Nyerere Against Islam in Zanzibar and Tanganyika

Mimi kila nilichoandika kuhusu Nyerere nina ushahidi.
Una ushahidi kwa mujibu wa nani?
Kitabu changu "The Life and Times of Abdulwahid Sykes..." kimechapwa London mwaka 1998.
Kwa mtu anayechunguza mambo, kitabu si tatizo facts are. Suala kuu ni ukweli wa kinachozungumziwa.
Nyerere yu hai na alikisoma.
Sikusuburi afe ndiyo nizungumze habari zake.
Ningefurahi ukaweka na feedback au response yake kuhusiana na tuhuma zako.
Nadhani ushaelewa kuwa uoga si sifa yangu.
Acha sifa zako zionekane na zisemwe na wengine, sio na wewe mwenewe kwa kujipigia chapuo.
Lete jingine kama lipo.

Yapo mengi, ila tuanze na haya/
 
Una ushahidi kwa mujibu wa nani?
Kwa mtu anayechunguza mambo, kitabu si tatizo facts are. Suala kuu ni ukweli wa kinachozungumziwa.

Ningefurahi ukaweka na feedback au response yake kuhusiana na tuhuma zako.

Acha sifa zako zionekane na zisemwe na wengine, sio na wewe mwenewe kwa kujipigia chapuo.

Yapo mengi, ila tuanze na haya/[/COLOR]

Kwa kawaida mtu mwenye kutukana huwa sijadilinae chochote.
Lakini hii post ya pili imekuja na adabu.

Kuhusu niache wengine wanisemee hili halitowezekana kwa kuwa uleinitukana kuwa mimi ni...ni wewe kwa hiyo siwezi kusubiri mtu mwingine anijibie. Ndiyo nikakujibu uongo si sifa yangu na ndiyo maana hata hapa JF natumia jina langu halisi sijajificha.

Ushahidi ninao kwa kila nilichosema nimeweka ushahidi katika kitabu. Ikiwa wewe unataka ushahidi wa kimahakama katika tafiti ya kisomi hilo sijui tutalifanyaje lakini kama unaweza kuniongoza kwa kunifunza tufanyeje ili upatikane ushahidi kama wa mahakamani kama unavyoainishwa na ''law of evedence'' mimi Insha Allah niko tayari kutoa ushirikiano.
 
Mjadala wa watu waliofilisika mawazo. Siwezi kujadili hisia za mtu!
 
Ningeshangaa kama Mohamed Said asingetia mguu ndani ya hii thread ha ha ha ha ha ha.
 
Last edited by a moderator:
Kwa kawaida mtu mwenye kutukana huwa sijadilinae chochote.
Lakini hii post ya pili imekuja na adabu.

Kuhusu niache wengine wanisemee hili halitowezekana kwa kuwa uleinitukana kuwa mimi ni...ni wewe kwa hiyo siwezi kusubiri mtu mwingine anijibie. Ndiyo nikakujibu uongo si sifa yangu na ndiyo maana hata hapa JF natumia jina langu halisi sijajificha.

Ushahidi ninao kwa kila nilichosema nimeweka ushahidi katika kitabu. Ikiwa wewe unataka ushahidi wa kimahakama katika tafiti ya kisomi hilo sijui tutalifanyaje lakini kama unaweza kuniongoza kwa kunifunza tufanyeje ili upatikane ushahidi kama wa mahakamani kama unavyoainishwa na ''law of evedence'' mimi Insha Allah niko tayari kutoa ushirikiano.
Mohamed Said, kwa vile kila siku tunapata ufahamu mpya kuhusu yaliyojiri Zanzibar na Afrika Mashariki kwa ujumla, ningekuuliza maswali haya mawili:
1. Je, bado unaamini kuwa Okello alitumwa na Wakristo kwenda kufanya mapinduzi ZNZ
2. Je,Nyerere ndiye chanzo cha mapinduzi ya ZNZ

Ningependa unijibu kwa maoni yako na wala si nukuu za kitabu au vitabu kwasababu ninazo na nimezisoma sana.
 
Mohamed Said, kwa vile kila siku tunapata ufahamu mpya kuhusu yaliyojiri Zanzibar na Afrika Mashariki kwa ujumla, ningekuuliza maswali haya mawili:
1. Je, bado unaamini kuwa Okello alitumwa na Wakristo kwenda kufanya mapinduzi ZNZ
2. Je,Nyerere ndiye chanzo cha mapinduzi ya ZNZ

Ningependa unijibu kwa maoni yako na wala si nukuu za kitabu au vitabu kwasababu ninazo na nimezisoma sana.
Mzee Said vipi umekimbia mnakasha? Tunahitaji darsa!!!
 
