko sahihi kadiri ilivyoyaona na kuyashuhudia mabadiliko,manung'uniko,malalamiko,miiko.matamko na mihemko ya pande zote za Muungano.
Hoja yangu ni kuwa, Mwalimu Nyerere na Mzee Karume walikuwa sahihi kwa muda wao na matumizi yetu kama nchi. Na Tume ya Jaji Warioba iko sahihi kadiri ya wakati huu tulionao. Nasema Mwalimu Nyerere na Mzee Karume si biblia kwa maana ya maneno,matendo,mawazo na maamuzi yao. Yatabaki kukumbukwa na kutumiwa kama msingi lakini hayatabaki kama nyororo ya kufunga fikra na changamoto za kinchi.
Serikali tatu,moja au mbili ni maamuzi yetu.Lakini, Waasisi wasitufunge kubadilika
cc Waberoya Nguruvi3 Yericko Nyerere, Ben Saanane Chris Lukosi Mzee Mwanakijiji Mamndenyi FaizaFoxy MSALANI Simiyu Yetu ifweero Ruttashobolwa Pasco zumbemkuu JokaKuu na wengineo karibuni kwa mjadala
Lakini, hatupaswi kuyachukulia maamuzi na maneno yao kama Msahafu,kwa maana ya kutobadilika. Muundo huu wa Muungano wa Serikali mbili ulitokana na hekima yao,sababu zao,mazingira waliyoyaona kama viongozi wakuu wa mataifa ya Tanganyika na Zanzibar na kadhalika na kadhalika. Waasisi hawa walitumia kila aina ya ujuzi,ufikiri,mantiki na hoja kufikia hapo kwenye Serikali mbili. Sasa hawapo. Mzee Karume alituacha mwaka 1972 wakati Mwalimu Nyerere alituacha mwaka 1999.
Waliotuacha nasi na Muungano waliouweka ulivyo wao,wametuacha na mazingira tofauti. Mazingira ya kiuchumi,kisiasa,kiutamaduni na kijamii kwa ujumla. Mazingira ya kimaendeleo, ushirikiano na nchi nyingine, nchi kusonga mbele na sayansi na teknolojia. Nchi imebadilika. Hoja za kimuungano haziwezi kubaki vile vile. Lazima zibadilike.
Tume ya Jaji Warioba ilipitia kila ainaya nyaraka ya busara ya Waasisi hawa. Ilitumia nyaraka hizo kama msingi wa kupambanisha ya wakati ule na ya sasa. Wananchi wakasikilizwa na kunukuliwa.Mwisho mwishoni, Tume ya Jaji Warioba ikafika tamati ya kuwa na Serikali tatu. Tume iko sahihi kadiri ilivyoyaona na kuyashuhudia mabadiliko,manung'uniko,malalamiko,miiko.matamko na mihemko ya pande zote za Muungano.
Hoja yangu ni kuwa, Mwalimu Nyerere na Mzee Karume walikuwa sahihi kwa muda wao na matumizi yetu kama nchi. Na Tume ya Jaji Warioba iko sahihi kadiri ya wakati huu tulionao. Nasema Mwalimu Nyerere na Mzee Karume si biblia kwa maana ya maneno,matendo,mawazo na maamuzi yao. Yatabaki kukumbukwa na kutumiwa kama msingi lakini hayatabaki kama nyororo ya kufunga fikra na changamoto za kinchi.
Serikali tatu,moja au mbili ni maamuzi yetu.Lakini, Waasisi wasitufunge kubadilika
cc Waberoya Nguruvi3 Yericko Nyerere, Ben Saanane Chris Lukosi Mzee Mwanakijiji Mamndenyi FaizaFoxy MSALANI Simiyu Yetu ifweero Ruttashobolwa Pasco zumbemkuu JokaKuu na wengineo karibuni kwa mjadala
Last edited by a moderator: