...Kwa msaada wa Mwenyezi Mungu, na imani mliyonayo juu yetu, tunapata,
na tutazidi kupata nguvu za kuendesha serikali yenu. Lakini tunawaomba
msisahau, na mara nyingi sana, nimekukumbusheni jambo hili, kwamba
serikali haiwezi kufanya kila kitu.
Utajiri wa Tanganyika, bado uko ardhini. Hatuanzi na akiba kubwa ya
fedha kama Ghana kwa mfano, iliyoanza nayo ilipopata uhuru wake.
Hatuna mkononi fedha walizonazo ndugu zetu wa Nigeria. Kwa kweli,
elimu yetu iko nyuma zaidi kuliko Kenya na Uganda.
Kwa hiyo, tunaanza bila ya kuwa na wananchi wa kutosha, wenye elimu ya
juu, tunayohitaji katika jitihada zetu za kujenga utajiri wa nchi hii.
Lakini matatizo haya, hayanitishi mimi, hayawatishi wenzangu, na wala
hatuombi kwamba yawatisheni ninyi. Tunayaona kwamba ni jaribio tu.
Lakini jaribio hili, na umasikini, si la serikali tu, ni la kila raia
wa Tanganyika.
...
HIVI JAMANI ALIMAANISHA NINI HUYU MKUU WA NCHI ALIYETUKUKA?
na tutazidi kupata nguvu za kuendesha serikali yenu. Lakini tunawaomba
msisahau, na mara nyingi sana, nimekukumbusheni jambo hili, kwamba
serikali haiwezi kufanya kila kitu.
Utajiri wa Tanganyika, bado uko ardhini. Hatuanzi na akiba kubwa ya
fedha kama Ghana kwa mfano, iliyoanza nayo ilipopata uhuru wake.
Hatuna mkononi fedha walizonazo ndugu zetu wa Nigeria. Kwa kweli,
elimu yetu iko nyuma zaidi kuliko Kenya na Uganda.
Kwa hiyo, tunaanza bila ya kuwa na wananchi wa kutosha, wenye elimu ya
juu, tunayohitaji katika jitihada zetu za kujenga utajiri wa nchi hii.
Lakini matatizo haya, hayanitishi mimi, hayawatishi wenzangu, na wala
hatuombi kwamba yawatisheni ninyi. Tunayaona kwamba ni jaribio tu.
Lakini jaribio hili, na umasikini, si la serikali tu, ni la kila raia
wa Tanganyika.
...
HIVI JAMANI ALIMAANISHA NINI HUYU MKUU WA NCHI ALIYETUKUKA?