Mzee Said vipi umekimbia mnakasha? Tunahitaji darsa!!!

Sijakimbia mnakasha ndugu yangu. Tatizo ni kuwa mie siwezi kutukanana sasa inapofika hali ya kejeli na matusi basi huvunjika nguvu.

Insha Allah mimi nipo na hii ilm ni amana na kwa kuwa nyie wenye amana mmekuja kudai amana yenu ni wajibu wangu nirejeshe amana hiyo kwenu.

Insha Allah tutaendelea na darsa kadri Allah atakavyotuwezesha.
 
Mohamed Said, kwa vile kila siku tunapata ufahamu mpya kuhusu yaliyojiri Zanzibar na Afrika Mashariki kwa ujumla, ningekuuliza maswali haya mawili:
1. Je, bado unaamini kuwa Okello alitumwa na Wakristo kwenda kufanya mapinduzi ZNZ
2. Je,Nyerere ndiye chanzo cha mapinduzi ya ZNZ

Ningependa unijibu kwa maoni yako na wala si nukuu za kitabu au vitabu kwasababu ninazo na nimezisoma sana.

Umeniuliza swali nami nimelipokea ila sijui kwa nini uaniwekea masharti jinsi ya kujibu.
Inaelekea unaniamini sana kiasi cha kutaka fikra zangu pasi na kufanya rejea za vitabu vya wasomi.

Insha Allah nitajitahidi kujibu.

Okello.

Kwanza hebu ngoja tumuweke pembeni Insha Allah wakati wake utakapofika tutamzungumza.

Ningependa tuanze na watu, sehemu na matokeo muhimu katika mapinduzi ya Zanzibar.

Kulikuwa na kambi Kipumbwi iliyokuwa imewekwa rasmi kwa kuwafunza mamluki wa Kimakonde kutoka shamba la mkonge la Sakura na kwengineko kwenda kuivamia Zanzibar.

Hawa Wamakonde walikuwa wakifanya kazi ya manamba katika mashamba ya mkonge Tanga.

Hawa Wamakonde kutoka Kipumbwi ndiyo waliovushwa kwenda Zanzibar mwaka 1961 kuipigia kura ASP na mwaka 1964 kwenda kupindua serikali ya Mohamed Shamte ambayo ilikuwa ni muungano wa vyama viwili ZPPP na ZNP.

Walioshughulika na kambi hii upande wa Tanganyika walikuwa Jumanne Abdallah aliyekuwa RC wa Tanga, Victor Mkello aliyekuwa kiongozi wa chama cha wakata mkonge na Mohamed Omari Mkwawa kijana wa mjini Tanga aliyepewa kazi ya kuwatia Wamakonde katika kambi na kuwavusha.

Jimmy Ringo mwanachama wa ASP alikuwa Tanga mjini ofisi ya TANU Br. 14 akiratibu operasheni hii yote.
Jimmy Ringo alikuja kuuawa baada ya mapinduzi.

Mauaji mengi sana ya Waarabu siku ya mapinduzi yalifanywa na hawa Wamakonde kutoka Kipumbwi wakiwa na John Okello.

Asikuambie mtu ati mapinduzi ya Zanzibar yalifanywa na ASP na Umma Party ya Abdulrahman Babu.

Swali la kujiuliza ni nani aliruhusu kuwekwa kwa kambi hii hapo Kipumbwi?
 
Umeniuliza swali nami nimelipokea ila sijui kwa nini uaniwekea masharti jinsi ya kujibu.
Inaelekea unaniamini sana kiasi cha kutaka fikra zangu pasi na kufanya rejea za vitabu vya wasomi.

Insha Allah nitajitahidi kujibu.

Okello.

Kwanza hebu ngoja tumuweke pembeni Insha Allah wakati wake utakapofika tutamzungumza.

Ningependa tuanze na watu, sehemu na matokeo muhimu katika mapinduzi ya Zanzibar.

Kulikuwa na kambi Kipumbwi iliyokuwa imewekwa rasmi kwa kuwafunza mamluki wa Kimakonde kutoka shamba la mkonge la Sakura na kwengineko kwenda kuivamia Zanzibar.

Hawa Wamakonde walikuwa wakifanya kazi ya manamba katika mashamba ya mkonge Tanga.

