Hali ni tete kwa tuliopoteza ajira, maisha ni magumu familia zetu zinateseka sana. Kapesa kadogo kalikokuwa kanaenda NSSF kwa miaka na miaka nako huwezi kupewa. unatakiwa mpaka ufikishe umri wa miaka 60, ni mlima mrefu huo ukiwa huna kazi.
Wanakuambia watakuwa wanakulipa 33% ya uliokuwa mshahara wako kwa miezi sita, na hilo utasugua miguu ofisi za NSSF mpaka uchakae, hakuna hela. Ni kama vile ni fao hewa.
Hivi kuna nini kimetokea katika shirika hili? hakuna mtu anapenda kupoteza kazi aje kudai hizo hela, kazi katika private sector zinapotea ghafla na bila kutegemea kipindi hiki. Tanzania kwa sasa ajira mpya ni chache sana, ati ukipoteza kazi leo, kesho utapata nyingine.
Inasikitisha na kuumiza nafsi unapoona watoto wako wanarudishwa shule kwasababu umeshindwa kulipa ada, huwezi kumudu hata gharama za matibabu, wakati unapesa mahali. Inamaana gani ktk umri wa miaka 60, upewe pesa, wakati watoto walishakosa shule?
Nikiwa bado na umri wa miaka hii 46, pesa yangu inamaana zaidi kwani naweza kuitumia kuwekeza na ikafaa kwa familia yangu kuliko sasa kubakia huko na mie maisha yangu kubomoka.
Sasa tunaanza kuuza hata thamani tulizozikusanya ilikujikimu, tuoneane huruma basi, mambo ya kusubiri mpaka umri wa miaka 60 libakie kwa watumishi wa umma ambao kazi zao ni za kudumu hata dahali.
Wanakuambia watakuwa wanakulipa 33% ya uliokuwa mshahara wako kwa miezi sita, na hilo utasugua miguu ofisi za NSSF mpaka uchakae, hakuna hela. Ni kama vile ni fao hewa.
Hivi kuna nini kimetokea katika shirika hili? hakuna mtu anapenda kupoteza kazi aje kudai hizo hela, kazi katika private sector zinapotea ghafla na bila kutegemea kipindi hiki. Tanzania kwa sasa ajira mpya ni chache sana, ati ukipoteza kazi leo, kesho utapata nyingine.
Inasikitisha na kuumiza nafsi unapoona watoto wako wanarudishwa shule kwasababu umeshindwa kulipa ada, huwezi kumudu hata gharama za matibabu, wakati unapesa mahali. Inamaana gani ktk umri wa miaka 60, upewe pesa, wakati watoto walishakosa shule?
Nikiwa bado na umri wa miaka hii 46, pesa yangu inamaana zaidi kwani naweza kuitumia kuwekeza na ikafaa kwa familia yangu kuliko sasa kubakia huko na mie maisha yangu kubomoka.
Sasa tunaanza kuuza hata thamani tulizozikusanya ilikujikimu, tuoneane huruma basi, mambo ya kusubiri mpaka umri wa miaka 60 libakie kwa watumishi wa umma ambao kazi zao ni za kudumu hata dahali.