Hawa Wamakonde kutoka Kipumbwi ndiyo waliovushwa kwenda Zanzibar mwaka 1961 kuipigia kura ASP na mwaka 1964 kwenda kupindua serikali ya Mohamed Shamte ambayo ilikuwa ni muungano wa vyama viwili ZPPP na ZNP.

Walioshughulika na kambi hii upande wa Tanganyika walikuwa Jumanne Abdallah aliyekuwa RC wa Tanga, Victor Mkello aliyekuwa kiongozi wa chama cha wakata mkonge na Mohamed Omari Mkwawa kijana wa mjini Tanga aliyepewa kazi ya kuwatia Wamakonde katika kambi na kuwavusha.

Jimmy Ringo mwanachama wa ASP alikuwa Tanga mjini ofisi ya TANU Br. 14 akiratibu operasheni hii yote.
Jimmy Ringo alikuja kuuawa baada ya mapinduzi.

Mauaji mengi sana ya Waarabu siku ya mapinduzi yalifanywa na hawa Wamakonde kutoka Kipumbwi wakiwa na John Okello.

Asikuambie mtu ati mapinduzi ya Zanzibar yalifanywa na ASP na Umma Party ya Abdulrahman Babu.

Swali la kujiuliza ni nani aliruhusu kuwekwa kwa kambi hii hapo Kipumbwi?
Sijakuwekea masharti ya kujibu, nisichokitpendelea katika mjadala ni nukuu za maandishi yako ambayo tayari nimeyasoma mara nyingi sana, na nimesoma maandiko ya wanazuoni wengine mara nyingi sana.

Mzee Said, ukiangalia maswali niliyokuuliza bado hujajibu, ulichofanya ni kuzunguka. Maswali yapo wazi kabisa.

1. Je,bado unaamini Okello alitumwa kwenda kufanya mapinduzi Zanzibar

2. Je, Nyerere ndiye chanzo cha mapinduzi (Umeongelea wakata mkonge na wamakonde, ningependa utufahamishe endapo Nyerere aliwatuma au walitumwa na mtu mwingine). Nasema hivi ili mbele ya safari tujue tunamjadili nani na siyo kuzunguka zunguka porini kwa kutaja makundi.
 
Nimeona umenitukana.
Hata hivyo nitakujibu.

Mimi kila nilichoandika kuhusu Nyerere nina ushahidi.
Kitabu changu "The Life and Times of Abdulwahid Sykes..." kimechapwa London mwaka 1998.

Nyerere yu hai na alikisoma.
Sikusuburi afe ndiyo nizungumze habari zake.

sidhani kama wewe ni kati ya author ambao nyerere alikuwa akiwasoma, hii itakuwa ni kashfa kwa nyerere how can such a genius read fools writings such as yours, disgusting.
 
Mohamed Said,
Nadhani unafahamu wazi kuwa unachokieleza kina walakini ndio maana hujibu maswali.
Unafaham kuwa mapinduzi hayakufanywa na Nyerere wala Okello hakutumwa kama unavyowaaminisha watu.

Unafahamu kuwa unahitaji kitu cha ziada kuunganisha ukristo na Nyerere katika hali ya kisiasa iliyopo sasa.
Unafahamu kuwa wanazuoni WZN wamekupinga kwa hoja hizi.

Nimekuuliza maswali very basic na umegundua kuwa mbele ya safari utakwama, kama kawaida umeahirisha mnakasha ili nyuzi nyingine ianzishwe.

Mada hii ni nzuri sana na nilidhani tungekuwa na mnakasha mzuri sana, sidhani kama litatokea hilo.
 
Wanajamvi, kabla ya kueleza jambo nililokusudia nimeiweka makala hii iliyotoka katika gazeti la Rai Mwema tole 227 la tarehe 22 feb 2012 makusudi kabisa.
Mwandishi wa Makala hii ni Ahmed Rajab ambaye hana tatizo la kidini na Mohamed Said litakalo kwaza mjadala.
Mohamed Said atufahamishe haya yafuatayo

1. Je, naye alifanya mahojiano na Wna mapinduzi kama alivyodai mwenzake Ahmed Rajab
2. Je, anaikubali au kuikataa makala hii kwa ukweli au uongo wake?

Kwanza naanza kwa kumnukuu
Mohamed Said; Asikuambie mtu ati mapinduzi ya Zanzibar yalifanywa na ASP na Umma Party ya Abdulrahman Babu

Ahmed Rajab;YAFUATAYO ni masimulizi mafupi ya kipindi kifupi cha Mapinduzi ya Zanzibar ya Januari, 1964 yaliyoipindua serikali ya ubia ya chama cha Zanzibar Nationalist (maarufu Hizbu) na kile cha Zanzibar and Pemba People's Party (ZPPP). Tunaangazia nini hasa kilitokea usiku wa Jumamosi Januari 11, yaliyojiri siku ya pili yake na mwezi mzima wa Januari, mwaka 1964 .
Tumeyakusanya masimulizi haya baada ya kuzungumza na walioshiriki katika Mapinduzi hayo ambao baadaye walisaidia kudhibiti madaraka na kuunda taasisi zilizoziba pengo la Serikali iliyopinduliwa ya Waziri Mkuu, Muhammed Shamte Hamadi.

Usiku wa manane wa Januari 11, makada wapatao 200 wa Umoja wa Vijana wa Afro-Shirazi (Afro-Shirazi Youth League) walielekea kwenye kambi ya polisi ya Ziwani, nje kidogo ya mji huko Unguja.

Wakiongozwa na Yusuf Himid wapinduzi hao hawakukabiliwa na upinzani walipofika Ziwani ila waliikuta ghala ya silaha iko wazi na wakazinyakua silaha na kukimbia nazo hadi kwenye uwanja ulio nje ya jengo la Raha Leo.

Hapo ndipo palipokuwa makao makuu ya Mapinduzi kwa siku chache na ndipo wapinduzi walikokuwa wakipewa silaha.
Studio za redio ya Serikali pia zilikuwa hapo.

Moja ya sababu zilizoyafanya Mapinduzi yafanikiwe haraka ni uamuzi wa viongozi wa Serikali iliyopinduliwa - Sheikh Muhammed Shamte na Sheikh Ali Muhsin Barwani - kuwataka wafuasi wao wasitumie nguvu kuyapinga.

Hivyo, mbali na mapigano yaliyozuka saa za asubuhi ya Jumapili Januari 12, mbele ya Steshini ya Polisi Malindi, hapajazuka mapigano Unguja kati ya waliopindua na waliopinduliwa. Pemba nako pia hakukuwa na upinzani ijapokuwa kisiwa hicho kilikuwa ngome ya vyama vya ZNP na ZPPP.

Wengi wa wapiganaji waliokuwa kwenye Stesheni ya Polisi ya Malindi walikuwa wakuu wa polisi Wakiingereza. Wakipigana na makada wa Umma Party ambao ndio pia waliouteka uwanja wa ndege, bandari pamoja na kituo cha mawasiliano ya nje cha Cable & Wireless, kilichokuwa kwenye jengo ambalo sasa ni Hoteli ya Serena Mji Mkongwe.

Kwa hakika, kinyume cha baadhi ya watu walivyoandika hapakutokea mauaji ya kimbari. Aliyeanzisha uvumi huo alikuwa John Okello aliyeandika kwenye kitabu chake kuhusu Mapinduzi ya Zanzibar kwamba watu zaidi ya elfu kumi waliuliwa. Okello aliongeza kwamba aliamrishwa na Yesu Kristo kuwakomboa ‘Waafrika' wa Zanzibar kutoka kwa ‘wageni'.

Tutamrejelea Okello na wengine waliokuwa Raha Leo baadaye. Kwanza tukumbushe kwamba mkesha wa Januari 12, mwaka 1964, Zanzibar haikuwa na jeshi. Kulikuwa polisi waliokuwa wakiongozwa na Waingereza. Wengi wa askari polisi walikuwa raia wa Tanganyika. Serikali iliyopinduliwa ilikataa kuandikiana mkataba wa kijeshi na Uingereza kwa sababu ikihisi mkataba kama huo utaonekana kuwa wa kikoloni.

Hatuwezi kusema ni nani hasa aliyepiga risasi ya mwanzo au ya mwisho katika Mapinduzi. Naitoshe tusemapo kwamba kwa vile hakukuwa na upinzani, Serikali iliyokuwa madarakani iliporomoka kama ‘nyumba ya karata'.
Tuwarejelee sasa waliokuwa Raha Leo, makao makuu ya Mapinduzi kwa siku chache. Kwanza tumuangalie Okello ambaye sauti yake ndiyo iliyokuwa ikivuma kwenye Redio Zanzibar.

Hatuna uhakika nani alimpeleka Okello Raha Leo. Wengine wanasema ni Yusuf Himidi. Wengine wanasema ni Seif Bakari aliyetoa rai atumiwe kutoa matangazo kwenye redio kwa vile sauti yake ilikuwa na lafudhi ngeni ya kutisha.
Uhakika tulio nao ni kwamba Okello alipotokea Raha Leo na mabastola yake, Aboud Jumbe alishtuka na akauliza: "Nani huyu? Katokea wapi?"

Kijana huyo aliyekuwa na umri wa miaka 27 hakujulikana kabla ya Mapinduzi. Alikuwa mtu asiyejua kuandika wala kusoma na akili zake zikimtosha mwenyewe. Hakuwa na sifa za uongozi na wala hakushiriki katika vuguvugu lolote la kisiasa.

Akijibandika cheo cha kijeshi cha Field Marshall ni yeye aliyetangaza kwamba serikali ya ZNP/ZPPP imepinduliwa.
Kwa hakika, kazi hiyo ya kutangaza kufanikiwa kwa Mapinduzi kwanza alipewa Ramadhan Haji, mmoja wa wapinduzi. Lakini alikataa. Jina la Okello lisingelisikika lau Ramadhan Haji angekubali kutangaza kwamba Serikali imepinduliwa na kwamba wapinduzi waliidhibiti nchi.

Waliokuwa wakiongoza mambo Raha Leo tangu Mapinduzi yaanze, hadi Jumatatu Januari 13, walikuwa Aboud Jumbe, mmoja wa viongozi wa chama cha Afro-Shirazi (ASP), Thabit Kombo (Katibu Mkuu wa ASP) na Badawi Qullatein wa Umma Party. Muda wote huo, Sheikh Abeid Amani Karume (kiongozi wa ASP), Abdulrahman Babu (mwenyekiti wa Umma Party) na Abdalla Kassim Hanga (ASP) walikuwa Dar es Salaam.

Mnamo siku hizo hizo liliundwa Baraza la Mapinduzi na Baraza la Mawaziri lililokuwa na mamlaka kamili ya kuiendesha Zanzibar. Mabaraza hayo mawili yalikuwa taasisi kuu za Serikali ya kimapinduzi ya Jamhuri ya Watu wa Zanzibar. Na sio ile iitwayo ‘Kamati ya Watu Kumi na Nne' ambayo baadhi ya watu wanasema kuwa ndiyo iliyoandaa Mapinduzi.

Okello akipenda kujigamba kwamba ndiye aliyeyapanga na kuyaongoza Mapinduzi. Alikuwa akitoa matamshi ya kushtusha na ya ajabu-ajabu kwenye Redio Zanzibar. Kwa mfano, siku moja alidai kwamba alipwe mshahara mkubwa zaidi ya aliokuwa akilipwa Rais Karume. Siku nyingine akasema kwamba kasri zote alizokuwa akitumia sultani kupumzikia apewe yeye.

Kuna siku aliyotoa hukumu kwamba mzee mmoja wa zaidi ya miaka 60 afungwe kwa miaka 99. Alisema kama huyo bwana atakufa gerezani basi mwanawe afungwe ili kuendeleza kifungo na mwanawe akifa basi mjukuu wake afungwe mpaka itimie miaka 99.
Nyakati nyingine aliwaonya watu wazitie moto familia zao na wao wenyewe mpaka wafe ‘kabla ya majeshi yangu kuja.' Alikuwa akitoa vitisho visivyowahi kamwe kusikika Zanzibar.

Kuna siku alitangaza kwamba wakazi wa eneo moja ambako alikuwa apite, wajipange foleni barabarani wakiwa wamevaa chupi tu.
Okello alikuwa ni adha, kitisho, kichekesho na fedheha kwa Zanzibar. Viongozi wapya wa nchi walichoka naye na wakaamua kumchukulia hatua. Salim Rashid, mmoja wa viongozi wa Umma Party aliyekuwa katibu wa Baraza la Mapinduzi anasema kwamba, kwanza alilizungumza suala la Okello na Sheikh Karume. Halafu akalizungumza na Brigadia Yusuf Himid na mwisho yeye, Yusuf Himid na Kanali Ali Mahfoudh wakalitafutia dawa.

Ilisadifu kuwa siku moja Okello alisafiri kwenda Dar es Salaam akifuatana na Jaha Ubwa, aliyekuwa katibu wake. Walipokuwa wanatarajiwa kurudi Zanzibar, Karume, Yusuf Himid, Salim Rashid na Ali Mahfoudh walikwenda uwanja wa ndege kumsubiri.
Siku hiyo anaikumbuka vizuri Luteni Hashil Seif aliyekuwa ofisa wa zamu kwenye kambi ya jeshi huko Migombani karibu na uwanja wa ndege. Alipigiwa simu akitakiwa aende kwa haraka uwanja wa ndege. Hakuambiwa anaitiwa nini.


Alipofika ndipo alipoambiwa kwamba kuna ndege ya Shirika la Ndege la Afrika ya Mashariki iliyokuwa inakuja kutoka Dar es Salaam ndani yake wakiwemo pia Okello na Jaha Ubwa. Akaelezwa kwamba awaruhusu abiria wote pamoja na Ubwa washuke, lakini amzuie Okello asishuke. Halafu amwambie rubani ampeleke Okello Kenya.

Hashil naye akampigia simu komredi mwenzake Luteni Amour Dugheshina kumwita aende uwanja wa ndege amsaidie. Maluteni wote wawili walikuwa na bunduki za aina ya ‘machine gun'.

Ndege ilipotua walipanda ndani ya ndege, wakampokonya silaha Okello na kutekeleza amri waliopewa.
Rubani wa ndege alikasirika sana. ‘Uso wake ulighadhibika, utafikiri mnyama aliyekosewa risasi,' alieleza Hashil.
Lakini rubani hakuwa na la kufanya ila kuiwasha ndege na kuelekea Kenya.

Huku nyuma Salim Rashid akampigia simu Oginga Odinga, Makamu wa Rais wa Kenya, kumuarifu kwamba wamemfukuza Okello na ‘wanamrejesha' Kenya. Alifanya hivyo kwa makosa kwa sababu kutokana na jina lake akifikiri kuwa Okello ni Mjaluo kutoka Kenya.
Kumbe alikuwa mtu wa kabila la Acholi aliyezaliwa Uganda na alikwenda Unguja kabla ya kuhamia Pemba ambako alikuwa mwashi, mtiaji rangi nyumba na mpasuaji mawe.

Swali la kujiuliza hapa ni; je, iwapo kweli Okello alikuwa ‘kiongozi mpendwa wa Mapinduzi' ilikuwaje wafuasi wake na wanamapinduzi wenzake wasimtetee alipoadhiriwa uwanja wa ndege na kufukuzwa nchini? Ilikuwaje akafukuzwa kwa urahisi hivyo?

Kuna uzushi mwingi kuhusu kipindi hiki kifupi cha historia ya Zanzibar. Kwa mfano, kuna filamu ya kubuni ya Wataliana inayoonyesha maiti chungu nzima za watu waliopigwa risasi. Filamu hiyo ilikuwa na lengo moja tu; kuonyesha ‘ukatili na unyama wa Waafrika.'
Hakuna ithibati yoyote kwamba watu waliouawa katika siku za mwanzo za Mapinduzi walifika elfu kumi. Ukweli ni kwamba jumla ya watu waliouawa siku hizo haipindukii 200, katika sehemu za mjini hawazidi 25.

Uzushi mwingine ni kwamba walipelekwa Watanganyika, Zanzibar wakiwa na silaha kwenda kupindua. Na si kweli kwamba Mapinduzi yalikuwa na msisitizo wa kikabila. Katika kipindi cha mwanzo cha Mapinduzi msisitizo ulikuwa wa kitabaka. Nyimbo zilizokuwa zikiimbwa kwenye Redio Zanzibar zikiwazungumzia ‘wakwezi na wakulima' na wafanyakazi kwa jumla na si makabila.

Mapinduzi ya Zanzibar yalianzisha taasisi mpya za utawala zikiwa pamoja na Baraza la Mapinduzi, Baraza la Mawaziri na ofisi ya Rais. Taasisi hizo zilikuwa zifanye kazi kwa muda wa mwaka mmoja tu kwa vile ilikwishaamuliwa kwamba Januari 1965 pafanywe uchaguzi wa kulichagua Bunge la Katiba, lililokuwa litunge Katiba ya kudumu ya Zanzibar.

Baraza la Mapinduzi la Zanzibar pamoja na Serikali mpya zilianza kwa ubia baina ya chama cha ASP na Umma Party. Ingawa wanachama wa ASP ndio waliofanya Mapinduzi waliutambua mchango wa wafuasi wa Umma Party na hasa mchango wa makada wao waliopata mafunzo ya kijeshi nchini Cuba.

Vijana hao wa Umma walizitia wasiwasi serikali za Marekani na Uingereza na kuzifanya ziamini kuwa utawala mpya wa Zanzibar ulikuwa wa ‘kikomunisti'. Dhana hiyo ndiyo iliyosababisha kuchukuliwa hatua ya kuyachimba na kuyagandamiza Mapinduzi ya Zanzibar yaliyodumu kutoka Januari 12, hadi 26 Aprili, mwaka 1964

Ni kwa msingi wa maandishi haya Mohamed Said anaweza kutusaidia kubainisha kwa kuyakubali au kuyakanusha.
Mambo mengi aliyosema kuhusu Nyerere na Tanganyika, mwandishi mwenzake Ahmed Rajab ambaye hana ''doa'' ameyakanusha.

Hapa hakuna bias kwasababu wote ni waislam, na wana hulka ya kuishambulia Tanganyika na Nyerere.
Kwanini jambo hili wametofautiana kiasi cha kutiana madole machoni?

Kuna data zaidi zinakuja.
 
Sijakuwekea masharti ya kujibu, nisichokitpendelea katika mjadala ni nukuu za maandishi yako ambayo tayari nimeyasoma mara nyingi sana, na nimesoma maandiko ya wanazuoni wengine mara nyingi sana.

Mzee Said, ukiangalia maswali niliyokuuliza bado hujajibu, ulichofanya ni kuzunguka. Maswali yapo wazi kabisa.

1. Je,bado unaamini Okello alitumwa kwenda kufanya mapinduzi Zanzibar

2. Je, Nyerere ndiye chanzo cha mapinduzi (Umeongelea wakata mkonge na wamakonde, ningependa utufahamishe endapo Nyerere aliwatuma au walitumwa na mtu mwingine). Nasema hivi ili mbele ya safari tujue tunamjadili nani na siyo kuzunguka zunguka porini kwa kutaja makundi.

Ndugu yangu ni maswali yapi ambayo mimi sijayajibu?
Tafadhali hebu niwekee tena moja baada ya jingine.

Insha Allah nitajitahidi kujibu kama ninayo majibu yake.
 
Wanajamvi, kabla ya kueleza jambo nililokusudia nimeiweka makala hii iliyotoka katika gazeti la Rai Mwema tole 227 la tarehe 22 feb 2012 makusudi kabisa.
Mwandishi wa Makala hii ni Ahmed Rajab ambaye hana tatizo la kidini na Mohamed Said litakalo kwaza mjadala.
Mohamed Said atufahamishe haya yafuatayo

1. Je, naye alifanya mahojiano na Wna mapinduzi kama alivyodai mwenzake Ahmed Rajab
2. Je, anaikubali au kuikataa makala hii kwa ukweli au uongo wake?

Kwanza naanza kwa kumnukuu



Ni kwa msingi wa maandishi haya Mohamed Said anaweza kutusaidia kubainisha kwa kuyakubali au kuyakanusha.
Mambo mengi aliyosema kuhusu Nyerere na Tanganyika, mwandishi mwenzake Ahmed Rajab ambaye hana ''doa'' ameyakanusha.

Hapa hakuna bias kwasababu wote ni waislam, na wana hulka ya kuishambulia Tanganyika na Nyerere.
Kwanini jambo hili wametofautiana kiasi cha kutiana madole machoni?

Kuna data zaidi zinakuja.

Ndugu yangu kuhusu kufanya mahojiano na wanamapinduzi wengine kama alivyofanya Ahmed Rajab mimi nimezungumza na baadhi kama alivyofanya Ahmed Rajab.

Siyakanushi maandishi ya Ahmed Rajab ila ninalosema ni kuwa huo ni upande anojua yeye.
Uko upande mwingine ambao yeye huenda haujui kabisa na kwa kweli si wengi wenye kuujua.

Hadi leo ukiwatajia huo upande mwingine wa mwezi watakanusha.
Mimi naelewa kwa nini wanakanusha.

Ni hulka ya binadamu kuiogopa fedheha au kuikubali aibu ya kusutwa.

Upande huu mwingine ulitakiwa usijulikane kabisa.

Nitakuwekea hapa kwa mukhtasari.

Kuna ''connection'' ya Wayahudi, silaha kutoka Algeria ambazo zilipokelewa Tanganyika, kuna jeshi la mamluki wa Kimakonde kutoka Kipumbwi katika mapinduzi ya Zanzibar.

Nitakufahamisha kitu kimoja.
Hadi kufika asubuhi serikali ya Jamshid ilikuwa ishaangushwa.

Makomredi waliingia siku ya pili asubuhi si wao waliopiga pigo la kwanza.
Waliingia asubuhi kucheza ngoma uwanjani mwali keshatolewa ndani na keshapekekwa kwa mumewe.

Hii ndiyo sababu hadi leo hakuna comrade hata mmoja aliyethubutu kunyanyua kalamu
kuandika kuhusu historia ya mapinduzi ya Zanzibar.

Kwa kumaliza ningependa kusema kuwa naamini hiyo kauli yako ya ''data'' hukukusudia kunitisha na data
bali ni kunogesha maandishi yako.

La ikiwa kusudio ni kuniwekea vitisho vya data ahlan wasaalan.
Mimi naogopa kitu kimoja tu.

Matusi.

Ama kuhusu hilo la Ahmed Rajab kutokuwa na ''doa'' la dini sijui unakusudia nini khasa.
Kuwa hana mapenzi na Uislam au kitu gani?
 
Nianze kwa kuweka sawa msemo ''hana doa''. Hapa nilimaanisha kuwa angeandika mtu mwingine zaidi ya Mwislam basi ingeshakuwa doa ya kuwa anapindisha historia kuwadhulumu waislam. Yeye ni Mwislam kama wengine na wala sikuongelea uumini wake kwasababu nia ya mja anaijua mwenyezi mungu peke yake.

Mohamed, Mzee Nasor Moyo katika mada zake nyingi amekuwa kifanyia reference ''mimi ni mwanapinduzi'' na pale bwawani mwezi oktoba 2012 aliuliza nani anayajua mapinduzi zaidi yake.

Karume alikuwa na kauli za mapinduzi kama ilivyokuwa kwa jumbe, Mwinyi, Salim, Abdul Wakili, Thabiti Kombo Jecha, Aman Karume, Abdallah Natepe n.k.
Swali hapa ni kuwa je, hawa wote walikuwa vibaraka wa Mwalimu Nyerere?
 
Ukristo au uislam vyote tumepokea kutoka kwa waliotutawala. Bahati mbaya waliotawaliwa na tamaduni za kiarabu walitawaliwa mpaka nafsi. Babu zetu walimjua Mungu na walikuwa na taratibu(dini) zao za kumwabudu ila waliposhindwa vita zilitupwa na kuitwa za kishenji. Mungu hakuumba vyote? Wapi manabii na mitume weusi-Acheni kushabikia vya nje!!
ACHA UWONGO na acha miporojo ya kina mikmunisti ya kuuwa dini!
 
Waislamu pambaneni na adui yenu mkubwa (ujinga) a.k.a kutoliona darasa msitafute majibu mepesi kwenye mambo magumu na yamsingi. poor of you!
 
sidhani kama wewe ni kati ya author ambao nyerere alikuwa akiwasoma, hii itakuwa ni kashfa kwa nyerere how can such a genius read fools writings such as yours, disgusting.

Nadhani ''fools writings'' umekusudia ''fool's writings.''

Juu ya kuwa yanaweza kuwa maandishi yangu ni ya ''mwandishi mjinga'' genius lazima ayasome kwanza ndipo atakapoweza kuyahukumu kama ni ya mtu mjinga.

Kukitazama kitabu tu gamba lake hatoweza kujua kilichomo.

Iwe itakavyokuwa.

Kitabu changu kimepata ''review'' mbili ndani ya Cambridge Journal of African History kutoka kwa mabingwa wa historia
ya Afrika - John Iliffe na Jonathon Glassman kutoka Cambridge University na Nortwestern University Chicago.

Haikuishia hapo ikafuatilia na mialiko kadhaa kutoka vyuo vikuu Marekani na Ulaya.
Nimealikwa Nortwestern University kuzungumza na katika wasikizaji na wauliza maswali alikuwa Prof. Jonathon Glassman.

Haikuishia hapo.

Mwaka jana Abdulwahid Sykes akapewa medali kama mpigania uhuru wa Tanganyika
baada ya kusahaulika kwa miaka 50.

Kitabu kimechangia sana katika kumtambua kuwa yeye ndiye chimbuko la TANU.

Bado.
Kitabu kinakwenda toleo la tatu Insha Allah.

Sasa mjinga nani?
Mimi mwandishi au wasomaji wangu?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom